Kamati ya kudumu ya bunge ya Afya na masuala ya Ukimwi yatembelea JKCI



Daktari Bingwa wa magonjwa ya moyo kwa watoto wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Deogratis Nkya akiwaonesha wajumbe wa kamati ya kudumu ya  bunge ya Afya na masuala ya Ukimwi  jinsi wanavyofanya upasuaji wa kuzibua tundu la moyo wa mtoto bila ya kufungua kifua wakati kamati hiyo ilipofanya ziara ya kutembelea JKCI  kwa ajili ya kuona huduma mbalimbali za matibabu ya moyo zinazotolewa. Kulia kwa Dkt. Nkya  ni makamu Mwenyekiti wa kamati hiyo Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile Mbunge wa Kigamboni.

Daktari bingwa wa upasuaji wa moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Alex Joseph akiwaeleza wajumbe wa kamati ya kudumu ya  bunge ya Afya na masuala ya Ukimwi aina za upasuaji wa moyo zinazofanyika katika Taasisi hiyo wakati kamati hiyo ilipotembelea JKCI  kwa ajili ya kuona huduma mbalimbali za matibabu ya moyo zinazotolewa.

Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) ambaye pia ni misimamizi wa wodi ya watoto Theresia Marimo akiwaeleza wajumbe wa kamati ya kudumu ya  bunge ya Afya na masuala ya Ukimwi huduma za matibabu ya moyo wanazozipata watoto waliolazwa katika wodi hiyo.

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akiwaongoza wajumbe wa kamati ya kudumu ya  bunge ya Afya na masuala ya Ukimwi kwenda kuona ujenzi wa jengo la utawala na vipimo unavyoendelea. Kushoto kwa Mkurugenzi  ni Makamu Mwenyekiti wa kamati hiyo Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile Mbunge wa Kigamboni.


Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu akizungumza na wajumbe wa kamati ya kudumu ya  bunge ya Afya na masuala ya Ukimwi wakati kamati hiyo ilipofanya ziara ya kutembelea Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa ajili ya kuona huduma mbalimbali za matibabu ya moyo zinazotolewa. Kulia kwa Mhe. Waziri ni Makamu Mwenyekiti wa kamati hiyo Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile Mbunge wa Kigamboni  na kushoto ni Naibu Waziri wa Afya Mhe. Dkt.Godwin Mollel.

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akisoma taarifa ya utendaji kazi wa Taasisi hiyo kwa wajumbe wa kamati ya kudumu ya  bunge ya Afya na masuala ya Ukimwi wakati kamati hiyo ilipofanya ziara ya kutembelea JKCI  kwa ajili ya kuona huduma mbalimbali za matibabu ya moyo zinazotolewa.


Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya  bunge ya Afya na masuala ya Ukimwi Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile Mbunge wa Kigamboni  akizungumza na vyombo vya habari wakati kamati hiyo ilipofanya ziara ya kutembelea Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI)  kwa ajili ya kuona huduma mbalimbali za matibabu ya moyo zinazotolewa.

Picha na Khamisi Mussa 









 

Comments

Popular posts from this blog

JKCI na AICC Hospitali kutoa huduma za uchunguzi na matibabu ya moyo katika kikao kazi cha wenyeviti na watendaji wakuu wa Taasisi za Umma

JKCI yapata tuzo ya taasisi ambayo imetoa mchango wa kipekee kiuchumi na kijamii katika kuleta matokeo makubwa kwa kipindi cha mwaka 2023/2024

Maabara ya JKCI yapata ithibati ya kimataifa (ISO 15189:2012)