JKCI na Appolo Hospital kushirikiana matibabu ya moyo

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akizungumza na madaktari bingwa wa upasuaji wa moyo kutoka Hospitali ya Apollo iliyopo nchini India walipotembelea Taasisi hiyo tawi la Oysterbay jana jijini Dar es Salaam.

Daktari bingwa wa upasuaji wa moyo kutoka Hospitali ya Apollo iliyopo nchini India Mrithyunjaya Kalmath akijadiliana na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge alipotembelea Taasisi hiyo tawi la Oysterbay jana jijini Dar es Salaam 

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akimpatia zawadi daktari bingwa wa upasuaji wa moyo kutoka Hospitali ya Appolo iliyopo nchini India Ashwani Singh wakati wataalamu kutoka Hospitali ya Appolo walipotembelea taasisi hiyo jana jijini Dar es Salaam


Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akiwa katika picha ya pamoja na madaktari bingwa wa upasuaji wa moyo kutoka Hospitali ya Appolo iliyopo nchini India  walipotembelea JKCI kuona maendeleo na uwekezaji uliowekezwa jana jijini Dar es Salaam.

Na: JKCI

******************************************************************************************************

Madaktari bingwa wa upasuaji wa moyo kutoka Hospitali ya Apollo nchini India watembelea Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) tawi la Oysterbay kuangalia uwekezaji uliowekezwa pamoja na maendeleo ya Taasisi hiyo.

Akizungumza na Madaktari hao jana jijini Dar es Salaam Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge alisema mbali na kuangalia uwekezaji wa taasisi hiyo pia wamekubaliana kushirikiana katika masuala ya upasuaji wa moyo na kubadilishana ujuzi.

Dkt. Kisenge alisema ushirikiano huo utawasaidia wataalamu wa JKCI kupata ujuzi na kuweza kufanya upasuaji mkubwa wa moyo kwa kutumia njia ya tundu dogo kuwasaidia wagonjwa kupunguza muda wa kukaa hospitalini.

“Madaktari bingwa kutoka Hospitali ya Apollo iliyopo nchini India wamekuja kujionea maendeleo makubwa yaliyofanya na Taasisi yetu katika tawi letu la Oystebay na kuahidi kushirikiana nasi katika matibabu ya upasuaji wa moyo kwa wagonjwa wetu” alisema Dkt. Kisenge

Dkt. Kisenge alisema sambamba na kubadilisha ujuzi JKCI na Hospitali ya Appolo watakuwa wanabadilishana wataalamu kwa kuwapeleka Appolo na wa Appolo kwenda JKCI kujifunza mambo mbalimbali katika kutoa huduma ya upasuaji wa moyo.

“Kwa kufanya hivyo kutawasaidia wataalamu wetu kukutana na wenzao kubadilishana ujuzi ili wote kwa pamoja tuweze kuokoa maisha ya wagonjwa wetu wa moyo”, alisema Dkt. Kisenge

Kwa upande wake Daktari bingwa wa upasuaji wa moyo kutoka Hospitali ya Appolo iliyopo nchini India Mrithyunjaya Kalmath alisema amefurahi kuona wataalamu wa Hospitali ya Appolo wanaenda kushirikiana na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete kwani wamekuwa wakiisikia Taasisi hiyo kutokana na huduma bobezi za matibabu ya moyo inazozifanya.

“Ushirikiano wetu utaende kurahisisha huduma za upasuaji mkubwa wa moyo kwani tutatoa huduma hizo kwa kutumia njia ya tundu dogo na kuwapunguzia wagonjwa maumivu na muda wa kukaa hospitali”, alisema Dkt. Kalmath

Dkt. Kalmath alisema wanaahidi kufanya kazi ya kuokoa maisha ya wagonjwa wa moyo wanaotibiwa na Taasisi hiyo na kuleta maendeleo katika utoaji wa huduma bingwa bobezi za matibabu ya moyo.


Comments

Popular posts from this blog

Wateja wa CRDB kutibiwa JKCI kwa punguzo la asilimia 50%

Wanawake wa JKCI SACCOS wanaongoza kwa kumiliki hisa

JKCI, MOI NA MNH waitwa Comoro kutoa huduma za matibabu ya kibingwa