Posts

Showing posts from March, 2024

Mashabiki wa Arsenal Afrika watoa msaada wa milioni 16 na kuchangia damu JKCI

Image
  Mashabiki wa Arsenal Afrika  kutoka nchi za Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda, Zambia na Ethiopia wakiwa katika picha ya pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe. Edward Mpogolo pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge wakati washabiki hao walipotembelea JKCI leo kwa ajili ya kuchangia matibabu ya watoto wenye matatizo ya moyo pamoja na kutoa damu kwa ajili ya watoto wanaofanyiwa upasuaji. Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akipokea mfano wa hundi ya shilingi milioni 16 kutoka kwa Mwenyekiti wa  Mashabiki wa Arsenal Tanzania (ASCTZ) Raymond Anthony wakati mashabiki wa timu hiyo kutoka nchi za Afrika walipofika JKCI leo kwaajili ya kuchangia matibabu ya watoto wenye matatizo ya moyo pamoja na kutoa damu kwa ajili ya wanaofanyiwa upasuaji. Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe. Edward Mpogolo akizungumza na mashabiki wa   Arsenal Afrika  wakati mashabiki hao walipofika katika Taa...

Tiba mkoba ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu yampa fursa ya kugundua tatizo la moyo

Image

Tiba mkoba yamuwezesha kupata huduma za kibingwa JKCI

Image
Wataalamu wa afya wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakimfanyia mgonjwa upasuaji wa tundu dogo kwa kutumia mtambo wa cathlab kumuwekea kifaa cha kuusaidia moyo kufanya kazi vizuri (Pacemaker). Mgonjwa huyo alifanyiwa uchunguzi katika kambi maalumu ya matibabu ya moyo iliyofanyika Mkoani Kagera wiki iliyopita. Daktari bingwa wa moyo na mfumo wa umeme wa moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Yona Gandye akimuwekea mgonjwa kifaa cha kuusaidia moyo kufanya kazi vizuri (Pacemaker) kwa kutumia mtambo wa Cathlab. Mgonjwa huyo alifanyiwa uchunguzi katika kambi maalumu ya matibabu ya moyo iliyofanyika Mkoani Kagera wiki iliyopita. ******************************************************************************************** Mgonjwa aliyefanyiwa uchunguzi katika kambi maalumu ya matibabu ya moyo iliyofanyika mkoani Kagera wiki iliyopita awekewa kifaa cha kuusaidia moyo kufanya kazi vizuri “Pacemaker”. Mgonjwa huyo alikuwa na matatizo ya mfumo wa umeme wa moyo hivyo mapigo yake ya mo...

Dkt. Kisenge: Shinikizo la juu la damu linaua; Chukua tahadhari

Image
Mkurugenzi wa Huduma ya Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Robert Mallya akimpima Salome Majaliwa shinikizo la damu (BP) wakati wa maadhimisho ya siku ya shinikizo la juu la damu duniani ambayo hufanyika kila mwaka tarehe 17 mwezi wa tano. ********************************************************************************************************************************************************************************************* Na Anna Nkinda - JKCI Asilimia 25 ya vifo vya magonjwa ya moyo vinavyotokea duniani vinasababishwa na ugonjwa wa shinikizo la juu la damu . Hayo yamesemwa leo jijini Dar es Salaam na   Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge wakati akiongea na waandishi wa habari kuhusu mafanikio yaliyopatikana katika taasisi hiyo kwa kipindi cha miaka mitatu ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan. Dkt. Kisenge ambaye pia ni daktari bingwa wa magonjwa ya moyo alisema kwa kipin...

Wataalamu wa JKCI wapatiwa mafunzo ya kujikinga na kuwakinga wagojwa na maambukizi

Image
Mwezeshaji wa kitaifa wa mafunzo ya kuzuia maambukizi kutoka kwa mgonjwa kwenda kwa mtoa huduma na kutoka kwa mtoa huduma kwenda kwa mgonjwa (IPC) ambaye pia ni Daktari kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) Josephat Luyaga akiwafundisha wataalamu wa afya wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) namna ya kujikinga na maambukizi wakati wa mafunzo hayo ya siku tatu yaliyoanza leo katika ukumbi wa Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam. Mwezeshaji wa kitaifa wa mafunzo ya kuzuia maambukizi kutoka kwa mgonjwa kwenda kwa mtoa huduma na kutoka kwa mtoa huduma kwenda kwa mgonjwa (IPC) ambaye pia ni Afisa Uuguzi kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) Odillo Byabato akiwafundisha wataalamu wa afya wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) jinsi ya kujikinga na maambukizi wakati wa mafunzo hayo ya siku tatu yaliyoanza leo katika ukumbi wa Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam. Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Jilala Luchagula akichangia mada wakati wa mafunzo ya ...

Wagonjwa 361,894 watibiwa JKCI kwa kipindi cha miaka mitatu

Image
  Wataalamu wa magonjwa ya moyo na mishipa ya damu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na wenzao wa Hospitali ya Starcare ya nchini India wakifanya upasuaji mdogo wa moyo wa kubadilisha valvu ya mshipa mkubwa wa damu (Aortic Valve) bila kufungua kifua (Transcatheter Aortic Valve Implantation procedure – TAVI) katika kambi maalumu ya siku mbili ya matibabu ya moyo inayofanyika JKCI. Upasuaji huo mdogo wa kubadilisha valvu ulifanyika kwa mara ya kwanza hapa nchini. ********************************************************************************************************************************************************************************************************************* Jumla ya wagonjwa 361,894 watu wazima wakiwa 331,557 na watoto 30,337 wametibiwa kwa kipindi cha miaka mitatu katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) iliyopo jijini Dar es Salaam.   Kati ya wagonjwa hao 361,894 waliotibiwa katika taasisi hiyo wagonjwa waliolazwa walikuwa 13,325 huku watu...

Watu 447 wapimwa moyo Kagera

Image
Daktari wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Janeth Mmari na mwenzake wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Bukoba (BRRH) Martin Rwabilimbo wakimsikiliza mwananchi aliyefika BBRH kwaajili ya kupata huduma ya matibabu ya moyo wakati wa kambi maalumu ya siku tano ya uchunguzi na matibabu iliyomalizika hivi karibuni mkoani Kagera. Wataalamu wa Taaasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na wenzao wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Bukoba (BRRH) wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kumalizkia kwa kambi maalum ya upimaji na matibabu ya moyo iliyofanyika mkoani Kagera. Jumla ya watu 447 wakiwemo watu wazima 405 na watoto 42 walifanyiwa uchunguzi wa moyo katika kambi hiyo. Afisa Uuguzi wa Hospitali ya  Rufaa ya Mkoa Bukoba (BRRH) Ernest Lengesela akimpima kipimo cha kuangalia shinikizo la damu mwilini mwananchi aliyefika katika hospitali hiyo kwa ajili ya kupata huduma za matibabu ya moyo wakati wa kambi maalumu ya upimaji iliyofanywa na wataalamu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kus...

RC Mwasa: Wananchi Kagera changamkieni fursa ya kupima moyo

Image
Mkuu wa Mkoa wa Kagera Mhe. Hajati Fatma Mwasa akizungumza na wananchi waliofika katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Bukoba (BRRH) kwa ajili ya kupata huduma za matibabu ya moyo zinazotolewa na wataalamu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na wenzao wa BRRH wakati wa ufunguzi wa kambi maalumu ya siku tano ya uchunguzi na matibabu ya moyo ambapo hadi sasa watu 288 wameshapata huduma za matibabu. Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Yona Gandye akizungumza na wananchi waliofika katika Hospitali ya  Rufaa ya Mkoa Bukoba (BRRH) kwa ajili ya kupata huduma za matibabu ya moyo zinazotolewa na wataalamu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na wenzao wa BRRH wakati wa ufunguzi wa kambi maalumu ya siku tano ya uchunguzi na matibabu ya moyo ambapo hadi sasa watu 288 wameshapata huduma za matibabu.  Baadhi ya wakazi wa mkoa wa Kagera wakimsikiliza mkuu wa mkoa huo Mhe. Hajati Fatma Mwasa wakati wa ...

Kagera wafikiwa na huduma za kibingwa za matibabu ya moyo

Image
Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Yona Gandye   akizungumza na wataalamu wa afya wa   Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Bukoba (BRRH) pamoja na wa JKCI kabla ya kuanza kwa zoezi la siku tano la upimaji na matibabu ya moyo kwa wananchi wa mkoa wa Kagera. Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Bukoba (BRRH) Dkt. Museleta Nyakiroto akizungumza na wataalamu wa afya wa hospitali hiyo pamoja na wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kabla ya kuanza kwa zoezi la siku tano la upimaji na matibabu ya moyo kwa wananchi wa mkoa wa Kagera. Baadhi wa wananchi wa Kagera waliofika katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Bukoba (BRRH) wakisubiri kwenda kufanyiwa vipimo vya kuangalia jinsi moyo unavyofanya kazi (Echocardiography) na mfumo wa umeme wa moyo unavyofanya (Electrocardiography) wakati wa kambi maalumu ya siku tano ya upimaji na matibabu ya moyo kwa wananchi wa mkoa wa Kagera. Afisa Lishe waTaasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Maria Samlongo na M...

Wadau wakutana kujadili Mitaala ya mafunzo ya upasuaji wa moyo

Image
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akielezea namna JKCI na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) zitakavyotoa mafunzo kwa wataalamu wa afya wakati wa kikao cha kupitia mitaala ya program za mafunzo ya upasuaji wa moyo na upasuaji wa tundu dogo mwishoni mwa wiki katika Hoteli ya Serena iliyopo jijini Dar es Salaam Msajili kutoka Baraza la Madaktari la Tanganyika (MCT) Dkt. David Mzava akitoa maoni yake wakati wa kikao cha kupitia mitaala ya program za mafunzo ya upasuaji wa moyo na upasuaji wa tundu dogo zitakazofanywa na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) mwishoni mwa wiki katika Hoteli ya Serena iliyopo jijini Dar es Salaam Daktari bingwa wa upasuaji wa moyo na mishipa ya damu kwa watoto wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Godwin Sharau akichangia mada wakati wa kiako cha kupitia mitaala ya program za mafunzo ya upasuaji wa moyo na upasuaji wa tundu dogo zitakazofanywa na JKCI kw...

Wafurahia kufanyiwa ECHO na ECG bila malipo

Image
Mtaalamu wa afya kutoka Shirika la Cardiostart International la nchini Marekani Savannah Breaker pamoja na madaktari wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete Hospitali ya Dar Group Samweli Mbilinyi na Masanja James wakijadiliana baada ya kumfanyia mgonjwa kipimo cha kuangalia mfumo wa umeme wa moyo (ECG) wakati wa kambi maalumu ya siku mbili ya kufanya vipimo vya moyo kwa wananchi wa Dar es Salaam bila malipo iliyofanyika katika Hospitali ya JKCI Dar Group. Daktari wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete Hospitali ya Dar Group Marsia Tillya na mtaalamu wa afya kutoka Shirika la Cardiostart International la nchini Marekani Sarah King wakimfanyia kipimo cha kuangalia jinsi moyo unavyofanya kazi (ECHO) mwananchi aliyefika katika Hospitali hiyo wakati wa kambi maalumu ya siku mbili ya kufanya vipimo vya moyo kwa wananchi wa Dar es Salaam bila malipo. Baadhi ya wananchi wa mkoa wa Dar es Salaam wakiwa katika foleni ya kufanya vipimo vya moyo wakati wa kambi maalumu ya siku mbili ya kufanya vipimo vya mo...