Posts

Showing posts from November, 2023

Bulembo aipongeza JKCI kupeleka vipimo waliko wananchi

Image
  Mkuu wa Wilaya ya   Kigamboni Mhe. Halima Bulembo akimsalimia mwananchi aliyefika katika Hospitali ya Wilaya hiyo kwaajili ya kupata huduma ya uchunguzi na matibabu ya moyo zinazotolewa na wataalamu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na wenzao wa Kigamboni. Kulia ni Mkurugenzi wa Hospitali ya JKCI Dar Group Dkt. Tulizo Shemu. Mkuu wa Wilaya ya  Kigamboni Mhe. Halima Bulembo akiwasili katika viwanja vya Hospitali ya wilaya hiyo kwaajili ya kuangalia huduma za upimaji na matibabu ya moyo zinatolewa na wataalamu ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na wenzao wa Hospitali hiyo.  Kulia kwa Mkuu wa Wilaya ni Mkurugenzi wa Hospitali ya JKCI Dar Group Dkt. Tulizo Shemu. Mkuu wa Wilaya ya     Kigamboni Mhe. Halima Bulembo akipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi wa Hospitali ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dar Group Dkt. Tulizo Shemu kuhusu kambi maalumu ya upimaji na matiababu ya moyo inayofanywa na wataamu wa JKCI kwa kushirikiana na wenzao

Matibabu ya moyo kuimarishwa

Image
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akizungumza na wageni kutoka Hospitali ya Jimbo la Shandong iliyopo nchini China walipotembelea JKCI jana kwaajili ya kuangalia huduma zinazotolewa na kujadiliana maeneo ya kushirikiana. Mkurugenzi wa Idara ya Tiba kutoka Hospitali ya Jimbo la Shandong Dkt. Mali Xin akielezea namna ambavyo China imejipanga kushirikiana na JKCI kutoa huduma za kibingwa wakati wajumbe kutoka Hospitali ya Jimbo la Shandong iliyopo nchini China walipotembelea JKCI jana na kukutana na uongozi wa Taasisi hiyo. Baadhi ya wajumbe kutoka Hospitali ya Jimbo la Shandong iliyopo nchini China wakisikiliza wakati wa kikao na viongozi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kujadili maeneo ya kushirikiana katika kuboresha huduma za matibabu ya moyo nchini jana katika Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam. Baadhi ya wajumbe kutoka Hospitali ya Jimbo la Shandong iliyopo nchini China wakitembelea maeneo ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete

JKCI yakutana na wazabuni wake

Image
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akizungumza na  wazabuni  wa huduma na bidhaa  wa Taasisi hiyo    wakati wa kikao cha kuimarisha uhusiano na kufahamu changamoto mbalimbali zinazowakabili    kilichofanyika leo katika ukumbi wa mikutano wa Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam. Mkurugenzi wa Tiba Shirikishi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Delilah Kimambo akielezea namna ambavyo Idara yake inafanya kazi na waagizaji na wasambazaji wa dawa za binadamu na vifaa tiba     wakati wa kikao cha kuimarisha uhusiano na kufahamu changamoto mbalimbali zinazowakabili  wazabuni  wa huduma na bidhaa  wa Taasisi hiyo kilichofanyika leo katika ukumbi wa mikutano wa JKCI uliopo jijini Dar es Salaam. Mkuu wa Kitengo cha Ununuzi na Ugavi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Daniel Bunare akijibu hoja zilizotolewa na  wazabuni wa huduma na bidhaa  wa Taasisi hiyo      wakati wa kikao cha kuimarisha uhusiano na kufahamu changamoto mbalimbal

JKCI: Kigamboni njooni kupima moyo

Image
Daktari wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Samwel George na mwenzake wa Hospitali ya wilaya Kigamboni Ally Kumbuka wakimsikiliza mwananchi aliyefika katika hospitali ya Kigamboni kwaajili ya kupata huduma za upimaji na matibabu ya moyo. Wataalamu wa JKCI na wenzao wa Kigamboni wanafanya kambi maalumu ya matibabu ya moyo ya siku tano kwa wananchi wa wilaya hiyo. Mtafiti wa Taasisi ya Moyo jakaya Kikwete (JKCI) Saad Kamtoi akichukuwa taarifa za mwananchi aliyefika katika Hospitali ya wilaya Kigamboni kwaajili ya kupata huduma za upimaji na matibabu ya moyo.Wataalamu wa JKCI na wenzao wa Kigamboni wanafanya kambi maalumu ya matibabu ya moyo ya siku tano kwa wananchi wa wilaya hiyo.     Mwakilishi wa kampuni ya uingizaji na usambazaji wa dawa za binadamu ya Micro Labs Ltd Festus Asenga akimpatia dawa za kupunguza mafuta mwilini mwananchi aliyefika katika Hospitali ya wilaya Kigamboni kwaajili ya kupata huduma za upimaji na matibabu ya moyo. Kampuni ya uingizaji na usambaz

Magonjwa ya kinywa, meno na njia ya hewa tishio matatizo ya valvu za moyo

Image
 Madaktari bingwa wa upasuaji wa moyo na mishipa ya damu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na wenzao kutoka Shirika la Open Heart International (OHI) lililopo nchini Australia wakimfanyia mgonjwa upasuaji wa kupandikiza valvu ya moyo wakati wa kambi maalumu ya siku sita iliyomalizika leo katika Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam. Jumla ya wagonjwa 25 watoto 16 na watu wazima tisa walifanyiwa upasuaji katika kambi hiyo. Mtaalamu wa kuendesha mashine ya kuusaidia moyo na mapafu kufanya kazi (Heart Lung Machine) wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Lujani Hoho akiendesha mashine hiyo wakati wa kambi maalumu ya siku sita inayofanywa na wataalamu wa afya wa JKCI kwa kushirikiana na wenzao kutoka Shirika la Open Heart International (OHI) la nchini Australia. *************************************************************************************************************************************************************************************************************************

Dkt. Kisenge: Waleteni Wagonjwa wa moyo kutibiwa JKCI; Msiwapeleke nje ya nchi

Image
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akizungumza na waandishi wa habari katika kambi maalumu ya upasuaji wa moyo  inayofanywa na wataalamu wa JKCI kwa kushirikiana na wenzao kutoka Shirika la Open Heart International la nchini Australia. *********************************************************************************************************************************************************************************************** Madaktari nchini wameombwa kuwapeleka wagonjwa wenye matatizo ya moyo   katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwaajili ya matibabu na siyo nje ya nchi kwani Serikali imewekeza vya kutosha katika vifaa tiba na rasilimali watu.   Ombi hilo limetolewa leo jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge wakati akizungumza na waandishi wa habari kwenye kambi maalumu ya upasuaji wa moyo inayofanywa na wataalamu wa JKCI kwa kushirikiana na wenzao kutoka Shirika la

Wakumbushwa madhara ya kutoa na kupokea rushwa

Image
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akitoa neno la shukrani kwa niaba ya wafanyakazi wa Taasisi hiyo mara baada ya kupata mafunzo ya kuzuia rushwa eneo la kazi. Mafunzo hayo yametolewa leo jijini Dar es Salaam na     Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU). Mkuu wa uendeshaji umma kutoka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Nerry Mwakyusa akiwafundisha wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) madhara ya kutoa na kupokea rushwa kutoka kwa wananchi wanaopata huduma    katika Taasisi hiyo iliyopo    jijini Dar es Salaam. Baadhi ya wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakifuatilia mafunzo ya kuzuia na kupambana na rushwa eneo la kazi yaliyotolewa leo jijini Dar es Salaam na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU).

JKCI kufanya upimaji na matibabu ya moyo wilayani Kigamboni

Image
  Afisa Utafiti na Mafunzo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Saad Kamtoi akichukuwa taarifa za mwananchi aliyefika JKCI hospitali ya Dar Group kwaajili ya upimaji na matibabu ya moyo wakati wa maadhimisho ya siku ya moyo Duniani yaliyofanyika mwishoni mwa mwezi Septemba mwaka huu jijini Dar es Salaam. ************************************************************************************************************************************************************************************ Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na Hospitali ya Wilaya ya   Kigamboni tutatoa huduma za tiba mkoba zinazojulikana kwa   jina la   Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Outreach Services kwa kufanya upimaji na matibabu ya magonjwa ya moyo kwa wananchi wa Mkoa wa Dar es Salaam na Mikoa ya jirani. Upimaji huu utafanyika kwa watoto na watu wazima kuanzia tarehe 27/11/2023 hadi tarehe 01/12/2023  saa mbili kamili asubuhi mpaka saa 10 kamili jioni katika Viwanja vya Hospitali ya Wilaya Kigamboni

20 kufanyiwa upasuaji wa moyo

Image
  Madaktari bingwa wa magonjwa ya moyo na mishipa ya damu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakishirikiana na wenzao kutoka shirika la Open Heart International (OHI) lililopo nchini Australia kumfanyia upasuaji wa kufungua mlango wa moyo wa chini kushoto ulikuwa umeziba na kutopitisha damu vizuri mgonjwa mwenye matatizo ya valvu wakati wa kambi maalumu ya siku 4 iliyoanza leo katika Taasisi hiyo. Jumla ya watu wazima 10 watafanyiwa upasuaji katika kambi hiyo inayotoa huduma za matibabu pamoja na mafunzo kwa wataalamu wa afya wa JKCI. Madaktari bingwa wa magonjwa ya moyo kwa watoto wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakishirikiana na wenzao kutoka Shirila la Open Heart International (OHI) lililopo nchini Australia kuziba tundu na kufungua mishipa ya damu iliyoziba (tof repair) wakati wa kambi maalumu ya siku 4 iliyoanza leo katika Taasisi hiyo. Jumla ya watoto 10 watafanyiwa upasuaji katika kambi hiyo inayotoa huduma za matibabu pamoja na mafunzo kwa wataalamu wa afya wa JK

Wagojwa 32,867 watibiwa moyo JKCI kwa kipindi cha miezi mitatu

Image
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akizungumza na wafanyakazi wa Taasisi hiyo wakati wa kikao cha kutoa taarifa ya utendaji kazi kwa kipindi cha miezi mitatu ya Julai hadi Oktoba 2023 kilichofanyika leo katika ukumbi wa Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam. Wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakifuatilia taarifa zilizokuwa zikitolewa wakati wa kikao cha Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi hiyo na wafanyakazi kutoa taarifa ya utendaji kazi kwa kipindi cha miezi mitatu ya Julai hadi Oktoba 2023 kilichofanyika leo katika ukumbi wa Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam. Daktari bingwa wa usingizi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Mhe. Balozi Ulisubisya Mpoki akielezea maendeleo ya Taasisi hiyo tangu kuanzishwa wakati wa kikao cha Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi hiyo na wafanyakazi kutoa taarifa ya utendaji kazi kwa kipindi cha miezi mitatu ya Julai hadi Oktoba 2023 kilichofanyika leo katika ukumbi wa Taasisi hiyo iliy

Wafanyakazi wa JKCI wafundishwa jinsi ya kutumia mfumo wa ununuzi wa umma kwa njia ya mtandao – NeST

Image
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akizungumza na wafanyakazi wa Taasisi hiyo wanaoshiriki mafunzo ya siku tano ya mfumo wa ununuzi wa umma kwa njia ya mtandao – NeST yanayofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Ununuzi na Ugavi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Bunare Daniel. Mkuu wa Kitengo cha Ununuzi na Ugavi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Bunare Daniel akizungumza na wafanyakazi wa Taasisi hiyo wanaoshiriki mafunzo ya siku tano ya mfumo wa ununuzi wa umma kwa njia ya mtandao – NeST yanayofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge. Mkufunzi kutoka Mamlaka ya Kudhibiti Ununuzi wa Umma (PPRA) Furael Lema Furael Lema akiwafundisha wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kuhusu mfumo wa ununuzi wa umma kwa njia ya m