Vijana wa Fountain Gate Academy kupimwa moyo
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya (JKCI) Dkt. Angela Muhozya na Mkurugenzi wa Fountain Gate Sports Academy Japhet Makau wakibadilishana hati ya makubaliano ya kuanzisha na kusimamia programu ya uchunguzi wa magonjwa ya moyo kwa wanamichezo wa Academy hiyo jana wakati wa hafla fupi ya kusaini hati hiyo Jijini Dar es Salaam.
Kaimu
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya (JKCI) Dkt. Angela Muhozya na
Rais wa Fountain Gate Sports Academy Japhet Makau wakionesha hati ya
makubaliano ya kuanzisha na kusimamia programu ya uchunguzi wa magonjwa ya moyo
kwa wanamichezo wa Academy hiyo wakati wa hafla fupi ya kusaini hati hiyo
iliyofanyika jana Jijini Dar es Salaam.
Kaimu
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya (JKCI) Dkt. Angela Muhozya na
Rais wa Fountain Gate Sports Academy Japhet Makau wakiwa katika picha ya pamoja
na wanafunzi wa Fountain Gate Academy mara baada ya kusaini hati ya makubaliano
ya kuanzisha na kusimamia programu ya uchunguzi wa magonjwa ya moyo kwa
wanamichezo wa Academy hiyo iliofanyika jana Jijini Dar es Salaam.
**************************************************************************************************************
Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI)
kwa kushirikiana na Klabu ya Fountain Gate Academy na Chama cha Madaktari wa
Michezo Tanzania (TMSA) wasaini makubaliano kuanzisha na kusimamia programu ya
uchunguzi wa magonjwa ya moyo kwa wanamichezo wa academy hiyo.
Akizungumza wakati wa kusaini
makubaliano hayo jana jijini Dar es Salaam Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi
ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Angela Muhozya alisema makubaliano hayo
yamelenga kufanya uchunguzi wa awali wa moyo kwa wachezaji wa Fountain Gate FC
pamoja na wanafunzi wa shule 15 zinazomilikiwa na Academy hiyo.
“Makubaliano haya yatatoa fursa kwa
wanafunzi wa Fountain Gate waliopo katika shule 15 zilizopo mikoa mbalimbali ya
Tanzania wanaoshiriki katika shughuli za michezo mbalimbali ikiwemo mpira wa
miguu”, alisema Dkt. Angela
Dkt. Angela alisema mpango huo wa
kuanzisha sports cardiology program inayohusisha pre-participation cardiac
screening kwa wanamichezo ni hatua muhimu katika kuhakikisha usalama wa
wanamichezo nchini.
“Lengo letu ni kubaini mapema
matatizo ya moyo ambayo yanaweza kuwa hatari na yasiyoonekana kwa macho ili
kuyazuia kabla hayajasababisha madhara makubwa”,
“Hii ni pamoja na kuzuia vifo vya
ghafla vya moyo (sudden cardiac death), ambavyo vimekuwa vikishuhudiwa duniani
kote kwa wanamichezo, hata wale waliokuwa wakionekana kuwa na afya njema”,
alisema Dkt. Angela
Kwa upande wake Mkurugenzi wa
Fountain Gate Academy Japhet Makau alisema Taasisi hiyo imepata fursa ya kushirikiana
na JKCI kulinda afya za wachezaji wake na kuwaweka watoto katika mikono salama kwa
kuwafanyia vipimo vya moyo kabla ya kuingia kwenye michezo.
Makau alisema Taasisi yake inaamini
JKCI itaondoa hofu kwa wachezaji wakati wapo uwanjani na kuwajenga vijana
kujiamini hivyo kuongeza nguvu katika michezo yao.
Progamu hiyo mpya na ya kipekee ni
sehemu ya upanuzi wa huduma za kinga inayofanya na JKCI katika jamii, na
kuelekeza nguvu katika kuzuia vifo vya ghafla vya wanamichezo hasa kwa vijana
wanaoshiriki michezo.
Programu hiyo imesainiwa mara baada
ya JKCI kusaini mkataba na Shirika la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) hivi
karibuni wakiwa na lengo la kuwalinda wachezaji na madhara yanayoweza
kujitokeza pindi wanapokuwa uwanjani.
Comments
Post a Comment