JKCI yapongezwa kwa kuanza kutekeleza Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050
Waziri wa Nchi, Ofisi
ya Rais, Mipango na Uwekezaji Mhe. Prof. Kitila Mkumbo akiweka jiwe la msingi
la Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) tawi la Temeke kwa niaba ya Waziri
Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Mwigulu Nchemba jana wakati wa
hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi iliyofanyika katika Taasisi hiyo tawi la Dar
Group lililopo Tazara jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Nchi, Ofisi
ya Rais, Mipango na Uwekezaji Mhe. Prof. Kitila Mkumbo, Naibu Waziri wa Afya
Dkt. Florence Samizi na viongozi mbalimbali wakiwa katika picha ya pamoja mara baada
ya hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi la Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI)
tawi la Temeke iliyofanyika jana katika Hospitali ya JKCI Dar Group iliyopo
Tazara jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Nchi, Ofisi
ya Rais, Mipango na Uwekezaji Mhe. Prof. Kitila Mkumbo akipokea zawadi kutoka
kwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI)
Dkt. Hassan Mahmoud Mshinda wakati wa hafla ya uwekaji jiwe la msingi la
Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) tawi la Temeke iliyofanyika jana katika
Hospitali ya JKCI Dar Group iliyopo Tazara jijini Dar es Salaam.
Daktari bingwa wa
magonjwa ya moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar
Group Eva Wakuganda akimueleza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mipango na
Uwekezaji Mhe. Prof. Kitila Mkumbo namna JKCI ilivyojiandaa kuwahudumia
mchezaji aliyepata majeruhi kwa kutumia teknolojia ya kisasa wakati wa hafla ya
uwekaji jiwe la msingi la Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) tawi la Temeke
iliyofanyika jana katika Hospitali ya JKCI Dar Group iliyopo Tazara jijini Dar
es Salaam.
Waziri wa Nchi, Ofisi
ya Rais, Mipango na Uwekezaji Mhe. Prof. Kitila Mkumbo, Naibu Waziri wa Afya
Dkt. Florence Samizi na viongozi mbalimbali wakiwa katika picha ya pamoja mara
baada ya hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi la Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete
(JKCI) tawi la Temeke iliyofanyika jana katika Hospitali ya JKCI Dar Group
iliyopo Tazara jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Nchi, Ofisi
ya Rais, Mipango na Uwekezaji Mhe. Prof. Kitila Mkumbo, Naibu Waziri wa Afya
Dkt. Florence Samizi, viongozi mbalimbali na wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo
Jakaya Kikwete (JKCI) wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya hafla ya uwekaji
wa jiwe la msingi la Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) tawi la Temeke
iliyofanyika jana katika Hospitali ya JKCI Dar Group iliyopo Tazara jijini Dar
es Salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa
Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akimueleza Waziri wa
Nchi, Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji Mhe. Prof. Kitila Mkumbo mipango ya
Taasisi hiyo alipomwakilisha Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Mhe. Mwigulu Nchemba katika hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi iliyofanyika jana
katika Taasisi hiyo tawi la Dar Group lililopo Tazara jijini Dar es Salaam.
Na JKCI
***************************************************************************************************************
Taasisi
ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) imepongezwa kwa kuanza kutekeleza Dira ya Taifa
ya Maendeleo 2050 kwa kuweka jiwe la msingi la Taasisi hiyo tawi la Temeke.
Pongezi
hizo zimetolewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais - Mipango na Uwekezaji Mhe.
Prof. Kitila Mkumbo alipokuwa akimuwakilisha Waziri Mkuu wa Jamuhuri ya
Muungano wa Tanzania Mhe. Mwigulu Nchemba katika hafla ya uwekaji wa jiwe la
msingi iliyofanyika jana katika Tawi la JKCI Hospitali ya Dar Group iliyopo
Tazara jijini Dar es Salaam.
Prof.
Mkumbo alisema hatua ya uwekaji wa jiwe hilo la msingi inaenda sambamba na
maandalizi ya ujenzi wa jengo litakalokuwa likitoa huduma za tiba ya michezo
kwaajili ya maandalizi ya michuano ya AFCON 2027 ambapo Tanzania ni mwenyeji wa
michuano hiyo.
“Uwekezaji
huu muhimu unaenda kukuza na kuhamasisha utalii tiba nchini kwani utawasaidia watalii
wanaokuja Tanzania kupata huduma bora za afya katika taasisi zetu za afya
ikiwemo JKCI”, alisema Prof. Mkumbo.
Prof.
Mkumbo alisema katika kipindi cha miaka 10 iliyopita JKCI imeokoa zaidi ya
shilingi bilioni 37 ambazo zilikuwa zikitumika kuwapeleka wagonjwa wa moyo nje
ya nchi kwaajili ya matibabu.
“Taasisi
hii imekuwa ikishiriki katika utekelezaji wa malengo ya Serikali kwa kuokoa
fedha nyingi ambazo kwa sasa zinaelekezwa kwenye shughuli nyingine za
maendeleo”, alisema Prof. Mkumbo.
Akizungumza
kwa Niaba ya Waziri wa Afya Mhe. Mohamed Mchengerwa Naibu Waziri wa Afya Dkt.
Florence Samizi alisema uwekezaji wa jengo la tiba ya michezo utasaidia kutoa
huduma muhimu za uchunguzi na matibabu kwa wanamichezo ikiwa ni hatua za
kimkakati kuelekea AFCON 2027.
“Tunafungua
ukurasa mpya wa huduma za moyo nchini kwa kuweka kituo muhimu kitakachotoa huduma
za kinga, uchunguzi na ushauri wakitalaamu kwa wananchi na wanamichezo ili
waweze kushiriki na kufurahia mashindano ya AFCON 2027 kwa usalama unaozingatia
viwango vya kimataifa”,
“Tunamshukuru
Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea
kuimarisha miundombinu ya afya ikiwemo vifaa tiba, mafunzo kwa watalaamu wa
afya yote ili huduma bingwa ziwafikie wananchi kwa karibu”, alisema Dkt.
Florence
Dkt.
Florence alisema JKCI ina dhamira ya dhati ya kusogeza huduma karibu na
wananchi kwani kuanzishwa kwa tawi la Arusha Lutheran Medical Center (ALMC)
kumepanua wigo wa huduma za dharula za moyo kwa wananchi na watalii wanaotembelea
nchini.
Kwa
upande wake Mkurugenzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter
Kisenge alisema uwekezaji huo wenye thamani ya shilingi bilioni 18 utaifanya
JKCI kuendelea kuwa kinara katika utoaji wa huduma za Kibingwa na ubingwa
bobezi katika tiba ya moyo pamoja na huduma nyingine maalumu kwa viwango vya
kimataifa.
“Jengo
hili litakuwa la pili kwa ukubwa barani Afrika katika kutoa huduma za uchunguzi
na matibabu ya magonjwa ya moyo pamoja na huduma za tiba ya michezo (Sport
Medicine) hivyo kuchochea wanamichezo kutoka mataifa mbalimbali kuja kupata huduma
JKCI”, alisema Dkt. Kisenge.
Katika
hatua nyingine Dkt. Kisenge alisema kutokana na kuongezeka kwa magonjwa yasiyoambukiza
JKCI imeanzisha kampeni ya Jua Namba Zako yenye lengo la kuhamasisha wananchi
kutambua hali zao za afya na kuokoa Maisha.
Aidha
Dkt. Kisenge alisema JKCI imeendelea kuwafikia wananchi kupitia huduma za tiba
mkoba ambapo hadi sasa mikoa 23 imefikiwa na kusaidia kuokoa maisha ya wagonjwa
wenye matatizo ya moyo na mishipa ya damu, pia kufikisha huduma hizo katika nchi
jirani ikiwemo Jamuhuri ya kidemokrasia ya Congo (DRC), Malawi, Zambia na
Visiwa vya Comoro.

.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)



Comments
Post a Comment