Global Fund watembelea JKCI kuangalia mtambo wa Oksijeni

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akizungumza na viongozi kutoka Mfuko wa Dunia wa Kupambana na Ukimwi, Kifua kikuu na Ukoma (Global Fund) walipotembelea Taasisi hiyo jana kwaajili ya kuangalia mtambo wa Oksijeni uliosimikwa katika Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam.

Mhandisi wa vifaa tiba kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya kikwete (JKCI) Eng. Abela Rweguza akiwaelezea viongozi kutoka Mfuko wa Dunia wa Kupambana na Ukimwi, Kifua kikuu na Ukoma (Global Fund) namna ambavyo JKCI imefaidika na mtambo wa Oksijeni uliosimikwa JKCI wakati wa ziara yao jana kuangalia namna unavyofanya kazi.

Msimamizi wa chumba cha uangalizi maalumu cha watoto wenye magonjwa ya moyo (ICU) Mohamed Wamara akiwaelezea namna oksijeni inavyowafikia watoto waliolazwa ICU viongozi kutoka Mfuko wa Dunia wa Kupambana na Ukimwi, Kifua kikuu na Ukoma (Global Fund) walipotembelea Taasisi hiyo jana kuangalia namna mtambo wa Oksijeni uliosimikwa JKCI unavyofanya kazi.

Mhandisi wa vifaa tiba kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete Eng. Veronica Mugendi akiwaonesha baadhi ya mitungi iliyojaa oksijeni viongozi kutoka Mfuko wa Dunia wa Kupambana na Ukimwi, Kifua Kikuu na Ukoma (Global Fund) walipotembelea Taasisi hiyo jana kuangalia namna mtambo wa Oksijeni uliosimikwa JKCI unavyofanya kazi.


Viongozi kutoka Mfuko wa Dunia wa Kupambana na Ukimwi, Kifua Kikuu na Ukoma (Global Fund) wakiangalia mtambo wa oksijeni uliosimikwa katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) walipotembelea Taasisi hiyo jana kuangalia namna mtambo huo unavyofanya kazi.

Picha na: JKCI

*********************************************************************************************************

Comments

Popular posts from this blog

JKCI na AICC Hospitali kutoa huduma za uchunguzi na matibabu ya moyo katika kikao kazi cha wenyeviti na watendaji wakuu wa Taasisi za Umma

JKCI yapata tuzo ya taasisi ambayo imetoa mchango wa kipekee kiuchumi na kijamii katika kuleta matokeo makubwa kwa kipindi cha mwaka 2023/2024

Wafanyakazi waliohama JKCI waagwa