KKKT Kitunda wafikiwa na huduma ya upimaji magonjwa yasiyoambukiza
Wakazi wa Kitunda wakisubiri kupatiwa huduma za uchunguzi na
matibabu ya magonjwa yasiyoambukiza wakati wa kambi maalumu ya siku tatu ya tiba
mkoba ijulikanayo kwa jina la Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Outreach Services
inayofanyika katika viwanja vya kanisa la KKKT Dayosisi ya Mashariki na Pwani
jimbo la kati Usharika wa Kitunda Relini.
Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya
Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group Samueli Rweyemamu akimpima kipimo cha
kuangali jinsi moyo unavyofanya kazi mkazi wa Kitunda wakati wa kambi maalumu
ya siku tatu ya tiba mkoba ijulikanayo kwa jina la Mhe. Dkt. Samia Suluhu
Hassan Outreach Services inayofanyika katika viwanja vya kanisa la KKKT
Dayosisi ya Mashariki na Pwani jimbo la kati Usharika wa Kitunda Relini.
Afisa Uuguzi wa JKCI Hospitali ya Dar Group Tufike Mwakibinga
akimchoma chanjo ya homa ya ini Mchungaji wa kanisa la KKKT Dayosisi ya
Mashariki na Pwani jimbo la kati usharika wa Kitunda Relini Edson Mgeni wakati
wa kambi maalumu ya siku tatu ya tiba mkoba ijulikanayo kwa jina la Mhe. Dkt.
Samia Suluhu Hassan Outreach Services inayofanyika katika viwanja vya kanisa la
KKKT Dayosisi ya Mashariki na Pwani jimbo la kati Usharika wa Kitunda Relini.
Afisa Uuguzi kutoka Taasisi ya Saratani ya Ocean Road (ORCI)
Saidina Msuya akimpatia ushauri mara baada ya kupima saratani ya matiti mkazi
wa Kitunda aliyefika kambi maalumu ya siku tatu ya tiba mkoba ijulikanayo kwa
jina la Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Outreach Services inayofanyika katika
viwanja vya kanisa la KKKT Dayosisi ya Mashariki na Pwani jimbo la kati
Usharika wa Kitunda Relini.
Picha na: Khamis Mussa
********************************************************************************************************
Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group
kufanya upimaji wa magonjwa ya moyo na magonjwa mengine yasiyoambukiza kwa wakazi
na waumini wa KKKT Kitunda.
Upimaji huo ulioanza jana unafanyika kwa siku tatu katika kambi
maalumu ya tiba mkoba ijulikanayo kwa jina la Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan
Outreach Services katika viwanja vya kanisa la KKKT Dayosisi ya Mashariki na
Pwani jimbo la kati Usharika wa Kitunda Relini.
Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam
Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali
ya Dar Group Samueli Rweyemamu alisema upimaji huo umefanyika katika eneo la
kanisa kuwapa nafasi watu kuonana na mchungaji kwani wapo watu wenye changamoto
za familia na maisha zinazowapelekea kupata magonjwa yasiyoambukiza.
“Katika kambi hii tumekuja na daktari bingwa wa saikolojioa
kuangalia afya ya akili kwani tatizo la afya ya akili limekuwa kubwa katika
jamii, watu wenye tatizo hilo wakirudi kwa mchungaji wakapata huduma za kiroho
watakaa vizuri na kuepuka magonjwa ya shinikizo la damu”, alisema Dkt.
Rweyemamu
Dkt. Rweyemamu alisema lengo kuu la kambi hiyo ni pamoja na
kufikisha huduma katika jamii, kutoa ushauri wa namna ya kujikinga na magonjwa
yasiyoambukiza na kutoa huduma za matibabu endelevu kwa watu watakaogundulika
kuwa na magonjwa yasiyoambukiza.
“Katika kambi hii tutatoa huduma za kuchunguza na kutoa
chanjo ya homa ya ini, kuchunguza na kutoa matibabu ya kansa na tezi dumu,
kuchunguza na kutoa matibabu ya magonjwa ya sukari, shinikizo la damu na moyo,
kuchunguza na kutoa matibabu ya matatizo ya masikio pamoja na kutoa huduma kwa
watu wanaohitaji ushauri wa kimwili na kiroho”, alisema Dkt. Rweyemamu
Kwa upande wake daktari bingwa wa magonjwa ya moyo kwa watoto
wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group Eva Wakuganda
aliwataka wakazi wa kitunda na maeneo ya jirani kutumia siku tatu za kambi hiyo
kuwafikisha watoto kufanyiwa uchunguzi wa magonjwa ya moyo.
Dkt. Eva alisema wazazi wakiwa na utaratibu wa kuwafanyia
uchunguzi wa afya watoto wao watawasaidia kugundua matatizo ya kiafya mapema na
kumpa nafasi mtoto kupata matibabu mapema kwani magonjwa mengi ya moyo kwa
watoto yanakuwa na muda wa matibabu na pale muda unapovuka inakuwa ngumu
kumtibu mtoto.
“Kuna wakati tunakutana na changamoto za matibabu kwa watoto
wenye magonjwa ya moyo kwani unakuta mtoto alihitaji kufanyiwa upasuaji wa moyo
kabla hajafikisha mwaka mmoja lakini kwasababu mzazi hakugundua mapema anamleta
mtoto akiwa na zaidi ya mwaka mmoja hivyo kukwamisha baadhi ya matibabu”,
alisema Dkt. Eva
Naye Mkuu wa jimbo la kati kanisa la KKKT Dayosisi ya
Mashariki na Pwani Mchungani Frank Kimambo aliwataka waumini wa KKKT kuona
umuhimu wa kufanya uchungzi wa afya ili washiriki kikamilifu katika kumtumikia
Mungu pamoja na kushiriki katika shughuli za kiuchumi na maendeleo kwa kuwa
shughuli hizo zinahitaji watu wenye afya.
Mchungaji Kimambo alisema kati ya ibada zote zilizofanyika
mwaka huu katika Kanisa la KKKT Usharika wa Kitunda Relini hii imekuwa ibada
kubwa kwani waumini na wakazi wa kitunda wameweza kufikiwa na huduma za afya
bila gharama hivyo kuushukuru uongozi wa kanisa hilo.
“Nawashukuru madaktari bingwa wa JKCI, Ocean Road, Muhimbili na
Hospitali ya Magereza kwa kuacha ofisi zenu na kuja kutuhudumia, Mungu amewapa
uwezo kwaajili ya kushughulika na miili hii iliyoumbwa naye, nisadaka kubwa
sana mmeitoa kwaajili yetu”, alisema Mchungaji Kimambo
Upimaji huo unafanywa na madaktari bingwa kutoka Taasisi ya
Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Taasisi ya
Saratani Ocean Road (ORCI) na Hospitali ya magereza ya Ukonga.
Comments
Post a Comment