Wahandisi wafanyiwa uchunguzi wa viashiria vya magonjwa ya moyo
Wahandisi walioshiriki mkutano wa 30 wa wahandisi washauri Afrika (FIDIC Afrika) wakiwa katika foleni ya kupata huduma za uchunguzi wa magonjwa ya moyo kwenye banda la Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) katika Ukumbi wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere International Convention Center (JNICC) uliopo jijini Dar es Salaam.
Mtaalamu wa huduma za afya mtandao kutoka kampuni ya
Cloudscript inayofanya kazi na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Beatrice
Mmari akiwafundisha wahandisi namna ya kutumia huduma ya afya mtandao kupitia
mfumo wa Cloudscript walipotembelea banda la JKCI wakati wa mkutano wa 30 wa
wahandisi washauri Afrika (FIDIC Africa) uliofanyika katika ukumbi wa kimataifa
wa Mwalimu Julius Nyerere International Convention Center (JNICC) uliopo jijini
Dar es Salaam.
Daktari kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Samweli
George akimpatia ushauri muhandisi aliyepatiwa huduma za uchunguzi wa magonjwa
ya moyo katika banda la Taasisi hiyo wakati wa mkutano wa 30 wa wahandisi washauri
Afrika (FIDIC Africa) uliofanyika katika ukumbi wa kimataifa wa Mwalimu Julius
Nyerere International Convention Center (JNICC) uliopo jijini Dar es Salaam.
Picha na: JKCI
*******************************************************************************************************************
Wahandisi kutoka nchi mbalimbali za Afrika wameishukuru
Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kuijali jamii na kuwapelekea huduma
za uchunguzi wa magonjwa ya moyo.
Pongezi hizo zimetolewa hivi karibuni na wahandisi waliotembelea banda
la JKCI lililokuwa katika maonesho yaliyofanyika wakati wa mkutano wa 30 wa
wahandisi washauri Afrika (FIDIC Africa) jijini Dar es Salaam.
Akizungumza baada ya kupata huduma za uchunguzi wa magonjwa
ya moyo Mhandisi Raphael Joseph alisema JKCI imewathamini wahandisi kwa
kuwafikishia huduma za uchunguzi wa magonjwa ya moyo huduma ambayo wameipata
kirahisi.
“Huduma mnayoitoa hapa leo mmetuokoa sisi wahandisi lakini
sio sisi tu bali mmeokoa kundi kubwa la watu wanaotuzunguka kwani tunapopata
changamoto za kiafya familia zetu zinakuwa kwenye changamoto pia”, alisema
Raphael
Raphael alisema nimuhimu vikao mbalimbali vya kisekta na vya
serikali wataalamu wa afya wakahusishwa upande wa kutoa huduma za uchunguzi wa
magonjwa yasiyoambukiza kuwasaidia kujitambua.
Kwa upande wake mhandisi Benard Malongo alisema mkutano wa 30
wa wahandisi washauri Afrika umewatendea haki washiriki kwa kuwafikishia huduma
za uchunguzi wa afya.
Benard alisema watu wanapopewa nafasi ya kuchunguza afya zao
watumie nafasi hizo vizuri kwani huduma za matibabu ni za gharama na wananchi
wengi mara nyingi hushindwa kumudu gharama hizo.
Akielezea mwitikio wa kupima afya kwa wahandisi hao Daktari
wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Samweli George alisema jumla ya
wahandisi 96 wamefanyiwa uchunguzi wa magonjwa ya moyo na kupewa ushauri kuhusu
lishe na afya bora.
Dkt. Samweli alisema watu 14 walikutwa na tatizo la shinikizo
la juu la damu na wawili walikuwa na tatizo la sukari iliyo juu sana matatizo yaliyohitaji
kufanya uchunguzi zaidi hivyo kupewa rufaa kufika JKCI ili waweze kufanyiwa
vipimo vikubwa zaidi.
“Mbali na shinikizo la juu la damu wapo tuliowakuta na tatizo
la sukari kuwa juu sana ambapo mtu mmoja tumemkuta kiwango cha sukari yake
kwenye damu kuwa 33 ambayo inaweza kumsababishia kupoteza maisha”, alisema Dkt.
Samweli
Wahandisi waliotembelea banda la JKCI wametoka nchi
mbalimbali za Afrika zikiwemo Tanzania, Zambia, Nigeria na Uganda.
Comments
Post a Comment