JKCI yatoa huduma ya matibabu ya moyo Sabasaba
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI)
Dkt. Peter Kisenge akiangalia jinsi Daktari kutoka Hospitali ya JKCI Dar Group
Samweli Mbilinyi anavyotoa huduma ya dharura kwa wagonjwa alipotembelea banda
la Taasisi hiyo leo katika Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es
Salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akizungumza na wataalamu wa afya wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) alipotembelea banda la Hospitali hiyo leo katika Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam.
Afisa Uuguzi wa chumba cha uchunguzi na matibabu ya upasuaji
mdogo wa moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Flora Kasembe akiwaonesha
wananchi waliotembelea banda la Taasisi hiyo betri la moyo (pacemaker)
wanalowekewa wagonjwa ambao mapigo ya mioyo yao iko chini ya asilimia 50 wakati
wa Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam.
Afisa Huduma kwa Wateja wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete
(JKCI) Anuwarite John akiwaelezea wananchi waliotembelea banda la Taasisi hiyo huduma
zinazotolewa na JKCI wakati wa Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar
es Salaam.
Wananchi wakichagua bidhaa mbalimbali zinazouzwa na Shirika
lisilo la Kiserikali la Heart Team
Africa Foundation (HTAF) kwaajili ya kuchangia matibabu ya moyo kwa watoto
wanaotibiwa katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakati wa Maonesho ya
49 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam.
Picha na: JKCI
*****************************************************************************************************************************
Comments
Post a Comment