Kikao cha Bodi ya Wadhamini ya JKCI chafanyika Dar es Salaam
Mkurugenzi wa Tiba Shirikishi wa Taasisi ya Moyo
Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Delilah
Kimambo akiwaeleza wajumbe wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi hiyo upatikanaji wa
damu kwa wagonjwa wanaofanyiwa upasuaji wa moyo wakati wa kikao cha nne cha
Bodi hiyo kilichofanyika jana jijini Dar
es Salaam.
Mjumbe wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) ambaye pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili Prof. Mohamed Janabi akichangia mada wakati wa kikao cha nne cha Bodi hiyo kilichofanyika jana jijini Dar es Salaam.
Mjumbe wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) ambaye pia ni Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) Prof. Appolinary Kamuhabwa akichangia mada wakati wa kikao cha nne cha Bodi hiyo kilichofanyika jana jijini Dar es Salaam.
Mjumbe wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Mhe. Balozi Mwanaidi Sinare akichangia mada wakati wa kikao cha nne cha Bodi hiyo kilichofanyika jana jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya Viongozi wa Menejimenti ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakimsikiliza Kaimu Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi hiyo Asha Izina wakati wa kikao cha nne cha bodi hiyo kilichofanyika jana jijini Dar es Salaam.
Comments
Post a Comment