Waziri Simbachawene aipongeza JKCI kwa matibabu bure ya moyo Dodoma






Waziri wa nchi, Ofisi ya Rais, Menejiment ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. George Simbachawene akitazama valvu ya moyo wanayowekewa wagonjwa ambao valvu zao hazifanyi kazi vizuri alipotembela banda la Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakati wa Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika katika Viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma.



Waziri wa nchi, Ofisi ya Rais, Menejiment ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. George Simbachawene akitazama betri la moyo “Pacemaker” wanalowekewa wagonjwa ambao mapigo yao ya moyo yako chini ya asilimia 50 alipotembela banda la Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakati wa Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika katika Viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma.



Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Ghati Chacha akimkabidhi Waziri wa nchi, Ofisi ya Rais, Menejiment ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. George Simbachawene folder lenye taarifa za taasisi hiyo  wakati wa Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika katika Viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma.



Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Menejiment ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Juma Mkomi akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) alipotembelea banda la taasisi hiyo wakati wa Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika katika Viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma.



 Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Menejiment ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Juma Mkomi akizungumza na Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Ghati Chacha alipotembelea banda la taasisi hiyo  wakati wa Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika katika Viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma.

*************************************************************************************************************************************************************************************

Waziri wa nchi, Ofisi ya Rais, Menejiment ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. George Simbachawene ameipongeza Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kutoa huduma za upimaji na matibabu ya moyo kwa kuwafuata wananchi mahali walipo.

 

Pongezi hizo amezitoa jana alipotembelea banda la taasisi hiyo wakati wa Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika katika Viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma.

 

Akiwa katika banda la Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete Mhe. Simbachawene aliona huduma za ushauri, upimaji na matibabu ya moyo zinazotolewa kwa wananchi pamoja na vifaa visaidizi vya moyo ambavyo wanawekewa wagonjwa wanaofanyiwa upasuaji na vifaa vinavyotumika katika upasuaji wa moyo.

 

“Ninawapongeza kwa huduma mnayoitoa ya kuokoa maisha ya wananchi wenye shida za moyo, ninawasihi  muendelee na moyo wenu wa kujitoa ili watu wengi zaidi wafikiwe na hudum hii na kupata matibabu mapema”, alisema Mhe. Simbachawene.

 

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Ghati Chacha alisema huduma wanazozitoa katika maonesho hayo ni upimaji wa shinikizo la damu (BP), upimaji wa kiwango cha sukari kwenye damu, upimaji wa uwiano baina ya urefu na uzito, vipimo vya kuangalia jinsi moyo unavyofanya kazi.

 

“Pia tunatoa ushauri wa kiafya kuhusiana na magonjwa ya moyo, elimu ya lishe, elimu ya upasuaji wa moyo, elimu ya upandikizaji wa vifaa visaidizi vya moyo, elimu ya uzibuaji wa mishipa ya damu ya moyo na huduma ya utumishi na utawala”.

 

“Huduma hizi tunazitoa bila malipo yoyote yale, ninawaomba wananchi mtembelee banda letu ili muweze kupata huduma huduma za elimu, ushauri na upimaji wa magonjwa ya moyo”,  alisema Ghati.


Kaulimbiu ya maadhimisho hayo ni “Himiza matumizi ya mifumo ya kidigilali ili kuongeza upatikanaji wa taarifa na kuchagiza uwajibikaji”.


Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) imekuwa ikitoa huduma ya upimaji na matibabu ya moyo bila malipo ijulikanayo kwa jina la Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Outreach Services kwa kuwafuata wananchi mahali walipo ambapo hadi sasa wameshafika zaidi ya mikoa 20 na kuhudumia watu zaidi ya 21,324.

Comments

Popular posts from this blog

JKCI na AICC Hospitali kutoa huduma za uchunguzi na matibabu ya moyo katika kikao kazi cha wenyeviti na watendaji wakuu wa Taasisi za Umma

JKCI yapata tuzo ya taasisi ambayo imetoa mchango wa kipekee kiuchumi na kijamii katika kuleta matokeo makubwa kwa kipindi cha mwaka 2023/2024

Wafanyakazi waliohama JKCI waagwa