JKCI kushirikiana na chuo kikuu cha New York cha nchini Marekani katika matibabu ya moyo na utafiti wa magonjwa ya moyo

Viongozi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI), Kituo cha Utafiti Ifakara na wenzao wa Chuo Kikuu cha New York kilichopo nchini Marekani wakiwa katika kikao cha kujadili vipaumbele vya mahusiano kati ya JKCI na Chuo hicho kuhusiana na masuala ya utafiti, elimu na utoaji wa huduma kwa wagonjwa wa moyo. 

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge, viongozi wengine wa JKCI na viongozi wa Kituo cha Utafiti Ifakara wakimsikiliza mtaalam wa afya kutoka Chuo Kikuu cha New York kilichopo nchini Marekani akiwaonesha namna ambavyo wanatoa mafunzo kwa wanafunzi wa Udaktari walipotembelea chuo hicho kwaajili ya kujadili maeneo ya kushirikiana katika masuala ya utafiti, elimu na utuoaji wa huduma kwa wagonjwa wa moyo.

Mtaalamu wa afya kutoka Chuo Kikuu cha New York kilichopo nchini Marekani akiwaelezea viongozi kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na wenzao kutoka Kituo cha Utafiti Ifaraka namna ambavyo chuo hicho kinafanya kazi wakati viongozi hao walipotembela katika chuo hicho kujadili maeneo ya kushirikiana katika masuala ya utafiti, elimu na utoaji wa huduma kwa wagonjwa wa moyo.

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge, viongozi wengine wa JKCI na wenzao kutoka Kituo cha Utafiti Ifakara wakitembelea maeneo ya Chuo Kikuu cha New York kilichopo nchini Marekani mara baada ya kikao cha kujadili maeneo ya kushirikiana katika masuala ya utafiti, elimu na utuoaji wa huduma kwa wagonjwa wa moyo.


Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge, viongozi wengine wa JKCI, na wenzao kutoka Kituo cha Utafiti Ifakara wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kikao na viongozi wa Chuo Kikuu cha New York kilichopo nchini Marekani kujadili maeneo ya kushirikiana katika masuala ya utafiti, elimu na utuoaji wa huduma kwa wagonjwa wa moyo.

Picha na: JKCI

*******************************************************************************************************************************

Comments

Popular posts from this blog

Wataalamu wa JKCI kufanya upasuaji wa moyo nchini Zambia

JKCI na AICC Hospitali kutoa huduma za uchunguzi na matibabu ya moyo katika kikao kazi cha wenyeviti na watendaji wakuu wa Taasisi za Umma

JKCI yamshukuru Rais Dkt.Samia kwa kuwapa magari