JKCI kutoa huduma bure siku ya moyo Duniani

 


Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akizungumza na waandishi wa habari kuhusu maadhimisho ya siku ya moyo duniani yatakayofanyika tarehe 29/09/2023 jijini Dar es Salaam. 

*************************************************************************************************************************************************************************************************
Na Aveline Kitomary 
KATIKA Kuelekea maadhimisho ya siku ya Moyo Duniani Septemba 29 kila Mwaka Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na Chama cha Madaktari Bingwa wa Moyo Tanzania wanatarajia kutoa huduma za upimaji bure katika Tawi la JKCI la Dar Group Hospital iliyopo jijini Dar es Salaam.

Takwimu zinaonesha takribani watu milioni 20 hupoteza maisha Duniani kutokana na magonjwa ya moyo ambapo pia hapa nchini takribani asilimia 13 hupoteza maisha.

Akizungumza na Waandishi wa habari leo Jijini Dar es Salaam, Rais wa Chama cha Madaktari Bingwa wa Moyo Tanzania( TCS) ,Dk Roberth Mvungi amesema kambi maalum ya matibabu itakayohusisha uchunguzi na utambulishi wa kujua viashiria vya magonjwa ya moyo itafanyika kwa siku mbili Septemba 29 hadi 30,2023.

"Nchi yetu imepiga hatua sana katika matibabu ya moyo na chama kimeona ni heri kushirikiana na wadau wakubwa ambao wamehusika kubadilisha hadhi ya Tanzania katika kutibu na kukinga magonjwa ya moyo,"aneeleza.

Amesema kutakuwa na matembezi ambayo yataanza saa 12:00 asubuhi siku ya Septemba 30.

"Tutafanya uchunguzi wa afya Dar group Hospital watu wote wanakaribishwa kuangalia na kutambua afya yao na tuna matembezi maalum tutatembea kutoka uwanja wa uhuru Chang'ombe Temeke hadi Tazara Dar Group.

Alifafanua kuwa asilimia 80 ya magonjwa ya moyo yananikingika endapo ushauri wa wataaamu utafatwa.

Kauli mbiu "Tumia moyo, kulinda moyo wako".

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) Dk Peter Kisenge amesema Kwa kushirikiana na chama kwa pamoja wanaadhimisha siku ya moyo Duniani ambapo watapima wagonjwa matatizo ya moyo ambapo aliwaomba wananchi watoke majumbani mwao kuja kupima magonjwa ya moyo.

"Serikali imejikita kuimarisha afya tuna vifaa vya kisasa tutapima,madakatari bingwa watakuwepo hivyo wananchi wajitokeze unapokuja mapema utapata matibabu mapema hautatumia graharama na vipimo vitafanyika hadi siku ya Jumamosi na mazoezi yatafanyika ni muhimu mazoezi kufanyika kwa wakati ili kujikinga,"amesisitiza Dk Kisenge.

Amesema watapima kisukari,uzito na pia watatoa elimu ya lishe na wataaamu watakuwepo na watawaeleza madhara ya sigara na unywaji pombe uliokithiri.

Amesema mgeni rasmi katika maadhimisho hayo atakuwa mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Albert Chalamila.

Comments

Popular posts from this blog

Wataalamu wa JKCI kufanya upasuaji wa moyo nchini Zambia

JKCI na AICC Hospitali kutoa huduma za uchunguzi na matibabu ya moyo katika kikao kazi cha wenyeviti na watendaji wakuu wa Taasisi za Umma

JKCI yamshukuru Rais Dkt.Samia kwa kuwapa magari