20 kufanyiwa upasuaji wa moyo
Madaktari bingwa wa magonjwa ya moyo na mishipa ya damu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakishirikiana na wenzao kutoka shirika la Open Heart International (OHI) lililopo nchini Australia kumfanyia upasuaji wa kufungua mlango wa moyo wa chini kushoto ulikuwa umeziba na kutopitisha damu vizuri mgonjwa mwenye matatizo ya valvu wakati wa kambi maalumu ya siku 4 iliyoanza leo katika Taasisi hiyo. Jumla ya watu wazima 10 watafanyiwa upasuaji katika kambi hiyo inayotoa huduma za matibabu pamoja na mafunzo kwa wataalamu wa afya wa JKCI.
Madaktari bingwa wa magonjwa ya moyo kwa watoto wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakishirikiana na wenzao kutoka Shirila la Open Heart International (OHI) lililopo nchini Australia kuziba tundu na kufungua mishipa ya damu iliyoziba (tof repair) wakati wa kambi maalumu ya siku 4 iliyoanza leo katika Taasisi hiyo. Jumla ya watoto 10 watafanyiwa upasuaji katika kambi hiyo inayotoa huduma za matibabu pamoja na mafunzo kwa wataalamu wa afya wa JKCI.
Na:JKCI
***********************************************************************************************************
Comments
Post a Comment