Maboresho ya miundombinu yafanyika Hospitali ya JKCI Dar Group

Mhandisi wa vifaa tiba wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group Elpidius Prosper akiwaelezea viongozi wa taasisi hiyo maendeleo ya mradi wa mtambo wa kuzalisha oksijeni wakati viongozi wa taasisi hiyo walipotembelea miradi mbalimbali ya JKCI leo jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akizungumza na daktari wa huduma za dharura Hospitali ya JKCI Dar Group Nicole Kinyawa wakati wa ziara yake kutembelea miradi ya Taasisi hiyo leo jijini Dar es Salaam. Kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Hospitali ya JKCI Dar Group Dkt. Tulizo Shemu
Mhandisi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Lucas Paulo akiwaelezea viongozi wa taasisi hiyo maendeleo ya ukarabati wa chumba cha kufanyia upasuaji wakati viongozi wa taasisi hiyo walipotembelea miradi mbalimbali ya JKCI leo jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akizungumza na wafanyakazi wa Hospitali ya JKCI Dar Group wakati wa kikao cha wafanyakazi kujadili maendeleo ya Hospitali kilichofanyika leo jijini Dar es Salaam.

Baadhi ya Wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group wakifuatilia yaliyokuwa yakizungumzwa wakati wa kikao cha wafanyakazi kilichofanyika leo katika ukumbi wa Hospitali ya Dar Group iliyopo jijini Dar es Salaam.
Kaimu Mkurugenzi wa Hospitali ya JKCI Dar Group Dkt. Tulizo Shemu akielezea mafanikio ya Hospitali hiyo wakati wa kikao cha wafanyakazi wa Hospitali ya Dar Group kilichofanyika leo jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Fedha na Mipango wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete CPA. Agnes Kuhenga akifafanua jambo wakati wa kikao cha wafanyakazi wa Hospitali ya JKCI Dar Group kilichofanyika leo jijini Dar es Salaam.

Picha na: JKCI
************************************************************************************************************

Comments

Popular posts from this blog

Wateja wa CRDB kutibiwa JKCI kwa punguzo la asilimia 50%

Wanawake wa JKCI SACCOS wanaongoza kwa kumiliki hisa

JKCI, MOI NA MNH waitwa Comoro kutoa huduma za matibabu ya kibingwa