Bima ya afya kwa wote itawapunguzia wananchi kulipia gharama kubwa za matibabu ya moyo


 Waziri wa Afya Mhe. Jenista Mhagama akimsikiliza mtoto Ally Mwandu aliyefanyiwa upasuaji wa moyo katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) mara baada ya kumpatia ua la mkononi wakati alipowasili katika taasisi hiyo leo kwaajili ya kuangalia utoaji wa huduma  na mwelekeo wa taasisi hiyo tangu alipoteuliwa kuwa waziri wa afya mwezi Agosti mwaka huu.


Waziri wa Afya Mhe. Jenista Mhagama akiwa katika picha ya pamoja na wataalamu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI)  na kituo cha Mfalme Salman cha Misaada ya Kibinadamu cha nchini Saudi Arabia  alipotembelea JKCI leo kwaajili ya kuangalia utoaji wa huduma  na mwelekeo wa taasisi hiyo tangu alipoteuliwa kuwa waziri wa afya mwezi Agosti mwaka huu. 


Waziri wa Afya Mhe. Jenista Mhagama akizungumza na ndugu wa wagonjwa wanaotibiwa katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI)  wakati alipotembelea JKCI leo  JKCI leo kwaajili ya kuangalia utoaji wa huduma  na mwelekeo wa taasisi hiyo tangu alipoteuliwa kuwa waziri wa afya mwezi Agosti mwaka huu.


Waziri wa Afya Mhe. Jenista Mhagama akitembelea maeneo mbalimbali ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI)  wakati wa ziara yake aliyoifanya leo katika taasisi hiyo  
JKCI leo kwaajili ya kuangalia utoaji wa huduma  na mwelekeo wa taasisi hiyo tangu alipoteuliwa kuwa waziri wa afya mwezi Agosti mwaka huu.


Waziri wa Afya Mhe. Jenista Mhagama akizungumza na wagonjwa wanaotibiwa katika  Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI)  wakati wa ziara yake aliyoifanya leo katika taasisi hiyo  kwaajili ya 
 kuangalia utoaji wa huduma  na mwelekeo wa taasisi hiyo tangu alipoteuliwa kuwa waziri wa afya mwezi Agosti mwaka huu.


Waziri wa Afya Mhe. Jenista Mhagama akizungumza na wazazi ambao watoto wao wamelazwa katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI)  wakati wa ziara yake aliyoifanya leo katika taasisi hiyo leo kwaajili ya kuangalia utoaji wa huduma  na mwelekeo wa taasisi hiyo tangu alipoteuliwa kuwa waziri wa afya mwezi Agosti mwaka huu.


Waziri wa Afya Mhe. Jenista Mhagama akimsikiliza Mkurugenzi wa Tiba Shirikishi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI)  Dkt. Delilah Kimambo kuhusu ujenzi wa jengo la utawala na vipimo unaofanyika katika taasisi hiyo wakati wa ziara yake aliyoifanya leo katika taasisi hiyo  kwaajili ya kuangalia utoaji wa huduma  na mwelekeo wa taasisi hiyo tangu alipoteuliwa kuwa waziri wa afya mwezi Agosti mwaka huu.

******************************************************************************************************************************************************************************************

Na Stela Gama - JKCI

Kuanza kutumika kwa bima ya afya kwa wote kutasaidia kupunguza gharama za matibabu ya kibingwa yakiwemo ya moyo na hivyo kuwaondolea  wananchi mzigo mkubwa wa kulipia gharama hizo.

Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dar es Salaam na Waziri wa Afya Mhe. Jenista Mhagama wakati akizungumza na wagonjwa wanaotibiwa katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) alipofanya ziara ya kuangalia utoaji wa huduma na mwelekeo wa taasisi hiyo tangu alipoteuliwa kuwa waziri wa afya mwezi Agosti mwaka huu.

 Waziri Mhagama  alisema gharama za matibabu ya kibingwa ni kubwa na Serikali imekuwa na jukumu kubwa la kulipia gharama za matibabu kwa watu wasiokuwa na uwezo wa kulipia lakini kuanza kutumia kwa bima ya afya kwa wote kutawasaidia wananchi kupata huduma mahali popote walipo hata kama hawatakuwa na fedha mfukoni kipindi ambacho wataugua.

 “Ninawaomba bima ya afya kwa wote ikianza kutumika mjiunge kwani itawasaidia kupata matibabu mahali popote pale mlipo na itasaidia  kufuatilia matibabu ya  mgonjwa kutoka hospitali yoyote nchini kwani mfumo wa matibabu utakaotumika utakuwa ni mmoja”.

 “Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameendelea kusaidia mfuko unaohudumia watanzania kuweza kufikiwa na matibabu haya ya kibobezi kwa kutoa zaidi ya shilingi bilioni 6 ili ziweze kusaidia katika utoaji wa huduma hizo na kuanzisha mfumo wa bima ya afya kwa wote”, alisema Mhe. Jenista.

 Aidha Waziri Mhagama aliwapongeza wafanyakazi wa Taasisi hiyo kwa kazi nzuri wanazozifanya na ubunifu walionao katika kutoa tiba hapa nchini na kuona ni muhimu kuwe na mfumo wa kuzizawadia hospitali zinafanya ubunifu wa namna yoyote  kila mwaka ili kuweza kuhamasisha maendeleo katika sekta ya afya nchini.

 Mhe. Waziri huyo wa Afya alisema Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) ni taasisi pekee inayoongoza na yenye sifa na heshima ya kutoa matibabu ya kibobezi ya moyo hasa kwa ukanda wa Afrika Mashariki na Kati hivyo basi aliwaomba wataalamu wa Taasisi hiyo kuendelea kutoa huduma hizo kwa kujitoa kwani wagonjwa wanawategemea wao katika kuokoa maisha yao.

“Ninawasihi uongozi wa JKCI mjitahidi  kukuza shughuli na huduma zinazofanywa hapa ikiwemo kutoa huduma mpya za kibingwa mara kwa mara kwa kufanya hivyo mtapata wagonjwa wengi kutoka nje ya nchi na kuendelea kuimarisha utalii wa tiba kwani wagonjwa wengi watakuja kutibiwa hapa”, alisisitiza Mhe. Mhagama.

 Kwa upande wa wagonjwa wanaotibiwa katika taasisi hiyo walishukuru kwa huduma ya matibabu ya moyo wanayoipata na kusema kuwa kwa kiwango kikubwa imesaidia kuokoa maisha yao na ya  watoto wao wenye matatizo ya moyo. 

Happy Nkinda kutoka mkoani Geita alimwambia waziri huyo wa Afya kuwa  mtoto wake alikuwa akisumbuliwa na tatizo la tundu dogo kwenye moyo kwa muda mrefu na kumpeleka hospitali mbalimbali bila mafaniko mpaka pale alipopewa rufaa ya kwenda JKCI.

“Namshukuru sana Mungu, mara baada ya mtoto wangu kupatiwa matibabu kwa sasa anaendelea vizuri, pia nawashukuru waatalamu wa JKCI kwa huduma zao nzuri na ushirikiano wao kipindi chote cha matibabu”, alisema Happy. 

“ Mtoto wangu aligunduliwa kuwa na shida ya moyo katika moja ya hospitali iliyopo mkoani Mara na kupewa rufaa kuja JKCI ambapo aligundulika kuwa na tundu kwenye moyo, namshukuru Mungu na wataalamu wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete kwa kumfanyia upasuaji na sasa anaendelea vizuri”, alisema Edna.

 Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge alimshukuru Mhe. Waziri wa Afya Jenista Mhagama  kwa kutembembelea Taasisi hiyo na  kuona uwekezaji mkubwa ambao umefanywa na Serikali katika kutoa tiba ya magonjwa ya moyo  pamoja na kuwekeza katika rasilimali watu. 

“Taasisi yetu ni  moja ya taasisi bora za afya katika nchi za Afrika Mashariki na Kati hivyo mheshimiwa Waziri amekuja kuona huduma tunazozitoa, na wagonjwa wengi aliowauliza maswali walimjibu kuwa wameridhika na huduma tunazozitoa  na hii inaonesha ni jinsi gani wataalamu wa JKCI wanavyotoa huduma bora  kwa wagonjwa wanaowahudumia”, alisema Dkt. Kisenge.

 Dkt. Kisenge alisema wao kama taasisi wataendelea kuimarisha teknolojia ya matibabu ili waweze kuwafikia wananchi wengi zaidi hasa maeneo ambayo ni vigumu kwa wananchi kupata huduma za kibingwa za matibabu ya moyo.

Mkurugenzi huyo Mtendaji ambaye pia ni daktari bingwa wa magonjwa ya moyo na mishipa ya damu alisema kutokana na uwekezaji mkubwa wa vifaa tiba na rasiimali watu uliofanyika katika taasisi hiyo  umechangia kwa kiasi kikubwa kuleta wagonjwa kutoka nchi mbalimbali kuja kupata matibabu hapa nchini.

 

  

Comments

Popular posts from this blog

Wataalamu wa JKCI kufanya upasuaji wa moyo nchini Zambia

JKCI na AICC Hospitali kutoa huduma za uchunguzi na matibabu ya moyo katika kikao kazi cha wenyeviti na watendaji wakuu wa Taasisi za Umma

JKCI yamshukuru Rais Dkt.Samia kwa kuwapa magari