Wafanyakazi wa JKCI wafundishwa jinsi ya kutumia mfumo wa ununuzi wa umma kwa njia ya mtandao – NeST
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akizungumza na wafanyakazi wa Taasisi hiyo wanaoshiriki mafunzo ya siku tano ya mfumo wa ununuzi wa umma kwa njia ya mtandao – NeST yanayofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Ununuzi na Ugavi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Bunare Daniel.
Mkufunzi kutoka Mamlaka ya Kudhibiti Ununuzi wa Umma (PPRA) Furael Lema Furael Lema akiwafundisha wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kuhusu mfumo wa ununuzi wa umma kwa njia ya mtandao – NeST. Mafunzo hayo ya siku tano yanayofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam.
Mkufunzi kutoka Mamlaka ya Kudhibiti Ununuzi wa
Umma (PPRA) Furael Lema akiwaelekeza kwa kutumia simu ya mkononi na kompyuta
ndogo baadhi ya wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wanaoshiriki
mafunzo ya mfumo wa ununuzi wa umma kwa njia ya mtandao – NeST jinsi ya kutumia
mfumo huo. Mafunzo hayo ya siku tano yanafanyika katika ukumbi wa mikutano wa
Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam.
Wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wanaoshiriki mafunzo ya mfumo wa ununuzi wa umma kwa njia ya mtandao – NeST wakijifunza kwa njia ya vitendo kwa kutumia simu za mkononi na kompyuta ndogo jinsi ya kuingiza manunuzi katika mfumo huo. Mafunzo hayo ya siku tano yanafanyika katika ukumbi wa mikutano wa Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam.
Comments
Post a Comment