Taarifa kwa wataalamu wa afya nchini
Wataalamu wa
upasuaji wa moyo na mishipa ya damu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI)
wakimfanyia mgonjwa upasuaji wa kubadilisha Valvu iliyokuwa haipitishi damu
vizuri.
********************************************************************************************************************************************************************************************************************
TAARIFA KWA WATAALAMU WA AFYA NCHINI
KAMBI MAALUMU YA
UPASUAJI WA MISHIPA YA DAMU (AORTIC ANEURYSM STENTING)
Matibabu haya yatatolewa na wataalamu wa magonjwa ya moyo na mishipa ya damu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na wenzao kutoka Hospitali ya BLK ya nchini India katika kambi maalumu ya matibabu itakayofanyika tarehe 13 hadi 17 Novemba 2023 jijini Dar es Salaam. Wataalamu hawa watawafanyia wagonjwa watu wazima upasuaji wa mishipa ya damu kwa njia ya tundu dogo kwa kutumia mtambo wa Cathlab (Aneurysm Stenting).
Kwa taarifa zaidi wasiliana kwa simu namba 0685 110187 Dkt. Tryphone Kagaruki, 0716 696217 Dkt. Alex Joseph na 0788 308999 Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI).
“Afya ya Moyo Wako ni Jukumu Letu”.
Comments
Post a Comment