Waziri Mkuu Majaliwa aishauri JKCI kufungua matawi nje ya nchi

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa akimsikiliza Mkurugenzi wa Tiba wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Tatizo Waane alipotembelea banda la Taasisi hiyo wakati wa Mkutano Mkuu wa Chama cha Madaktari Tanzania (MAT) unaofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa (AICC) Arusha.

Madaktari bingwa wa magonjwa ya moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakizungumza na wadau wa sekta ya afya waliotembelea banda la Taasisi hiyo wakati wa Mkutano Mkuu wa Chama cha Madaktari Tanzania (MAT) unaofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa (AICC) Arusha.

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa akimpatia zawadi ya picha kutoka Chama cha Madaktari Tanzania (MAT) daktari bora wa mwaka ambaye ni bingwa wa upasuaji wa moyo kwa watoto katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Godwin Sharau leo wakati wa ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Chama cha Madaktari Tanzania (MAT) unaofanyika jijini Arusha.

Naibu Waziri wa Afya Mhe. Godwin Mollel akiwasili katika viwanja vya Kituo cha Mikutano cha Kimataifa (AICC) na kupokelewa na viongozi kutoka Taasisi za Afya wakati wa ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Chama cha Madaktari Tanzania (MAT) unaofanyika jijini Arusha.


Madaktari bingwa wa magonjwa ya moyo na upasuaji wa moyo kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Chama cha Madaktari Tanzania (MAT) uliofanyika leo katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa (AICC) Arusha.

Picha na: JKCI

**********************************************************************************************

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa aishauri Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kuangalia uwezekano wa kufungua matiwi ya Taasisi hiyo nje ya nchi.

Hayo ameyasema leo alipotembelea banda la Taasisi hiyo wakati akimwakilisha Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwenye Mkutano Mkuu wa Chama cha Madaktari Tanzania (MAT) unaofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha, jijini Arusha.

Mhe. Majaliwa alisema JKCI sasa inafanya vizuri na imesaidia kuipunguzia Serikali gharama ya kupeleka wagonjwa wa moyo kutibiwa nje ya nchi kwani sasa huduma nyingi za matibabu ya moyo zinapatikana hapa nchini.

“Hongereni sana kwa huduma nzuri mnayoitoa kwa wagonjwa wa moyo, JKCI sasa ni jicho la nchi katika masuala ya matibabu ya moyo kwa kuimarisha huduma zake na kuwapa unafuu wagonjwa wa moyo kupata huduma kirahisi, angalieni namna ya kupeleka huduma hizi nje ya mipaka ya Tanzania kwa kufungua matawi yenu”, alisema Mhe. Majaliwa

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Tiba kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Tatizo Waane alisema Taasisi hiyo imefanikiwa kufanya tiba utalii kwa kufanya kambi maalumu za matibabu ya moyo katika nchi za Comoro, Malawi na Zambia.

“Taasisi yetu imekuwa ikiwafikia wananchi wengi katika mikoa mbalimbali nchini kwa kufanya kambi maalumu za matibabu ya moyo pia tumeweza kuvuka mipaka ya Tanzania lengo likiwa kuimarisha tiba utalii nchini”, alisema Dkt. Waane

Dkt. Waane alisema Taasisi hiyo pia imeweza kuwasogezea huduma karibu wananchi kwa kufungua matiwi yake maeneo maeneo ya Kawe ili kuwapunguzia msongamano wa kupata huduma za matibabu ya moyo katika eneo moja.

Kwa kipindi cha miaka mnne Taasisi hiyo imeweza kuwapatia matibabu wagonjwa 689 kutoka nje ya nchi zikiwemo nchi za Somalia, Malawi, Kenya, Rwanda, Nigeria, Siera Leon, Zimbambe, Zambia, Uganda, Congo, Ethiopia, Burundi, na wengine kutoka nje ya Afrika katika nchi za Armenia, china, Ujerumani, India, Norway, Ufaransa na Uingereza.


Comments

Popular posts from this blog

JKCI na AICC Hospitali kutoa huduma za uchunguzi na matibabu ya moyo katika kikao kazi cha wenyeviti na watendaji wakuu wa Taasisi za Umma

JKCI yapata tuzo ya taasisi ambayo imetoa mchango wa kipekee kiuchumi na kijamii katika kuleta matokeo makubwa kwa kipindi cha mwaka 2023/2024

Wafanyakazi waliohama JKCI waagwa