Posts

Showing posts from April, 2025

Watu milioni 4.9 nchini husumbuliwa na magonjwa ya moyo

Image
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akimuelezea Makamu wa pili wa Rais Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla namna wanavyofanya upasuaji wa kubadilisha valvu ya moyo bila kufungua kifua wakati wa ufunguzi wa mkutano wa tatu wa kimataifa wa magonjwa ya moyo uliofanyika jana mjini Zanzibar. Afisa masoko kutoka kampuni ya Snibe Diagnostic Vonnie Feng akimuelezea Makamu wa pili wa Rais Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla huduma zinazotolewa na kampuni hiyo wakati wa ufunguzi wa mkutano wa tatu wa kimataifa wa magonjwa ya moyo uliofanyika jana mjini Zanzibar.   Kaimu Mtendaji Mkuu wa shirika lisilo la kiserikali Heart Team Africa Foundation (HTAF) Linda Gideon akimuonesha mmoja wa washiriki wa mkutano wa tatu wa kimataifa wa magonjwa ya moyo bidhaa zinazouzwa na shirika hilo kwaajili ya kukusanya fedha za matibabu ya watoto wenye magonjwa ya moyo wanaotibwa katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI...

JKCI yapata tuzo utoaji huduma bora za Afya 2025 ngazi ya hospitali maalum na Taifa

Image
Waziri wa Afya Mhe. Jenista Mhagama akimkabidhi tuzo ya mshindi wa utoaji wa huduma bora za Afya mwaka 2025 kundi la Hospitali maalumu na Taifa Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge wakati wa maadhimisho ya wiki ya Afya Kitaifa iliyohitimishwa leo jijini Dodoma. Waziri wa Afya Mhe. Jenista Mhagama akizungumza na mtoto Naima Kasiki aliyewahi kufanyiwa upasuaji wa moyo katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) alipotembelea banda la Taasisi hiyo wakati wa maadhimisho ya wiki ya Afya Kitaifa yaliyohitimishwa leo jijini Dodoma Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akimuelezea Waziri wa Afya huduma za utalii tiba zinazofanywa na Taasisi hiyo alipotembelea banda la JKCI wakati wa maadhimisho ya wiki ya Afya Kitaifa yaliyohitimishwa leo jijini Dodoma Wananchi wa mkoa wa Dodoma wakipata elimu kuhusu magonjwa ya moyo kutoka kwa wataalamu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) walipotembelea banda la Taasisi...

Utalii tiba waongeza idadi ya wagonjwa wanaotibiwa JKCI

Image
Afisa kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Adam Sembe akimuelezea mwananchi wa Dodoma huduma za utalii tiba zinazotolewa na Taasisi hiyo wakati wa maonesho ya kuadhimisha wiki ya afya kitaifa yanayofanyika katika kituo cha Mikutano cha Jakaya Kikwete kilichopo jijini Dodoma. Wananchi wa Dodoma wakipata elimu kuhusu magonjwa ya moyo katika banda la Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakati wa maonesho ya kuadhimisha wiki ya afya kitaifa yanayofanyika katika kituo cha Mikutano cha Jakaya Kikwete kilichopo jijini Dodoma. Na: JKCI ********************************************************************************************** Upatikanaji wa huduma za Utalii tiba katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) umesaidia kuongeza idadi ya wagonjwa wa nje ya nchi kutoka wagonjwa 316 mwaka 2023 hadi kufikia wagonjwa 689 mwaka 2024 wanaotibiwa na Taasisi hiyo. Hayo yamesemwa na Daktari bingwa wa upasuaji wa moyo na mishipa ya damu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Alex Benjamini wa...

Watu 249 wachunguzwa na kutibiwa moyo Zanzibar

Image
Afisa Muuguzi wa  Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Happy Mabonka akimuonesha huduma zinazotolewa na taasisi hiyo Afisa Muuguzi wa Hospitali ya Magogoni Saida Sadifa  wakati wa kambi maalumu ya upimaji na matibabu ya moyo iliyofanyika kwa siku nne  katika uwanja wa Amaani Zanzibar.  Watu 249 walipata huduma za uchunguzi na matibabu ya moyo  katika katika upimaji huo uliokwenda sambamba na kikao kazi cha 20 cha Maafisa Habari, Uhusiano na Itifaki wa Serikali. Hadija Said mkazi wa Daraja Bovu akimuonesha daftari lililoandikwa dawa za moyo anazozitumia Daktari wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dotto Sebastian wakati wa kambi maalumu ya upimaji na matibabu ya moyo iliyofanyika katika uwanja wa Amaani Zanzibar. Watu 249 walipata huduma za uchunguzi na matibabu ya moyo katika katika upimaji huo uliokwenda sambamba na kikao kazi cha 20 cha Maafisa Habari, Uhusiano na Itifaki wa Serikali. Wakazi wa Zanzibar wakiwa katika foleni ya kwenda kumuona ...

Ukuaji wa teknolojia wachochea ufanisi matibabu ya moyo

Image
Baadhi ya wadau wa sekta ya afya wakifuatilia mada inayohusu magonjwa ya moyo wakati wa mdahalo wa kitaaluma (Symposium) uliofanyika jana katika kituo cha mikutano cha Jakaya Kikwete  katika kuadhimisha ya wiki ya Afya kitaifa  **************************************************************************************** Imeelezwa kuwa ukuaji na maendeleo ya Teknolojia umechochea kwa kiwango kikubwa katika ufanisi wa kutoa huduma za uchunguzi na matibabu ya magonjwa ya moyo hapa nchini. Hayo yamebainishwa   jana Jijini Dodoma na Mkurugenzi wa Upasuaji wa Moyo kutoka Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Angela Muhozya wakati akitoa wasilisho kwenye mdahalo wa Kitaaluma (Symposium) uliofanyika wakati wa maadhimisho ya Wiki ya Afya Kitaifa. Dkt. Angela alisema matumizi ya Teknolojia yamekuwa na ufanisi mkubwa kwenye matibabu ya magonjwa ya moyo kwani kwa kutumia simu Janja App mwananchi anaweza kupima mapigo ya moyo, shinikizo la damu na umeme wa moyo.   “Serika...

JKCI yatoa huduma za matibabu ya moyo bila malipo Zanzibar

Image
   Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Aika Nnkya akimuonyesha mkazi wa Zanzibar kipimo cha kuangalia jinsi moyo wake unavyofanya kazi wakati wa zoezi la upimaji na matibabu ya magonjwa ya moyo bila malipo linalofanyika     katika uwanja wa Amaani. Daktari wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dotto Sebastian akimpatia dawa za moyo mkazi wa Zanzibar aliyefika   katika uwanja wa Amaani kupata huduma za uchunguzi na matibabu ya moyo zinazotolewa bila malipo katika kikao kazi cha 20 cha Maafisa Habari, Uhusiano na Itifaki wa Serikali.

Wakazi wa Zanzibar watakiwa kujitokezeni kupimwa afya ya moyo

Image
Afisa Muuguzi wa  Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Happy Mabonka akimpima shinikizo la damu mkazi wa Zanzibar aliyefika katika uwanja wa Amaani kwaajili ya kupata huduma za uchunguzi na matibabu ya moyo zinazotolewa bila malipo na wataalamu wa taasisi hiyo katika kikao kazi  cha 20 cha Maafisa Habari, Uhusiano na Itifaki wa Serikali kilichoandaliwa na Idara za Habari - Maelezo za Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar. Afisa Muuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Happy Mabonka akizungumza na wakazi wa Zanzibar waliokuwa wanasubiri kumuona daktari wakati wa zoezi la upimaji na matibabu ya moyo linalofanyika katika  uwanja wa Amaani. ************************************************************************************************************************************************************************************************************************ Wakazi wa Zanzibar wametakiwa kujitokeza kwa wingi kupata huduma za kibingw...