JKCI yakutana na wazabuni wake



Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akizungumza na wazabuni  wa huduma na bidhaa wa Taasisi hiyo  wakati wa kikao cha kuimarisha uhusiano na kufahamu changamoto mbalimbali zinazowakabili  kilichofanyika leo katika ukumbi wa mikutano wa Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi wa Tiba Shirikishi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Delilah Kimambo akielezea namna ambavyo Idara yake inafanya kazi na waagizaji na wasambazaji wa dawa za binadamu na vifaa tiba  wakati wa kikao cha kuimarisha uhusiano na kufahamu changamoto mbalimbali zinazowakabili wazabuni  wa huduma na bidhaa wa Taasisi hiyo kilichofanyika leo katika ukumbi wa mikutano wa JKCI uliopo jijini Dar es Salaam.

Mkuu wa Kitengo cha Ununuzi na Ugavi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Daniel Bunare akijibu hoja zilizotolewa na wazabuni wa huduma na bidhaa wa Taasisi hiyo   wakati wa kikao cha kuimarisha uhusiano na kufahamu changamoto mbalimbali zinazowakabili washitiri hao kilichofanyika leo katika ukumbi wa mikutano wa JKCI uliopo jijini Dar es Salaam.


Mwakilishi kutoka kampuni ya uagizaji na usambazaji wa dawa za binadamu ya Macnaughton Ltd Hawa Kazema akitoa maoni yake wakati wa kikao cha kuimarisha uhusiano na kufahamu changamoto mbalimbali zinazowakabili wazabuni na watoa huduma wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI)  kilichofanyika leo katika ukumbi wa mikutano wa Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam.


Mwakilishi kutoka kampuni ya uagizaji na usambazaji wa dawa za binadamu ya Gama Pharmaceutical Ltd Qutibah Salah akielezea changamoto zinazokwamisha upatikanaji wa dawa wakati wa kikao cha kuimarisha uhusiano na kufahamu changamoto mbalimbali zinazowakabili wazabuni wa huduma na bidhaa wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI)  kilichofanyika leo katika ukumbi wa mikutano wa Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam.


Mwakilishi kutoka kampuni ya uagizaji na usambazaji wa vifaa tiba ya Computech Ltd Sandip Datta akichangia mada wakati wa kikao cha kuimarisha uhusiano na kufahamu changamoto mbalimbali zinazowakabili wazabuni  wa huduma na bidhaa wa Taasisi hiyo kilichofanyika leo katika ukumbi wa mikutano wa JKCI uliopo jijini Dar es Salaam.


Mwakilishi kutoka kampuni ya usafi ya Care Sanitation na Suppliers Ltd Romana Mvungi akielezea namna kampuni hiyo inavyofanya kazi na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakati wa kikao cha kuimarisha uhusiano na kufahamu changamoto mbalimbali zinazowakabili wazabuni wa huduma na bidhaa wa Taasisi hiyo kilichofanyika leo katika ukumbi wa mikutano wa JKCI uliopo jijini Dar es Salaam.

*******************************************************************************************************************************************************************************************

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge amewaomba wazabuni  wa huduma na bidhaa  wa Taasisi hiyo  kushirikiana kwa pamoja  ili kuhakikisha wagonjwa  wanapata huduma bora na kwa wakati.

Dkt. Kisenge  ametoa ombi hilo leo wakati wa kikao chake na wazabuni wa huduma na bidhaa  kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam.

Dk. Kisenge alisema ili kuhakikisha dira ya Taasisi hiyo ambayo ni kuwa Taasisi yenye ubora wa kimataifa katika utoaji wa matibabu ya moyo, mafunzo na utafiti inafanikiwa ushirikiano wa pamoja unahitajika baina ya JKCI na wadau wake.

“Tukifanya kazi kwa pamoja tutatimiza dira ya JKCI, jukumu letu sisi ni kuhakikisha tunawalipa kwa wakati na jukumu lenu ni kuhakikisha mnaleta vifaa tiba na kutoa huduma iliyo bora na kwa wakati lakini kama kila mtu atashindwa kutimiza wajibu wake hatutaweza kufikia dira ya Taasisi”,.

“Zabuni za manunuzi ya vifaa na huduma  katika Taasisi yetu zinatangazwa kupitia mfumo wa ununuzi wa umma kwa njia ya mtandao - NeST kwa uwazi na kwa wakati, ni jukumu lenu kujisajili huko na kuhakikisha mmeomba na ikitokea mmeshindwa jinsi ya kuomba ombeni msaada kutoka ofisi ya manunuzi na ugavi  ili wawaelekeze”, alisema Dkt. Kisenge.

Mkurugenzi huyo Mtendaji ambaye pia ni daktari bingwa wa moyo aliwasihi washitiri hao badala ya kuagiza dawa za binadamu pamoja na vifaa  tiba nje ya nchi wajenge viwanda hapa nchini ili kurahisisha kupatikana kwa vifaa hivyo kirahisi zaidi.

Aidha Dkt. Kisenge alisema taasisi hiyo inahudumia wagonjwa wengi kutoka nje ya nchi  hii ni kutokana na huduma  bora inazozitoa na hivyo kutimiza maono ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya Tanzania kuwa nchi ya utalii wa matibabu.

Nao wazabuni  wa huduma na bidhaa  wa Taasisi hiyo  walishukuru kwa kuitwa kwao kushiriki katika mkutano huo na kusema kuwa umewasaidia kubadilishana mawazo, kuzidi kujenga  na kuimarisha uhusiano kati yao na JKCI na kuonesha  jinsi ambavyo JKCI imejipanga kuboresha huduma za matibabu.

Sandip Datta kutoka Computech Ltd. ambao ni wasambazaji wa vifaa tiba alishukuru kwa ushirikiano wanaoupata kutoka kwa wafanyakazi wa JKCI na kusema kuwa katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete hawapati changamoto kubwa ukilinganisha na Taasisi nyingine ambazo wanafanya nao kazi ni rahisi kwao watoa huduma na wazabuni kupata huduma.

“Sisi wasambazaji wa vifaa tiba huwa tunakutana na changamoto kutoka kwa watengenezaji wa vifaa tiba ambao wako nje ya nchi kuna wakati wanatupatia  vifaa vichache hatupati vyote kutokana na oda tunayowapa na kutufanya tulete vifaa pungufu tofauti na oda tuliyopewa, lakini tunajitahidi vifaa hivyo vinapokuwa tayari tunavileta kwa wakati ili wagonjwa wasikose huduma”,alisema Sandip.

 “Kupanda kwa dola kuliwasababishia vifaa vingi kupanda bei na kutokufika kwa wakati na wazabuni wengine walikaa kimya kwani walishindwa kuleta bidhaa husika kama Taasisi muangalie  kwa baadaye kama hali hiyo itatokea mtafanyaje  ili kukabiliana na changamoto hii”, alisema Ibrahim Kuhoga kutoka kampuni ya usambazaji wa dawa za binadamu ya AstraZeneca Ltd .

Lengo la kikao hicho kilichohudhuriwa na wazabuni wa huduma na bidhaa wa taasisi hiyo kilikuwa ni kuimarisha uhusiano na kufahamu changamoto mbalimbali zinazowakabili washitiri hao ili zitatuliwe kwa wakati.



Comments

Popular posts from this blog

Wataalamu wa JKCI kufanya upasuaji wa moyo nchini Zambia

JKCI na AICC Hospitali kutoa huduma za uchunguzi na matibabu ya moyo katika kikao kazi cha wenyeviti na watendaji wakuu wa Taasisi za Umma

JKCI yamshukuru Rais Dkt.Samia kwa kuwapa magari