Wataalamu wa JKCI wawasilisha utafiti walioufanya katika mkutano wa Kimataifa wa Kisayansi wa Magonjwa yasiyoambukiza

Mkuu wa Kitengo cha Utafiti na Mafunzo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Pedro Pallangyo akiwasilisha taarifa ya utafiti alioufanya kuhusu wanawake wanaopata magonjwa ya moyo kutanuka na kushindwa kufanya kazi kutokana na uzazi (Peripartum Cardiomyopathy) wakati wa mkutano wa kimataifa wa kisayansi wa magonjwa yasiyoambukiza unaofanyika katika ukumbi wa kimataifa wa mikutano wa Julius Nyerere.

Mtafiti kutoka Kituo cha Utafiti Ifakara anayeshirikiana na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Neema Kailembo akiwasilisha taarifa ya utafiti alioufanya wa matokeo ya awali yaliyogawanya makundi tofauti ya viashiria hatarishi vinavyosababisha mishipa ya damu kwenye moyo kuziba wakati wa mkutano wa kimataifa wa kisayansi wa magonjwa yasiyoambukiza unaofanyika katika ukumbi wa kimataifa wa mikutano wa Julius Nyerere.

Wataalamu wa afya kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Janeth Mmari na Neema Kailembo wakimsikiliza mtaalamu wa afya kutoka Hospitali ya Kilimanjaro Christian Medical Centre (KCMC) alipokuwa akiwaelezea kuhusu utafiti ulioufanyika KCMC kuhusu ugonjwa wa kiharusi  wakati wa mkutano wa kimataifa wa kisayansi wa magonjwa yasiyoambukiza unaofanyika katika ukumbi wa kimataifa wa mikutano wa Julius Nyerere.


Baadhi ya watafiti kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na  Kituo cha Utafiti Ifakara wakifuatilia mada zilizokuwa zikitolewa katika mkutano wa kimataifa wa kisayansi wa magonjwa yasiyoambukiza unaofanyika katika ukumbi wa kimataifa wa mikutano wa Julius Nyerere.

Comments

Popular posts from this blog

Wataalamu wa JKCI kufanya upasuaji wa moyo nchini Zambia

JKCI na AICC Hospitali kutoa huduma za uchunguzi na matibabu ya moyo katika kikao kazi cha wenyeviti na watendaji wakuu wa Taasisi za Umma

JKCI yamshukuru Rais Dkt.Samia kwa kuwapa magari