Banda la JKCI lawavutia wananchi kupima moyo


Naibu katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na wenye Ulemavu Zuhura Yunus akiwa katika picha ya Pamoja na wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) alipotembelea banda la JKCI kwaajili ya kuangalia huduma wanazozitoa katika  maonesho ya Kimataifa ya Wiki ya Usalama na Afya Mahali Pa kazi yanayofanyika katika viwanja vya Mandewa mkoani Singida.


Afisa Muuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group Fatma Joseph akimpima shinikizo la damu (BP) mkazi wa Singida aliyefika katika viwanja vya maonesho Mandewa kwaajili ya kupata huduma za uchunguzi na matibabu ya moyo zinazotolewa bila malipo katika Maonesho ya Kimataifa ya Wiki ya Usalama na Afya Mahali Pa Kazi.

Mkurugenzi wa Usalama na Afya kutoka Wakala wa Usalama na Afya Mahala pa Kazi (OSHA) Dkt. Jerome Materu akisaini kitabu cha wageni alipotembelea banda la Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakati wa maonesho ya Kimataifa ya Wiki ya Usalama na Afya Mahali Pa kazi yanayofanyika katika viwanja vya Mandewa mkoani Singida.

Mkazi wa Singida akipewa ushauri wa kiafya kuhusiana na magonjwa ya moyo kutoka kwa  daktari bingwa wa magonjwa yatokanayo na kazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group Elias Birago wakati wa maonesho  ya Kimataifa ya Wiki ya Usalama na Afya Mahali Pa kazi yanayofanyika katika  viwanja vya maonesho  Mandewa mkoani Singida.

Afisa Muuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group Fatma Joseph akimpima kiwango cha sukari kwenye damu mtoto aliyefika na wazazi wake katika banda la JKCI  kwaajili ya kupata huduma za uchunguzi na matibabu ya moyo zinazotolewa katika maonesho ya Kimataifa ya Wiki ya Usalama na Afya Mahali Pa kazi yanayofanyika mkoani Singida.

 

Comments

Popular posts from this blog

JKCI na AICC Hospitali kutoa huduma za uchunguzi na matibabu ya moyo katika kikao kazi cha wenyeviti na watendaji wakuu wa Taasisi za Umma

JKCI yapata tuzo ya taasisi ambayo imetoa mchango wa kipekee kiuchumi na kijamii katika kuleta matokeo makubwa kwa kipindi cha mwaka 2023/2024

Wafanyakazi waliohama JKCI waagwa