Viongozi watembelea banda la JKCI maonesho ya Osha

Afisa Muuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group Fatma Joseph akimpima shinikizo la damu (BP) na kiwango cha oksijeni mwilini Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na wenye Ulemavu Zuhura Yunus aliyetembelea banda la taasisi hiyo wakati wa maonesho ya Kimataifa ya Wiki ya Usalama na Afya Mahali Pa kazi yanayofanyika katika viwanja vya Mandewa mkoani Singida.


Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na wenye Ulemavu Zuhura Yunus akisaini kitabu cha wageni alipotembelea banda la Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwaajili ya kuangalia huduma za uchunguzi na matibabu ya moyo wanazozitoa katika maonesho ya Kimataifa ya Wiki ya Usalama na Afya Mahali Pa kazi yanayofanyika katika viwanja vya Mandewa mkoani Singida.

Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu Dkt. Edith Rwiza akisaini kitabu cha wageni alipotembelea banda la Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kupata huduma ya uchunguzi na matibabu ya moyo katika maonesho ya Kimataifa ya Wiki ya Usalama na Afya Mahali Pa kazi yanayofanyika katika viwanja vya Mandewa mkoani Singida.

Picha na: Jeremiah Ombelo

*************************************************************************************************************************


Comments

Popular posts from this blog

JKCI na AICC Hospitali kutoa huduma za uchunguzi na matibabu ya moyo katika kikao kazi cha wenyeviti na watendaji wakuu wa Taasisi za Umma

JKCI yapata tuzo ya taasisi ambayo imetoa mchango wa kipekee kiuchumi na kijamii katika kuleta matokeo makubwa kwa kipindi cha mwaka 2023/2024

Wafanyakazi waliohama JKCI waagwa