Posts

Showing posts from July, 2023

Kwa mara ya kwanza matibabu ya uzibuaji wa mishipa ya damu ya miguu yafanyika nchini

Image
Wataalamu wa magonjwa ya moyo na mishipa ya damu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakimfanyia mgonjwa upasuaji wa kuzibua mishipa ya damu ya miguu (Peripheral Interventions) ambayo haipitishi damu vizuri wakati wa kambi maalumu ya siku tano ya matibabu hayo inayofanyika jijini Dar es Salaam. Wagonjwa 100 wenye matatizo ya mishipa ya damu ya miguu iliyoziba wanatarajia kupatiwa matibabu katika kambi hiyo ambayo ni ya kwanza kufanyika hapa nchini Wataalamu wa magonjwa ya moyo na mishipa ya damu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na mwenzao kutoka Hospitali ya BLK iliyopo nchini India Suhail Bukhari wakimfanyia mgonjwa upasuaji wa kuzibua mishipa ya damu ya miguu (Peripheral Interventions) ambayo haipitishi damu vizuri wakati wa kambi maalumu ya siku tano ya matibabu hayo inayofanyika jijini Dar es Salaam. Wagonjwa 100 wenye matatizo ya mishipa ya damu ya miguu iliyoziba wanatarajia kupatiwa matibabu katika kambi hiyo ambayo ni ya kwanza kufanyika hapa nchini. Na: JKCI *****

Wagonjwa 70 kuzibuliwa mishipa ya damu ya miguu iliyoziba

Image
Wataalamu wa magonjwa ya moyo na mishipa ya damu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na mwenzao Suhail Bukhari kutoka Hospitali ya BLK iliyopo nchini India wakimfanyia mgonjwa upasuaji wa kuzibua mishipa ya damu ya miguu (Peripheral Interventions) ambayo haipitishi damu vizuri wakati wa kambi maalumu ya siku tano ya matibabu hayo inayofanyika jijini Dar es Salaam. Jumla ya wagonjwa 70 wenye matatizo ya mishipa ya damu ya miguu iliyoziba wanatarajia kupatiwa matibabu katika kambi hiyo ambayo ni ya kwanza kufanyika hapa nchini Picha na: JKCI ***********************************************************************************************************

Wafanyakazi wa JKCI wapata mafunzo ya kutoa huduma bora kwa wagonjwa

Image
  Mwezeshaji kutoka kampuni ya VERTEX Charles Nduku akiwafundisha wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) jinsi ya kutoa huduma bora kwa wateja wanaowahudumia wakati wa mafunzo hayo yaliyotolewa kwa wafanyakazi wa kada mbalimbali leo katika ukumbi wa JKCI uliopo jijini Dar es Salaam Baadhi ya washiriki wa mafunzo ya jinsi ya kutoa huduma bora kwa wateja wakifuatilia mada zilizokuwa zikiendelea kwenye mafunzo hayo leo katika ukumbi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) iliyopo jijini Dar es Salaam. Mfanyakazi wa mapokezi  wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Safina Tibanyendera akichangia mada wakati wa mafunzo ya jinsi ya kutoa huduma bora kwa wateja yaliyofanyika kwa wafanyakazi wa kada mbalimbali wa taasisi hiyo  leo katika ukumbi wa JKCI uliopo jijini Dar es Salaam. Mwezeshaji kutoka kampuni ya VERTEX Charles Nduku akiwafundisha wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) jinsi ya kutoa huduma bora kwa wateja wanaowahudumia wakati wa mafunzo hayo yaliyot

Mkurugenzi Mtendaji JKCI Dkt. Peter Kisenge aelezea Utekelezaji wa majuk...

Image

Wagonjwa 2760 wafanyiwa upasuaji wa moyo JKCI kwa mwaka wa fedha 2022/23

Image
  Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akizungumza na waandishi wa habari wakati wa mkutano wa kuelezea utekelezaji wa shughuli mbalimbali za  Taasisi hiyo na kutoa mwelekeo wa utekelezaji kwa mwaka wa fedha 2023/2024. Mkutano huo umefanyika leo katika ukumbi wa Idara ya Habari - MAELEZO jijini Dar es Salaam. ************************************************************************************************************************************************************************************************ TAARIFA YA MKURUGENZI MTENDAJI WA TAASISI YA MOYO JAKAYA KIKWETE (JKCI) DKT. PETER KISENGE KATIKA MKUTANO WA WAANDISHI WA HABARI ULIOFANYIKA KWENYE UKUMBI WA IDARA YA HABARI - MAELEZO, DAR ES SALAAM TAREHE 18 JULAI 2023. Ndugu Watumishi wa Umma, Ndugu Waandishi wa Habari, Mabibi na Mabwana, NAWASALIMU KWA JINA LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA…… Awali ya yote napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu, mwingi wa rehema ambaye ametuwezesha kuifik

Wapigwa msasa wa kuwahudumia wagonjwa wa dharura na mahututi

Image
Baadhi ya wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Kurugenzi ya Upasuaji wakimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi hiyo Dkt. Peter Kisenge wakati akifungua mafunzo ya siku mbili ya kuwahudumia wagonjwa wa dharura na mahututi wanaotibiwa katika Taasisi hiyo. Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akizungumza na watumishi wa Kurugenzi   ya Upasuaji wanaoshiriki mafunzo ya siku mbili ya kuwahudumia wagonjwa wa dharura na mahututi wakati akifungua mafunzo hayo   leo katika ukumbi wa Taasisi hiyo jijini Dar es Salaam. Mkurugenzi wa Upasuaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Angela Muhozya akitoa neno na shukrani wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya siku mbili ya  kuwahudumia wagonjwa wa dharura na mahututi yanayotolewa kwa wafanyakazi wa Kurugenzi hiyo leo jijini Dar es Salaam. Daktari bingwa wa upasuaji wa moyo kwa watoto wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Godwin Sharau akichangia mada wakati wa mafunzo ya siku mbili ya

20 watibiwa mfumo wa umeme wa moyo

Image
Madaktari bingwa wa moyo na mfumo wa umeme wa moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na wenzao kutoka Shirika la Madaktari Afrika la nchini Marekani wakimfanyia upasuaji wa tundu dogo kwa kutumia mtambo wa Cath lab mgonjwa mwenye matatizo ya mfumo wa umeme wa moyo wakati wa kambi maalum ya siku tano ya matibabu hayo. Kambi hiyo imemalizika leo ambapo jumla ya wagonjwa 20 wamefanyiwa upasuaji mdogo wa moyo Na: JKCI ***************************************************************************************************************** Wagonjwa 20 wenye matatizo ya mfumo wa umeme wa moyo wamefanyiwa upasuaji wa tundu dogo kwa kutumia mtambo wa Cathlab katika kambi maalum iliyofanywa na wataalam wa afya wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na wenzao kutoka Shirika la Madaktari Afrika la nchini Marekani. Kambi hiyo ya siku tano iliyomalizika leo ililenga kuwahudumia wagonjwa wenye matatizo ya mfumo wa umeme wa moyo, kuwasaidia wataalam wa afya ambao wapo masomoni kuji

JKCI yatoa huduma za uchunguzi na matibabu ya moyo SABASABA

Image

JKCI mshindi wa kwanza Sabasaba katika kundi na watoa huduma za afya

Image
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Hussein Ali Mwinyi akimkabidhi ngao ya mshindi wa kwanza katika kundi la watoa huduma za afya, vifaa tiba na teknolojia ihusuyo afya Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge wakati wa kufungwa kwa  maonesho ya 47 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam Sabasaba leo jijini Dar es Salaam Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa Taasisi hiyo walioshiriki kutoa huduma za upimaji na matibabu ya moyo  katika banda la JKCI wakati wa maonesho ya 47 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam baada ya kufungwa kwa maonesho hayo leo jijini Dar es Salaam. Jumla ya watu 742 walipata huduma za matibabu matibabu katika banda hilo Na: JKCI ************************************************************************************************************************ Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete imeibuka mshindi wa kwanza kati

Kambi maalum ya mfumo wa umeme wa moyo yafanyika JKCI

Image
Madaktari bingwa wa moyo na mfumo wa umeme wa moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na wenzao kutoka Shirika la Madaktari Afrika la nchini Marekani wakimfanyia upasuaji wa tundu dogo kwa kutumia mtambo wa Cathlab mgonjwa mwenye matatizo ya mfumo wa umeme wa moyo wakati wa kambi maalum ya siku tano ya matibabu hayo. Wataalam wa afya wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na wenzao kutoka Shirika la Madaktari Afrika la nchini Marekani wakiangalia umeme wa moyo unaoingia kwa mgonjwa unavyofanya kazi kwa kutumia mashine ya CRTD Programmer wakati wa kambi maalum ya siku tano ya matibabu hayo. Jumla ya wagonjwa 12 wameshapatiwa matibabu katika kambi hiyo. Picha na: Khamis Mussa ************************************************************************************************************

JKCI yashiriki mazoezi ya kutembea maandalizi ya mbio za CRDB Marathon

Image
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Albert Chalamila, Mkurugenzi Mkuu wa benki ya CRDB Abdulmajid Nsekela na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge pamoja na wadau wa mbio za CRDB Marathoni wakifanya mazoezi ya viungo ikiwa ni maandalizi ya kuelekea mbio za CRDB Marathon zitakazofanyika mwezi Agosti mwaka huu kuchangia matibabu ya watoto wenye magonjwa ya moyo wanaotibiwa JKCI. Baadhi ya viongozi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakifanya mazoezi ya viungo ikiwa ni maandalizi ya kuelekea mbio za CRDB Marathon zitakazofanyika mwezi Agosti mwaka huu kuchangia matibabu ya watoto wenye magonjwa ya moyo wanaotibiwa JKCI. Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Albert Chalamila, Mkurugenzi Mkuu wa benki ya pamoja na wadau wa mbio za CRDB Marathoni wakifanya mazoezi ya kutembea ikiwa ni maandalizi ya kuelekea mbio za CRDB Marathon zitakazofanyika mwezi Agosti mwaka huu kuchangia matibabu ya watoto wenye magonjwa ya moyo wanaotibiwa JKCI. Baadhi ya wa