Upimaji na matibabu ya magonjwa ya moyo Kisiwani Pemba


Mtaalamu wa kupima vipimo vya moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Paschal Kondi akimpima kipimo cha kuangalia jinsi moyo unavyofanya kazi mkazi wa Manyara wakati wa kambi maalum ya upimaji wa moyo iliyofanyika mwezi wa tano mwaka huu mkoani humo.  

 *************************************************************************************************************************************************************************************************

Wataalamu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na wenzao wa Hospitali ya Rufaa ya Abdulla Mzee iliyopo wilaya ya Mkoani Mkoa wa Kusini Pemba watafanya upimaji na matibabu ya magonjwa ya moyo kwa wananchi wa Kisiwa cha Pemba.

Upimaji huo utafanyika kwa watoto na watu wazima kuanzia tarehe 19/06/2023  hadi tarehe 23/06/2023  saa mbili kamili asubuhi mpaka saa 10 kamili jioni katika Hospitali ya Rufaa ya Abdulla Mzee.

Kutakuwa na wataalamu wa lishe ambao watatoa elimu ya lishe bora ambayo itawapa wananchi uelewa na  kufuata mtindo bora wa maisha ambao utawasaidia kuepukana na magonjwa ya moyo ambayo ni moja ya magonjwa yasiyoambukiza na yanaweza kuepukika kwa kufuata ushauri wa kitaalamu.

Watakaogundulika kuwa na matatizo ya moyo watafanyiwa uchunguzi zaidi na kupatiwa matibabu hapohapo au kupewa rufaa ya kuja kutibiwa katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI)  iliyopo Upanga jijini Dar es Salaam.

Tunawaomba wananchi mjitokeze kwa wingi kupima afya zenu kujua kama mna matatizo ya moyo ili kuanza matibabu mapema kwa atakayegundulika kuwa mgonjwa.


Kwa taarifa zaidi wasiliana kwa namba 0777905996 Dkt. Mohamed Faki Saleh na 0777509060 Dkt. Rashid Saleh Hemed.

 “Afya ya Moyo Wako ni Jukumu Letu”.

Comments

Popular posts from this blog

JKCI na AICC Hospitali kutoa huduma za uchunguzi na matibabu ya moyo katika kikao kazi cha wenyeviti na watendaji wakuu wa Taasisi za Umma

JKCI yapata tuzo ya taasisi ambayo imetoa mchango wa kipekee kiuchumi na kijamii katika kuleta matokeo makubwa kwa kipindi cha mwaka 2023/2024

Maabara ya JKCI yapata ithibati ya kimataifa (ISO 15189:2012)