Posts

Showing posts from July, 2025

JKCI kuanza mchakato wa upandikizaji wa moyo

Image
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akimkabidhi mfano wa moyo Mwenyekiti wa kamati ya upandikizaji wa moyo Dkt. Everist Nyawawa wakati wa uzinduzi wa kamati hiyo leo katika ukumbi wa JKCI uliopo jijini Dar es Salaam Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akiwajulia hali wanachama wa chama cha wagonjwa wa moyo nchini wakati wa uzinduzi wa kamati ya upandikizaji wa moyo uliofanyika leo katika ukumbi wa JKCI uliopo jijini Dar es Salaam Baadhi ya wanachama wa chama cha wagonjwa wa moyo nchini wakisikiliza wakati wa uzinduzi wa kamati ya upandikizaji wa moyo uliofanyika leo katika ukumbi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) uliopo jijini Dar es Salaam. Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akiwa katika picha ya pamoja na wahariri wa vyombo vya habari mara baada kumalizika kwa uzinduzi wa kamati ya upandikizaji wa moyo leo katika ukumbi wa Taasisi hiyo uliopo jij...

Tanzania yashiriki maonesho ya 97 ya Kilimo na Biashara ya Zambia

Image
 Balozi wa Tanzania nchini Zambia Mhe. Luteni Generali Mathew Edward Mkingule akipokea zawadi ya picha ya moyo kutoka kwa Daktari bingwa wa upasuaji wa moyo na mishipa ya damu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Alex Joseph alipotembelea banda la taasisi hiyo leo katika maonesho ya 97ya Kilimo na Biashara ya Zambia yanayofanyika jijini Lusaka. Kushoto ni daktari bingwa wa magonjwa ya moyo kwa watoto wa Taasisi hiyo Amanda Anyoti. Madakatari bingwa wa moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Alex Joseph na Amanda Anyoti wakiwaeleza majaji wa maonesho ya 97 ya Kilimo na Biashara ya Zambia huduma zinazotolewa na taasisi hiyo katika maonesho hayo yanayofanyika jijini Lusaka. Madakatari bingwa wa moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Alex Joseph na Amanda Anyoti wakizungumza na wakazi wa Zambia waliofika katika banda la taasisi hiyo kwa ajili ya kupata elimu ya magonjwa ya moyo pamoja na kufahamu huduma zinazotolewa na taasisi hiyo wakati wa maonesho ya 97 ya Kilimo na...

JKCI yaandaa mpango mkakati utalii tiba

Image
Wajumbe wa kamati ya utalii tiba ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakifanya majadiliano wakati wa kikao cha kuandaa mpango mkakati wa utalii tiba wa Taasisi hiyo kilichomalizika mwishoni mwa wiki mkoani Morogoro.    Mjumbe wa kamati ya utalii tiba ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Halifa Abdallah akichangia mada wakati wa kikao cha kuandaa mpango mkakati wa utalii tiba wa Taasisi hiyo kilichomalizika mwishoni mwa wiki mkoani Morogoro. Na: JKCI ******************************************************************************************************** Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) yaandaa mpango mkakati wa utalii tiba wa kuhakikisha tiba utalii Tanzania inashika hatamu kwa kutumia teknolojia katika kutoa huduma kwa wagonjwa wa ndani na nje ya nchi. Mpango mkakati huo ulioandaliwa kwa siku tatu na wajumbe wa kamati ya utalii tiba wa Taasisi hiyo umelenga kuitikia wito wa Mhe. Rais Dkt. Samia Sululhu Hassan kuhakikisha tiba utalii Tanzania inakuwa. Akizungu...

Heart Team Africa Foundation Yalenga Kuokoa Maisha ya Watoto Wenye Magonjwa ya Moyo

Image
Mwenyekiti wa Bodi ya Heart Team Africa Foundation (HTAF) Mhe. Mussa Zungu akizungumza   wakati wa kikao cha kwanza cha bodi ya wakurugenzi wa Heart team Africa Foundation (HTAF) kilichofanyika Protea Hotel iliyopo Jijini Dar es Salaam. Mwenyekiti wa Bodi ya Heart Team Africa Foundation (HTAF) Mhe. Mussa Zungu akiwa kwenye picha ya Pamoja na wajumbe wa bodi ya wakurugenzi wa shirika lisilo la kiserikali la Heart Team Africa Foundation (HTAF) baada ya kikao cha kwanza cha bodi ya wakurugenzi katika Hoteli ya Protea iliyopo jijini Dar es Salaam. Wajumbe wa bodi ya wakurugenzi wa shirika lisilo la kiserikali Heart Team Africa Foundation (HTAF) wakimsikiliza Mtendaji Mkuu wa Heart Team Africa Foundation (HTAF) Dkt. Naizihijwa Majani wakati akitoa ripoti kuhusu taasisi hiyo katita hoteli ya Protea iliyopo jijini Dar es Salaam. Mwenyekiti wa Bodi ya Heart Team Africa Foundation (HTAF) Mhe. Mussa Zungu na moja ya muasisi wa Heart Team Africa Foundation (HTAF) Dkt. Peter Kisenge wakisikili...

JKCI kutumia akiliunde kumtambua mtu kama atakuwa na magonjwa ya moyo baada ya miaka 10 ijayo

Image
Mkurugenzi wa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Robert Mallya akizungumza na Mkurugenzi wa Kampuni ya AtheroPoint ya nchini Marekani Dkt. Jasjit Suri alipotembelea taasisi hiyo jana kwaajili ya kuona namna watakavyotumia akiliunde kufanya uchunguzi utakaotambua hatari ya mtu kupata magonjwa ya moyo na mishipa ya damu baada ya miaka 10 ijayo. Mkuu wa Kitengo cha Maabara wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Thadeo Kavishe akimweleza Mkurugenzi wa Kampuni ya AtheroPoint ya nchini Marekani Dkt. Jasjit Suri vipimo vinavyofanyika katika maabara hiyo wakati Mkurugenzi huyo alipotembelea taasisi hiyo jana kwaajili ya kuona namna watakavyotumia akiliunde kufanya uchunguzi utakaotambua hatari ya mtu kupata magonjwa ya moyo na mishipa ya damu baada ya miaka 10 ijayo. Mkuu wa Kitengo cha magonjwa ya moyo kwa watu wazima Dkt. George Longopa akimweleza Mkurugenzi wa Kampuni ya AtheroPoint ya nchini Marekani Dkt. Jasjit Suri jinsi huduma za uchunguzi na upasuaji wa moyo kwa njia ya ...

Wafanyakazi wa JKCI wafundishwa namna ya kudhibiti wa msongo wa mawazo

Image
Mtaalamu wa Saikolojia na Mahusiano kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Dkt. Chris Mauki akiwafundisha wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) namna ya kukabiliana na msongo wa mawazo pamoja na kuweka mipaka ya kazi na mambo binafsi. Mafunzo hayo ya siku moja yalifanyika hivi karibuni   katika ukumbi wa mikutano wa Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam. Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akizungumza na wafanyakazi wa Taasisi hiyo wakati wa mafunzo ya udhibiti wa msongo wa mawazo yaliyofanyika hivi karibuni katika ukumbi wa mikutano Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam. Baadhi ya wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakisikiliza mafunzo ya udhibiti wa msongo wa mawazo yaliyokuwa yanatolewa na Mtaalamu wa Saikolojia na Mahusiano kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Dkt. Chris Mauki. Mafunzo hayo ya siku moja yalifanyika hivi karibuni    katika ukumbi wa mikutano wa Taasisi hiyo iliyopo jijini ...

Wafanyakazi wa JKCI wapewa mafunzo ya Uzalendo, Mawasiliano ndani ya Serikali na Uadilifu

Image
Mwezeshaji wa mafunzo ya Uzalendo, Mawasiliano ndani ya Serikali  na Uadilifu Balozi Omar Kashera akizungumza na wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakati wa mafunzo hayo ya siku moja yaliyofanyika jana katika ukumbi wa mikutano wa Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa JKCI Dkt. Peter Kisenge. Wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakisikiliza mafunzo ya Uzalendo, Mawasiliano ndani ya Serikali na Uadilifu yaliyokuwa yanatolewa jana na Balozi Omar Kashera katika ukumbi wa mikutano wa Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam.

Watu 1,369 wafanyiwa uchunguzi wa moyo maonesho ya Sabasaba

Image
Afisa Uuguzi kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group France Kapele akimfundisha mwananchi  namna ya kutoa huduma ya kwanza kwa mgonjwa wa dharura alipotembelea banda la Taasisi hiyo wakati wa maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba) yaliyomalizika hivi karibuni katika viwanja vya Mwalimu Nyerete barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam. Mjumbe wa Taasisi isiyo ya Kiserikali ya Heart Team Africa Foundation (HTAF) Irene Mbonde akizungumza na wananchi waliofika katika banda la taasisi hiyo kwaajili ya kuchangia  matibabu ya watoto wenye magonjwa ya moyo wanaotibiwa na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakati wa maonesho Sabasaba yaliyomalizika hivi karibuni jijini Dar es Salaam. *************************************************************************************************************************************************************************************** Watu 1,369 wakiwemo watu wazima 1,289 na watoto 80 wamepata hudum...

JKCI yaihamasisha jamii kupata chanjo ya homa ya ini

Image
Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Florah Kasembe akitoa elimu kuhusu namna ya kujikinga na magonjwa ya moyo kwa wananchi waliotembelea banda la Taasisi hiyo wakati wa Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (SABASABA). Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Agnes Kajangwa akimpima wingi wa sukari kwenye damu mwananchi aliyetembelea banda la Taasisi hiyo wakati wa maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (SABASABA) yanayoendelea katika viwanja vya Mwalimu Nyerere vilivyopo barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam. Mhasibu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) DianaRose Kaugila akizungumza na mwananchi aliyefika katika banda la Taasisi hiyo kwaajili ya kufanya uchunguzi wa magonjwa ya moyo wakati wa maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (SABASABA) yanayoendelea katika viwanja vya Mwalimu Nyerere vilivyopo barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam. Mtunza kumbukumbu za Afya ambaye pia ni mjumbe wa kamati ...

JKCI kuwajengea uwezo wataalamu wa Hospitali ya Benjamini Mkapa

Image
  Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge na Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Benjamini Mkapa (BMH) Prof. Abel Makubi wakisaini    makubaliano ya ushirikiano wa matibabu ya ubingwa bobezi wa magonjwa ya moyo kwa kutumia uwezo wa wataalamu wa ndani ya nchi. Makubaliano hayo yalisainiwa jana katika Hospitali ya Benjamini Mkapa iliyopo jijini Dodoma.  Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akimkabidhi Waziri wa Afya Mhe. Jenista Mhagama ripoti ya kambi maalumu ya matibabu iliyofanyika Visiwani Comoro na wataalamu kutoka JKCI, Hospitali ya Benjamini Mkapa (BMH), Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo Muhimbili (MOI) na Taasisi ya Saratani Ocean Road.  Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge na Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Benjamini Mkapa (BMH) Prof. Abel Makubi wakikabidhiana hati ya   makubaliano ya...

Wananchi wahimizwa kuchangia matibabu ya watoto wenye magonjwa ya mo

Image
Mjumbe wa Taasisi isiyo ya Kiserikali ya Heart Team Africa Foundation (HTAF) Irene Mbonde akiwakabidhi bidhaa zinazouzwa na Taasisi hiyo wadau waliochangia matibabu ya watoto wenye magonjwa ya moyo wanaotibiwa na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakati wa maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam. Na: JKCI ******************************************************************************************************** Wananchi wamehimizwa kujitokeza kuchangia gharama za matibabu ya watoto wenye magonjwa ya moyo wanaotibiwa na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI). Rai hiyo imetolewa leo na mjumbe wa Taasisi isiyo ya kiserikali ya Heart Team Africa Foundation (HTAF) Irene Mbonde wakati wa maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam yanayoendelea katika viwanja vya Mwalimu Nyerere vilivyopo barabara ya Kilwa. Irene alisema Taasisi hiyo ni mara yake ya kwanza kushiriki katika maonesho ya Sabasaba wakiwa na lengo la kuitambulisha taasisi hiyo katika jamii pamoja na ...

JKCI na Appolo Hospital kushirikiana matibabu ya moyo

Image
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akizungumza na madaktari bingwa wa upasuaji wa moyo kutoka Hospitali ya Apollo iliyopo nchini India walipotembelea Taasisi hiyo tawi la Oysterbay jana jijini Dar es Salaam. Daktari bingwa wa upasuaji wa moyo kutoka Hospitali ya Apollo iliyopo nchini India Mrithyunjaya Kalmath akijadiliana na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge alipotembelea Taasisi hiyo tawi la Oysterbay jana jijini Dar es Salaam  Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akimpatia zawadi daktari bingwa wa upasuaji wa moyo kutoka Hospitali ya Appolo iliyopo nchini India Ashwani Singh wakati wataalamu kutoka Hospitali ya Appolo walipotembelea taasisi hiyo jana jijini Dar es Salaam Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akiwa katika picha ya pamoja na madaktari bingwa wa upasuaji wa moyo kutoka Hospitali ya Appolo ili...