JKCI yasaini makubaliano na China ujenzi wa hospitali mpya ya moyo
Mkurugenzi
Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge na
Kiongozi wa kamati ya ukaguzi wa mradi wa ujenzi kutoka Jamhuri ya Watu wa
China Yang Ling wakionesha hati ya makubaliano ya ujenzi wa hospitali mpya moyo
mara baada ya kusaini hati hiyo jana katika ukumbi wa mikutano wa Taasisi hiyo
iliyopo jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi
Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge na
Kiongozi wa kamati ya ukaguzi wa mradi wa ujenzi kutoka Jamhuri ya Watu wa
China Yang Ling wakisaini hati ya makubaliano ya ujenzi wa hospitali mpya moyo jana
katika ukumbi wa mikutano wa Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi
Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akizungumza
na wafanyakazi wa JKCI pamoja na wataalamu wa mradi wa ujenzi kutoka Jamhuri ya
Watu wa China wakati wa hafla fupi ya kusaini hati ya makubaliano ya ujenzi wa
hospitali mpya moyo jana katika ukumbi wa mikutano wa Taasisi hiyo iliyopo
jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi
wa Kitengo cha Afrika ya Kusini na Mashariki, Wakala wa Ushirikiano wa
Kimataifa wa Kiuchumi (AIEC) chini ya Wizara ya Biashara ya China Li Qing
akizungumza wakati wa hafla fupi ya kusaini hati ya makubaliano ya ujenzi wa
hospitali mpya ya moyo iliyofanyika jana katika ukumbi wa mikutano wa Taasisi ya
Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) iliyopo jijini Dar es Salaam.
Wafanyakazi
wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na wataalamu wa mradi wa ujenzi kutoka
Jamhuri ya Watu wa China wakisikiliza wakati wa hafla fupi ya kusaini hati ya
makubaliano ya ujenzi wa hospitali ya moyo iliyofanyika jana katika ukumbi wa mikutano wa Taasisi hiyo
iliyopo jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi
Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akipokea
zawadi kutoka kwa Kiongozi wa kamati ya ukaguzi wa mradi kutoka Jamhuri ya Watu
wa China Yang Ling mara baada ya hafla fupi ya kusaini hati ya makubaliano ya
ujenzi wa hospitali mpya moyo iliyofanyika jana katika ukumbi wa mikutano wa
Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi
Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge
akimkabidhi zawadi Mkurugenzi wa Kitengo cha Afrika ya Kusini na Mashariki, Wakala
wa Ushirikiano wa Kimataifa wa Kiuchumi (AIEC) chini ya Wizara ya Biashara ya
China Li Qing wakati wa hafla fupi ya kusaini hati ya makubaliano ya ujenzi wa
hospitali mpya ya moyo iliyofanyika jana katika ukumbi wa mikutano wa Taasisi
hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi
Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akiwa
katika picha ya pamoja na Mkurugenzi wa Kitengo cha Afrika ya Kusini na Mashariki,
Wakala wa Ushirikiano wa Kimataifa wa Kiuchumi (AIEC) na wataalamu wa mradi wa
ujenzi kutoka Jamhuri ya Watu wa China wakati
wa hafla fupi ya kusaini hati ya
makubaliano ya ujenzi wa hospitali mpya moyo iliyofanyika jana katika ukumbi wa
mikutano wa Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam.
Na JKCI
***************************************************************************************************
Taasisi
ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na Wataalamu kutoka China wasaini hati ya
makubaliano ujenzi wa hospitali mpya ya moyo itakayoleta mabadiliko makubwa
katika utoaji wa huduma za kibingwa na ubingwa bobezi kwa wagonjwa wa moyo
nchini.
Hati
hiyo imesainiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI)
Dkt. Peter Kisenge pamoja na Kiongozi wa Kamati ya Ukaguzi wa Mradi kutoka Jamhuri
ya Watu wa China Yang Ling na kuahidi kuanza mchakato wa ujenzi huo mara baada
ya taratibu kukamilika.
Akizungumza
wakati wa hafla ya utiaji wa saini Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo
Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge alisema hospitali hiyo itasaidia
kuongeza upatikanaji wa huduma za uchunguzi na matibabu ya kibingwa, pamoja na
kuimarisha mazingira ya kazi kwa wataalamu wa afya wanaofanya kazi katika Taasisi
hiyo.
“Mradi
huu ni hatua muhimu sana katika kuimarisha uwezo wetu wa kutoa huduma za
matibabu ya moyo kwa viwango vya juu zaidi na kuhakikisha wananchi wengi zaidi wanapata
huduma bora kwa wakati”, alisema Dkt. Kisenge
Dkt.
Kisenge alisema mradi huo ni sehemu ya juhudi ya Serikali ya awamu ya sita ya
Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kuimarisha sekta ya afya na kupunguza vifo
vinavyotokana na magonjwa yasiyoambukiza yakiwemo magonjwa ya moyo.
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)



Comments
Post a Comment