Wafanyakazi wa JKCI wapatiwa mafunzo ya namna ya kutumia mfumo wa manunuzi wa NeST
Mkuu
wa Kitengo cha Ununuzi na Ugavi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Bunare
Daniel akiwafundisha wafanyakazi wa Taasisi hiyo namna ya kutumia mfumo mpya wa
kielektroniki wa manunuzi ya Umma (NeST) wakati wa kikao cha wafanyakazi hao
hivi karibuni katika ukumbi wa Taasisi hiyo.
Mkuu wa Kitengo cha Ununuzi na Ugavi wa Taasisi ya Moyo
Jakaya Kikwete (JKCI) Bunare Daniel akimuelekeza kwa vitendo namna ya kutumia
mfumo mpya wa kielektroniki wa manunuzi ya Umma (NeST) Afisa Uuguzi wa Taasisi
hiyo Salma Wibonela wakati wa kikao cha wafanyakazi hao hivi karibuni katika
ukumbi wa Taasisi hiyo.
Baadhi ya wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete
(JKCI) wakisikiliza wakati wa mafunzo ya namna ya kutumia mfumo mpya wa
kielektroniki wa manunuzi ya Umma (NeST) hivi karibuni katika ukumbi wa Taasisi
hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam.
Comments
Post a Comment