JKCI na BMH waimarisha utalii tiba, wafanya upasuaji wa moyo kwa watoto kutoka nchini Burundi
Wataalamu wa upasuaji
wa moyo kwa watoto wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na
wenzao wa Hospitali ya Benjamin Mkapa (BMH) wakimfanyia upasuaji wa moyo mtoto
mwenye tundu kwenye moyo kutoka nchini Burundi wakati wa kambi maalumu ya
upasuaji wa moyo kwa watoto iliyokuwa ikifanyika katika Hospitali hiyo iliyopo
jijini Dodoma.
Wataalamu wa kuhudumia
wagonjwa wa dharura na wanaohitaji uangalizi maalumu (ICU) wa Taasisi ya Moyo
Jakaya Kikwete (JKCI) wakimuhudumia mtoto kutoka nchini Burundi aliyefanyiwa
upasuaji wa moyo katika kambi maalumu iliyofanywa na wataalamu wa JKCI kwa
kushirikiana na wenzao wa Hospitali ya Benjamini Mkapa (BMH) iliyopo jijini
Dodoma.
Wataalamu wa upasuaji
wa moyo kwa watoto wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na
wenzao wa Hospitali ya Benjamin Mkapa (BMH) wakimfanyia upasuaji wa moyo mtoto
mwenye tundu kwenye moyo kutoka nchini Burundi wakati wa kambi maalumu ya
upasuaji wa moyo kwa watoto iliyokuwa ikifanyika katika Hospitali hiyo iliyopo
jijini Dodoma.
Afisa uuguzi wa Taasisi
ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Mohamed Wamara akitoa taarifa ya maendeleo ya
mtoto aliyefanyiwa upasuaji wa kuziba tundu kwenye moyo wakati wa kambi maalumu
ya upasuaji wa moyo kwa watoto kutoka nchini Burundi iliyofanywa na wataalamu
wa JKCI kwa kushrikiniana na wenzao wa Hospitali ya Benjamini Mkapa (BMH)
iliyopo jijini Dodoma.
Daktari bingwa wa
magonjwa ya moyo kwa watoto wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Stella
Mongela akimfanyia kipimo cha kuangalia jinsi moyo unavyofanya kazi (ECHO)
mtoto aliyefanyiwa upasuaji wa moyo kutoka nchini Burundi wakati wa kambi
maalumu ya upasuaji wa moyo kwa watoto iliyofanywa na wataalamu wa JKCI kwa
kushirikiana na wenzao wa Hospitali ya Hospitali ya Benjamini Mkapa (BMH)
iliyopo jijini Dodoma.
Mtaalamu wa kuendesha
mashine ya kuusaidia moyo na mapafu kufanya kazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya
Kikwete (JKCI) Sophia Lukonge akiendesha mashine hiyo wakati wa kambi maalumu
ya upasuaji wa moyo kwa watoto kutoka nchini Burundi iliyofanywa na wataalamu
wa JKCI kwa kushirikiana na wenzao wa Hospitali ya Benjamini Mkapa (BMH)
iliyopo jijini Dodoma.
Afisa Uuguzi anayefanya
kazi katika chumba cha upasuaji wa moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete
(JKCI) Mahawa Asenga akiandaa vifaa vya upasuaji wa moyo kwa watoto kutoka
nchini Burundi wakati wa kambi maalumu ya upasuaji wa moyo kwa watoto iliyofanywa
na wataalamu wa JKCI kwa kushirikiana na wenzao wa Hospitali ya Benjamini Mkapa
(BMH) iliyopo jijini Dodoma.
Na JKCI
***************************************************************************************************
Watoto kutoka nchini
Burundi waliokuwa na matatizo ya moyo ya kuzaliwa nayo wamefanyiwa upasuaji
mkubwa wa moyo na watalamu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana
na wenzao wa Hospitali ya Benjamini Mkapa (BMH) hatua inayoendelea kuifanya
Tanzania kuwa kitovu cha utalii tiba Barani Afrika.
Upasuaji huo umefanyika
katika kambi maalumu yenye malengo ya kuweka ushirikiano baina ya wataalamu hao,
kubadilishana ujuzi pamoja na kuonesha umahiri wa wataalamu wa Tanzania katika
kutoa huduma bingwa bobezi za upasuaji wa moyo kwa watoto.
Akizungumza wakati wa
kuhitimisha kambi hiyo Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Benjamin Mkapa (BMH)
Prof. Abel Makubi alisema mafanikio ya kambi hiyo yameonesha uwezo wa wataalamu
wa Kitanzania kutoa huduma za kibingwa kwa kushirikiana huku ikidhihirisha
matokeo ya uwekezaji mkubwa unaofanywa na Serikali katika sekta ya afya.
Prof. Makubi alisema
kambi hiyo ni mwanzo wa ushirikiano kati ya BMH na JKCI ukiwa na dhumuni la kuongeza
upatikanaji wa huduma za magonjwa ya moyo kwa watanzania na watu kutoka katika
mataifa mengine.
Aidha Prof. Makubi
alisema kambi hiyo imeandika historia katika Hospitali ya Benjamin Mkapa (BMH)
kwa kuwa mara ya kwanza kufanya upasuaji wa moyo kwa watoto kutoka nje ya
Tanzania jambo linaloonesha mafanikio ya utekelezaji wa mkakati wa tiba utalii
nchini.
Kwa upande wake Daktari
Bingwa wa Upasuaji wa Moyo kwa Watoto kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete
(JKCI) Godwin Sharau alisema ushirikiano huo umeiwezesha timu za wataalamu wa
upasuaji wa moyo kubadilishana uzoefu na kuongeza uwezo wa kutoa huduma za
kibingwa.
“Tumefurahia sana kupata
mwaliko kutoka Hospitali ya Benjamin Mkapa (BMH) kuungana nao kutoa huduma ya
upasuaji wa moyo kwa watoto waliotoka nchini Burundi, tunaziomba na Hospitali
nyingine nchini zishirikiane nasi lengo likiwa ni kuongeza ujuzi na kuokoa maisha
ya watoto wanaohitaji huduma za upasuaji wa moyo”, alisema Dkt. Godwin.
Naye Mratibu wa Utalii Tiba
kutoka Wizara ya Afya Dkt. Asha Mahita alisema mafanikio ya kambi hiyo yanaunga
mkono Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 iliyolenga kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha tiba utalii Barani Afrika.
“Serikali kupitia Dira
ya Taifa ya Maendeleo 2050 inataka Tanzania kuwa kitovu cha tiba utalii Barani
Afrika, leo tumejionea ushirikiano wa hospitali zetu hizi mbili zilivyoanza
kutekeleza maono hayo kwa vitendo”, alisema Dkt. Asha
Akitoa neno la shukrani
daktari kutoka nchini Burundi Nzitunga Octavie alisema familia za watoto
waliopatiwa matibabu katika kambi hiyo wameshukuru kwa ukarimu wa watanzania
kuanzia mapokezi yao hadi huduma walizopatiwa.
“Tulipofika hapa
tulijisikia kama tuko nyumbani tunashukuru sana madaktari wote waliofanya
upasuaji wa moyo kwa watoto wetu kwani tunaamini baada ya matibabu waliyoyapata
watapona”, alisema Dkt. Octavie
Dkt. Octavie alisema kupitia
kambi hiyo ameweza kujifunza mambo mengi ya kitaalamu yanayohusu magonjwa ya
moyo kwa watoto kwa kufanya kazi na wataalamu wa Tanzania katika kutoa huduma
kwa watoto waliotoka nchini Burundi.

.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)



Comments
Post a Comment