JKCI yashiriki kampeni ya afya check kutoa huduma za matibabu ya moyo
Katibu Tawala Mkoa wa Dar es Salaam Dkt. Toba
Nguvila akizungumza hivi karibuni na wananchi waliojitokeza kwenye uzinduzi wa
zoezi la upimaji wa afya bila malipo kwa wakazi wa mkoa wa Dar es Salaam linalofanyika
katika viwanja vya Barafu Mburahati. Zoezi hilo la upimaji wa siku 10
litafanyika katika halmashauri zote tano za mkoa wa Dar es Salaam.
Katibu Tawala Mkoa wa Dar es Salaam Dkt. Toba Nguvila
akikata Utepe hivi karibuni kuashiria uzinduzi wa zoezi la upimaji wa afya bila
malipo kwa wakazi wa mkoa wa Dar es Salaam linalofanyika katika viwanja vya
Barafu Mburahati. Zoezi hilo la upimaji wa siku 10 litafanyika katika halmashauri
zote tano za mkoa wa Dar es Salaam.
Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI)
Hospitali ya Dar Group Feliciana Mselle akimpima shinikizo la damu Katibu
Tawala Mkoa wa Dar es Salaam Dkt. Toba Nguvila alipotembelea banda la taasisi
hiyo wakati wa uzinduzi wa kampeni ya upimaji wa afya bila malipo kwa wakazi wa
mkoa wa Dar es Salaam.
Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo wa Taasisi ya
Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group Mlangwa Yango akizungumza na
mwananchi aliyejitokeza hivi karibuni wakati wa zoezi la uzinduzi wa upimaji wa
afya bila malipo kwa wakazi wa mkoa wa Dar es Salaam linalofanyika katika viwanja
vya Barafu Mburahati. Zoezi hilo la upimaji wa siku 10 litafanyika katika
halmashauri zote tano za mkoa wa Dar es Salaam.
Picha na Khamis Mussa
***************************************************************************************************
Comments
Post a Comment