Posts

Showing posts from June, 2025

JKCI yatoa huduma ya matibabu ya moyo Sabasaba

Image
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akiangalia jinsi Daktari kutoka Hospitali ya JKCI Dar Group Samweli Mbilinyi anavyotoa huduma ya dharura kwa wagonjwa alipotembelea banda la Taasisi hiyo leo katika Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam. Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akizungumza na wataalamu wa afya wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) alipotembelea banda la Hospitali hiyo leo katika Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam. Afisa Uuguzi wa chumba cha uchunguzi na matibabu ya upasuaji mdogo wa moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Flora Kasembe akiwaonesha wananchi waliotembelea banda la Taasisi hiyo betri la moyo (pacemaker) wanalowekewa wagonjwa ambao mapigo ya mioyo yao iko chini ya asilimia 50 wakati wa Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam. Afisa Huduma kwa Wateja wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Anuwarite John akiwa...

Makonda aishukuru JKCI kwa kufanya upimaji wa moyo kwa wakazi wa Arusha

Image
  Daktari Bingwa wa Watoto kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Rose Chengo akimweleza aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha Paul Makonda kuhusu watoto wanaotibiwa katika kambi maalum ya madaktari bingwa na wabobezi wa magonjwa mbalimbali inayofanyika katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid. Aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Paul Makonda akimsalimia mwananchi aliyefika kupata huduma ya uchunguzi na matibabu ya moyo katika banda la Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakati wa    kambi maalum ya madaktari bingwa na wabobezi wa magonjwa mbalimbali inayofanyika katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid. Aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha Paul Makonda akisalimiana na Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Mohamed Aloyce anayetoa huduma za matibabu ya moyo kwa wananchi wa mkoa huo zinazotolewa katika kambi maalum ya madaktari bingwa na wabobezi wa magonjwa mbalimbali inayofanyika katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha. K...

Viongozi wa JKCI watakiwa kuulinda utamaduni wao wa kuwahudumia wagonjwa

Image
Viongozi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakiwa katika picha ya pamoja jana na Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Mhe. Nickson Simon mara baada ya kufungua mafunzo ya siku mbili ya kuwajengea uwezo wa jinsi ya kutekeleza majukumu yao ya kazi viongozi wa taasisi hiyo yanayofanyika katika Shule ya Uongozi ya Mwalimu Julius Nyerere iliyopo wilayani humo. Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Mhe. Nickson Simon akifungua jana mafunzo ya siku mbili ya kuwajengea uwezo wa jinsi ya kutekeleza majukumu yao ya kazi viongozi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) yanayofanyika katika Shule ya Uongozi ya Mwalimu Julius Nyerere iliyopo wilayani humo. Kulia ni Mkurugenzi wa JKCI Dkt. Peter Kisenge. Kanali Mstaafu Joseph Simbakalia akizungumza na baadhi ya viongozi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) mara baada ya kumaliza kuwafundisha mada ya utaifa na uzalendo aliyoitoa katika mafunzo ya siku mbili ya kuwajengea uwezo wa jinsi ya kutekeleza majukumu yao ya kazi yanayofanyika katika Shule ya Uongozi ya Mw...

Mkurungenzi Mtendaji MNH akabidhi ofisi yake ya awali ya JKCI

Image
Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) Dkt. Delilah Kimambo akikabidhi ofisi kwa Kaimu Mkurugenzi wa Tiba Shirikishi  wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Naizihijwa Majani. Kabla ya kuteuliwa kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa MNH Dkt. Delilah alikuwa Mkurugenzi wa Tiba Shirikishi wa JKCI. Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) Dkt. Delilah Kimambo akizungumza na Kaimu Mkurugenzi wa Tiba Shirikishi   wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Naizihijwa Majani. Kabla ya kuteuliwa kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa MNH Dkt. Delilah alikuwa Mkurugenzi wa Tiba Shirikishi wa JKCI. Picha na: JKCI ********************************************************************************************************************

Kambi ya matibabu ya moyo bila malipo yafanyika Arusha

Image
Daktari Bingwa wa watoto wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Rose Chengo akimfanyia kipimo cha kuangalia jinsi moyo unavyofanya kazi mtoto aliyefika kupata huduma ya matibabu ya moyo katika kambi ya maalumu ya madaktari bingwa na wabobezi wa magonjwa mbalimbali iliyoandaliwa na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha inayofanyika katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid. Daktari wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Bertha Massawe akiongea na mkazi wa Arusha kuhusu magonjwa ya moyo wakati wa kambi maalumu ya madaktari bingwa na wabobezi wa magonjwa mbalimbali iliyoandaliwa na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha inayofanyika katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid. Wananchi wa mkoa wa Arusha wakiwa katika foleni ya kusubiri huduma ya matibabu ya moyo kwenye kambi maalumu ya madaktari bingwa na wabobezi wa magonjwa mbalimbali iliyoandaliwa na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa huo inayofanyika katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid. ***************************************************************************************...

Watu 506 wapimwa moyo Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma

Image
Daktari wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dotto Sebastian akiwafundisha jinsi moyo unavyofanya kazi wanafunzi waliotembelea banda la taasisi hiyo kwaajili ya kupata elimu ya magonjwa ya moyo wakati wa Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yaliyomalizika jana katika Viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma. Mtaalamu wa lishe wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Emmanuel Lingindo akitoa elimu ya lishe kwa wananchi waliofika katika banda la taasisi hiyo kwaajili ya kupata huduma za upimaji na matibabu ya moyo zilizokuwa zinatolewa kwenye Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yaliyomalizika jana katika Viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma. Afisa Tawala wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Adila Musa akimweza mwananchi huduma zinazotolewa na taasisi hiyo wakati wa Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yaliyomalizika jana katika Viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma. Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Honoratha Maucky ak...

JKCI yaelezea teknolojia inazozitumia wakati wa Kongamano la Kisayansi la MUHAS

Image
  Mkurugenzi wa Upasuaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Angela Muhozya akimsikiliza Mkuu wa wilaya ya Ubungo Mhe. Albert Msando alipotembelea banda la taasisi hiyo wakati wa Kongamano la 13 la kisanyansi la Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) lililofanyika hivi karibuni katika chuo hicho kampasi ya Mloganzila jijini Dar es Salaam. Mkurugenzi wa Upasuaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Angela Muhozya akimpatia moja ya kipeperushi kinachoelezea huduma zinazotolewa na  Taasisi hiyo Mkuu wa wilaya ya Ubungo Mhe. Albert Msando alipotembelea banda la taasisi hiyo wakati wa Kongamano la 13 la kisanyansi la Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) lililofanyika hivi karibuni katika chuo hicho kampasi ya Mloganzila jijini Dar es Salaam. Mkurugenzi wa Upasuaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Angela Muhozya akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa taasisi hiyo wakati wa Kongamano la 13 la kisanyan...

Wanaume wajitokeza kwa wingi kupima moyo Dodoma

Image
Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Ghati Chacha akimuhudumia mwananchi aliyefika katika banda la taasisi hiyo jana kwa ajili ya kupata huduma za upimaji na matibabu ya moyo  wakati wa Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika katika Viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma.    Afisa Muuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hania Bwahama akitoa elimu ya jinsi moyo unavyofanya kazi kwa mwananchi aliyefika katika banda la taasisi hiyo jana kwa ajili ya kupata elimu ya magonjwa ya moyo na kufahamu huduma zinazotolewa na JKCI wakati wa Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika katika Viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma.    Afisa Muuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Upendo Mwaipopo akimpima shinikizo la damu mkazi wa Dodoma aliyefika katika banda la taasisi hiyo jana kwa ajili ya kupata huduma za upimaji na matibabu ya moyo wakati wa Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi ...

Waziri Mkuu Majaliwa aishauri JKCI kufungua matawi nje ya nchi

Image
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa akimsikiliza Mkurugenzi wa Tiba wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Tatizo Waane alipotembelea banda la Taasisi hiyo wakati wa Mkutano Mkuu wa Chama cha Madaktari Tanzania (MAT) unaofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa (AICC) Arusha. Madaktari bingwa wa magonjwa ya moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakizungumza na wadau wa sekta ya afya waliotembelea banda la Taasisi hiyo wakati wa Mkutano Mkuu wa Chama cha Madaktari Tanzania (MAT) unaofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa (AICC) Arusha. Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa akimpatia zawadi ya picha kutoka Chama cha Madaktari Tanzania (MAT) daktari bora wa mwaka ambaye ni bingwa wa upasuaji wa moyo kwa watoto katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Godwin Sharau leo wakati wa ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Chama cha Madaktari Tanzania (MAT) unaofanyika jijini Arusha. Naib...

Majaliwa atoa wito kwa watoa huduma za afya kuzingatia maadili ya taaluma zao

Image
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa akizungumza na madaktari wakati wa Mkutano Mkuu wa Chama cha Madaktari Tanzania (MAT) unaofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa (AICC) Arusha. ******************************************************************************************** ▪ Asema Serikali imefanya uwekezaji mkubwa kuboresha huduma za afya WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa ametoa wito kwa mabaraza ya kitaaluma, Chama cha Madaktari na  vyama vingine vya kitaaluma kukemea vitendo vilivyo kinyume na maadili ya taaluma na kuchafua taswira ya fani hiyo. Ametoa wito huo leo Jumatano (Juni 18, 2025) alipomwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwenye Mkutano Mkuu wa Chama cha Madaktari Tanzania (MAT) na Kongamano la Kitaifa la Tiba pamoja na maadhimisho ya miaka 60 ya MAT, kwenye ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha, jijini Arusha. ”Wataalamu wote wa afya zingatieni miiko na maadili ya taaluma zenu kwa kutoa huduma bora kwa wan...

Waziri Simbachawene aipongeza JKCI kwa matibabu bure ya moyo Dodoma

Image
Waziri wa nchi, Ofisi ya Rais, Menejiment ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. George Simbachawene akitazama valvu ya moyo wanayowekewa wagonjwa ambao valvu zao hazifanyi kazi vizuri alipotembela banda la Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakati wa Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika katika Viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma. Waziri wa nchi, Ofisi ya Rais, Menejiment ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. George Simbachawene akitazama betri la moyo “Pacemaker” wanalowekewa wagonjwa ambao mapigo yao ya moyo yako chini ya asilimia 50 alipotembela banda la Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakati wa Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika katika Viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma. Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Ghati Chacha akimkabidhi Waziri wa nchi, Ofisi ya Rais, Menejiment ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. George Simbachawene folder lenye taarifa za taasisi hiyo ...

Vijana wa Fountain Gate Academy kupimwa moyo

Image
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya (JKCI) Dkt. Angela Muhozya na Mkurugenzi wa Fountain Gate Sports Academy Japhet Makau wakibadilishana hati ya makubaliano ya kuanzisha na kusimamia programu ya uchunguzi wa magonjwa ya moyo kwa wanamichezo wa Academy hiyo jana wakati wa hafla fupi ya kusaini hati hiyo Jijini Dar es Salaam. Wanafunzi wa shule ya Fountain Gate Academy wakisikiliza wakati wa hafla fupi ya kusaini hati ya makubaliano ya kuanzisha na kusimamia programu ya uchunguzi wa magonjwa ya moyo kwa wanamichezo wa Academy hiyo iliyofanyika katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) jana jijini Dar es Salaam. Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya (JKCI) Dkt. Angela Muhozya na Rais wa Fountain Gate Sports Academy Japhet Makau wakionesha hati ya makubaliano ya kuanzisha na kusimamia programu ya uchunguzi wa magonjwa ya moyo kwa wanamichezo wa Academy hiyo wakati wa hafla fupi ya kusaini hati hiyo iliyofanyika jana Jijini Dar es Salaam. Kaimu Mkurugenzi M...