JKCI kufanya upimaji na matibabu ya moyo wilayani Kigamboni
************************************************************************************************************************************************************************************
Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na Hospitali ya Wilaya ya Kigamboni tutatoa huduma za tiba mkoba zinazojulikana kwa jina la Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Outreach Services kwa kufanya upimaji na matibabu ya magonjwa ya moyo kwa wananchi wa Mkoa wa Dar es Salaam na Mikoa ya jirani.
Upimaji huu utafanyika kwa watoto na watu wazima kuanzia tarehe 27/11/2023 hadi tarehe 01/12/2023 saa mbili kamili asubuhi mpaka saa 10 kamili jioni katika Viwanja vya Hospitali ya Wilaya Kigamboni iliyopo eneo la Gezaulole.
Kutakuwa na madaktari bingwa wa moyo watakaoambatana na wataalamu wa lishe ambao watatoa elimu ya lishe bora itakayowapa wananchi uelewa wa kufuata mtindo bora wa maisha utakaowasaidia kuepukana na magonjwa yasiyoambukiza yakiwemo ya moyo ambayo yanaweza kuepukika kwa kufuata ushauri wa kitaalamu.
Watakaogundulika kuwa na matatizo ya moyo watafanyiwa uchunguzi zaidi na kupatiwa matibabu hapohapo au kupewa rufaa ya kuja kutibiwa katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) iliyopo Upanga jijini Dar es Salaam.
Comments
Post a Comment