Posts

Showing posts from September, 2023

Watu 689 wapimwa moyo Geita

Image
Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Salehe Mwinchete akimpima jinsi moyo unavyofanya kazi (Echocardiograph – ECHO) mwananchi wa Geita aliyefika katika banda la JKCI wakati wa maonyesho ya sita ya kitaifa ya teknolojia ya madini yaliyomalizika leo Mkoani Geita. Jumla ya watu 689 wamepatiwa huduma katika banda hilo. Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) anayetoa huduma katika kliniki maalumu Grace Mbanga akimpima shinikizo la damu mwananchi wa Geita aliyetembelea banda la JKCI wakati wa maonyesho ya sita ya kitaifa ya teknolojia ya madini yaliyomalizika leo Mkoani Geita. Jumla ya watu 689 wamepatiwa huduma katika banda hilo. Afisa kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Elimiliki Kileo akimpima urefu, uzito na uwiano wa urefu na uzito mkazi wa Geita aliyetembelea banda la JKCI wakati wa maonyesho ya sita ya kitaifa ya teknolojia ya madini yaliyomalizika leo Mkoani Geita. Jumla ya watu 689 wamepatiwa huduma katika banda hilo. Wa

Wasemavyo wakazi wa Geita huduma za matibabu ya moyo

Image
Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) anayetoa huduma katika kliniki maalum ya VIP Grace Mbanga akimpima sukari kwenye damu mkazi wa Geita aliyetembelea banda la Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakati wa maonesho ya sita ya kitaifa ya Teknolojia ya Madini yanayofanyika katika viwanja vya EPZA Bombambili mkoani Geita. ************************************************************************************************************** Wananchi wa Mkoa wa Geita wameishukuru Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kufikisha huduma za uchunguzi na matibabu ya magonjwa ya moyo kwa wananchi hao bila gharama. Shukrani hizo zimetolewa na wananchi mbalimbali waliotembelea banda la JKCI lililopo katika maonesho ya sita ya kitaifa ya Teknolojia ya madini yanayoendelea katika viwanja vya EPZA Bombambili mkoani Geita. Akizungumza na mwandishi wa habari hii Donard Francis alisema Taasisi ya JKCI imeonyesha kuwajali watanzania ambao hawakuwa na matarajio ya kuchunguza mioyo yao ku

Idadi ya wagonjwa wa moyo na shinikizo la damu yaongezeka nchini

Image
  Waziri wa Afya Mhe.Ummy Mwalimu akizungumza na wananchi waliohudhuria maadhimisho ya siku ya moyo duniani yaliyofanyika leo katika viwanja vya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group iliyopo Temeke jijini Dar es Salaam. Waziri wa Afya Mhe.Ummy Mwalimu akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kufika katika  viwanja vya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group iliyopo Temeke jijini Dar es Salaam kwaajili ya kushiriki maadhimisho ya siku ya moyo duniani. Waziri wa Afya Mhe.Ummy Mwalimu akikagua maeneo mbalimbali ya  Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group alipofika katika Hospitali hiyo leo  kwaajili ya maadhimisho ya siku ya moyp duniani.    Baadhi ya wananchi waliofika  katika viwanja vya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group iliyopo Temeke jijini Dar es Salaam wakipata huduma za upimaji na matibabu ya magonjwa ya moyo wakati wa maadhimisho ya siku ya moyo duniani. Baadhi   ya wafanyakazi wa Taasisi y

JKCI kutoa huduma bure siku ya moyo Duniani

Image
  Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akizungumza na waandishi wa habari kuhusu maadhimisho ya siku ya moyo duniani yatakayofanyika tarehe 29/09/2023 jijini Dar es Salaam.  ************************************************************************************************************************************************************************************************* Na Aveline Kitomary  KATIKA Kuelekea maadhimisho ya siku ya Moyo Duniani Septemba 29 kila Mwaka Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na Chama cha Madaktari Bingwa wa Moyo Tanzania wanatarajia kutoa huduma za upimaji bure katika Tawi la JKCI la Dar Group Hospital iliyopo jijini Dar es Salaam. Takwimu zinaonesha takribani watu milioni 20 hupoteza maisha Duniani kutokana na magonjwa ya moyo ambapo pia hapa nchini takribani asilimia 13 hupoteza maisha. Akizungumza na Waandishi wa habari leo Jijini Dar es Salaam, Rais wa Chama cha Madaktari Bingwa wa Moyo Tanzania( T

Daktari bingwa wa upasuaji mgumu wa moyo kwa watoto duniani aipongeza Serikali

Image
  Wataalamu wa upasuaji   wa moyo kwa watoto wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na mwenzao kutoka Chuo Kikuu cha Jagiellonian cha nchini Poland Prof.   Tomasz Mroczek wakifanya upasuaji wa kurekebisha mishipa ya damu ya moyo ambayo haijakaa katika mpangilio wake wakati wa kambi maalumu ya siku tano ya matibabu ya magonjwa ya moyo kwa watoto iliyofanyika JKCI. Prof. Mroczek ni mmoja wa madaktari bingwa wachache duniani wanaofanya upasuaji mgumu wa moyo kwa watoto alifika JKCI ili kuona namna ambavyo madaktari wa taasisi hiyo wanavyofanya upasuaji na kuangalia jinsi watakavyoweza kushirikiana katika kufanya upasuaji mgumu zaidi. *********************************************************************************************************************************************************************************************************** Mmoja wa madaktari bingwa wachache duniani wanaofanya upasuaji mgumu wa moyo kwa watoto Prof. Tomasz Mroczek kutoka Chuo Kikuu cha Jagiellonian cha nch

Matibabu ya moyo yatolewa bure kwenye maonesho ya Madini Mkoani Geita

Image
Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Salehe Mwinchete akimpima jinsi moyo unavyofanya kazi (Echocardiograph – ECHO) mkazi wa Geita wakati wa maonesho ya sita ya kimataifa ya Teknolojia ya Madini yanayofanyika katika Viwanja vya EPZA Bombambili mkoani Geita. JKCI inatoa huduma za uchunguzi na matibabu ya magonjwa ya moyo, Sukari kwenye damu na shinikizo la damu katika maonesho hayo.  Wananchi wa Mkoa wa Geita na mikoa ya jirani wakiendelea kupata huduma katika banda la Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakati wa maonesho ya sita ya kimataifa ya Teknolojia ya Madini yanayofanyika katika Viwanja vya EPZA Bombambili mkoani Geita. JKCI inatoa huduma za uchunguzi na matibabu ya magonjwa ya moyo, Sukari kwenye damu na shinikizo la damu katika maonesho hayo. Picha na: JKCI ********************************************************************************************

Upimaji na matibabu ya moyo katika maadhimisho ya siku ya moyo Duniani

Image
  Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group Christine Yonathan akimpima shinikizo la damu (BP) mpiga picha wa kituo cha Televisheni cha ITV Idrissa Magomeni wakati wa kambi maalumu ya matibabu ya siku mbili inayofanyika katika Hospitali hiyo mwanzoni mwa mwezi huu.  ***************************************************************************************************************************************************************************************************************** TAARIFA KWA UMMA UPIMAJI NA MATIBABU YA MAGONJWA YA MOYO KATIKA MAADHIMISHO YA SIKU YA MOYO DUNIANI Katika kuadhimisha siku ya Moyo Duniani tarehe 29/09/2023 yenye kauli mbiu “Tumia Moyo, Kulinda Moyo Wako” wataalamu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na Chama cha Madaktari Bingwa wa Moyo Tanzania (TCS) watatoa huduma ya upimaji na matibabu ya magonjwa ya moyo   kwa wananchi wa Mkoa wa Dar es Salaam na mikoa ya jirani. Upimaji huu utafanyika katika viwanja

Wagonjwa kutoka nje ya nchi wafurahia huduma za matibabu JKCI

Image
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akisikiliza mapigo ya moyo ya mgonjwa kutoka nchini Malawi Anna Kamwaza aliyelazwa katika Taasisi hiyo kwaajili ya kupatiwa matibabu na kuruhusiwa wiki hii baada ya hali yake kuimarika. Mkurugenzi wa Upasuaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Angela Muhozya akifanya maombi ya kumshukuru Mungu kwa kufanikisha matibabu ya mgonjwa kutoka nchini Malawi Anna Kamwaza wakati wa kumpa ruhusa ya kurejea nchini kwake baada ya afya yake kuimarika. Baadhi ya wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wanaofanya kazi katika kliniki ya VIP wakimpatia vipeperushi vinavyoelezea huduma zinazotolewa na Taasisi hiyo mgonjwa kutoka nchini Malawi Anna Kamwaza baada ya kufanyiwa upasuaji wa tundu dogo na kuwekewa kifaa cha kuusaidia moyo kusukuma damu vizuri (Cardiac Resynchronization Therapy Device – CRTD) wakati wa kuruhusiwa mapema wiki hii baada ya hali yake kuimarika. Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo

Watoto 439 wamefanyiwa upasuaji wa moyo na Kituo cha Mfalme Salman cha Misaada ya Kibinadamu

Image
Balozi wa Saudi Arabia nchini Tanzania Mhe. Yahya Ahmed Okeish akimjulia hali mtoto aliyepatiwa matibabu katika kambi maalum ya upasuaji wa moyo kwa watoto inayofanywa na wataalamu wa afya wa JKCI kwa kushirikiana na wenzao kutoka kituo cha Mfalme Salman cha Misaada ya Kibinadamu kutoka nchini Saudi Arabia wakati wa ziara yake kutembelea kambi hiyo leo jijini Dar es Salaam Balozi wa Saudi Arabia nchini Tanzania Mhe. Yahya Ahmed Okeish akisalimiana na madaktari bingwa wa upasuaji wa moyo kutoka kituo cha Mfalme Salman cha Misaada ya Kibinadamu kutoka nchini Saudi Arabia wakati wa ziara yake kutembelea kambi maalum ya matibabu ya moyo kwa watoto inayofanywa na watalamu wa afya kutoka Saudi Arabia na wenzao wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) leo jijini Dar es Salaam Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akitembelea moja ya chumba cha upasuaji wa moyo kuangalia huduma zinavyoendelea wakati wa kambi maalum ya matibabu ya moyo inayofanywa na

Watoto 24 wafanyiwa upasuaji wa moyo katika kambi ya matibabu inayoendelea JKCI

Image
Madaktari bingwa wa upasuaji wa moyo na mishipa ya damu kwa watoto wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakishirikiana na mwenzao kutoka Kituo cha Mfalme Salman cha Misaada ya Kibinadamu kilichopo nchini Saudi Arabia Mohammed Shihata kumfanyia upasuaji wa kurekebisha mishipa ya damu mtoto ambaye mishipa yake ya damu haipo katika mpangilio wake wakati wa kambi maalum ya siku tano ya matibabu ya magonjwa ya moyo kwa watoto inayoendelea JKCI. Mtaalamu wa kuendesha mashine ya kuusaidia moyo na mapafu kufanya kazi (Heart Lung Machine) wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Robert Luchemba na mwenzake kutoka Kituo cha Mfalme Salman cha Misaada ya Kibinadamu kilichopo nchini Saudi Arabia wakiendesha mashine hiyo wakati wa kambi maalum ya siku tano ya matibabu ya moyo kwa watoto inayofanyika JKCI. Daktari bingwa wa usingizi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Steven Nandi akiweka sawa mashine ya kuangalia mapigo ya moyo ya mgonjwa (monitor) wakati wa kambi maalum ya upasuaji wa moyo