Watu milioni 4.9 nchini husumbuliwa na magonjwa ya moyo

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akimuelezea Makamu wa pili wa Rais Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla namna wanavyofanya upasuaji wa kubadilisha valvu ya moyo bila kufungua kifua wakati wa ufunguzi wa mkutano wa tatu wa kimataifa wa magonjwa ya moyo uliofanyika jana mjini Zanzibar. Afisa masoko kutoka kampuni ya Snibe Diagnostic Vonnie Feng akimuelezea Makamu wa pili wa Rais Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla huduma zinazotolewa na kampuni hiyo wakati wa ufunguzi wa mkutano wa tatu wa kimataifa wa magonjwa ya moyo uliofanyika jana mjini Zanzibar. Kaimu Mtendaji Mkuu wa shirika lisilo la kiserikali Heart Team Africa Foundation (HTAF) Linda Gideon akimuonesha mmoja wa washiriki wa mkutano wa tatu wa kimataifa wa magonjwa ya moyo bidhaa zinazouzwa na shirika hilo kwaajili ya kukusanya fedha za matibabu ya watoto wenye magonjwa ya moyo wanaotibwa katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI...