JKCI mshindi wa kwanza wa jumla katika maonesho ya Sabasaba
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Majaliwa
Kassim Majaliwa akimpongeza Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano wa
Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Anna Nkinda baada ya Taasisi hiyo kuibuka
mshindi wa kwanza wa jumla katika maonesho ya 47 ya Biashara ya Kimataifa ya
Dar es Salaam (SABASABA) wakati wa ufunguzi wa maonesho hayo.
*****************************************************************************************************************
Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete imeibuka mshindi wa kwanza wa
jumla katika Maonesho ya 47 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (SABASABA)
yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere vilivyopo
barabara ya kilwa jijini Dar es Salaam.
Tuzo hiyo imetolewa leo na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa wakati wa ufunguzi wa Maonesho hayo
yenye washiriki 3514 kutoka ndani na nje ya nchi.
Comments
Post a Comment