Kambi maalum ya mfumo wa umeme wa moyo yafanyika JKCI
Madaktari
bingwa wa moyo na mfumo wa umeme wa moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete
(JKCI) na wenzao kutoka Shirika la Madaktari Afrika la nchini Marekani wakimfanyia
upasuaji wa tundu dogo kwa kutumia mtambo wa Cathlab mgonjwa mwenye matatizo ya
mfumo wa umeme wa moyo wakati wa kambi maalum ya siku tano ya matibabu hayo.
Wataalam wa afya wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na
wenzao kutoka Shirika la Madaktari Afrika la nchini Marekani wakiangalia umeme
wa moyo unaoingia kwa mgonjwa unavyofanya kazi kwa kutumia mashine ya CRTD
Programmer wakati wa kambi maalum ya siku tano ya matibabu hayo. Jumla ya
wagonjwa 12 wameshapatiwa matibabu katika kambi hiyo.
Picha na: Khamis Mussa
************************************************************************************************************
Comments
Post a Comment