JKCI yatoa huduma za uchunguzi wa afya Bonanza la NBC


 Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Ditram Mgimba akimpima uwiano wa urefu kwa uzito (BMI) mkazi wa Dar es Salaam aliyefika katika viwanja vya Police Office Mess Oysterbay wakati wa bonanza la NBC kuelekea mbio za NBC zitakazofanyika Julai 26 mwaka huu kwaajili ya kuchangia matibabu ya watoto wenye magonjwa ya moyo wanaotibiwa na JKCI


Daktari wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Moris Budotela akimuelezea umuhimu wa kupima afya mkazi wa Dar es Salaam aliyefika katika viwanja vya Police Office Mess Oysterbay wakati wa bonanza la NBC kuelekea mbio za NBC zitakazofanyika Julai 26 mwaka huu kwaajili ya kuchangia matibabu ya watoto wenye magonjwa ya moyo wanaotibiwa na JKCI.

Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Ditram Theodory Mgimba akimpima shinikizo la damu mkazi wa Dar es Salaam aliyefika katika viwanja vya Police Office Mess Oysterbay wakati wa bonanza la NBC kuelekea mbio za NBC zitakazofanyika Julai 26 mwaka huu kwaajili ya kuchangia matibabu ya watoto wenye magonjwa ya moyo wanaotibiwa na JKCI.

Afisa Utafiti wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Makrina Komba akimfanyia usajiri mkazi wa Dar es Salaam aliyefika katika viwanja vya Police Office Mess Oysterbay wakati wa bonanza la NBC kuelekea mbio za NBC zitakazofanyika Julai 26 mwaka huu kwaajili ya kuchangia matibabu ya watoto wenye magonjwa ya moyo wanaotibiwa na JKCI

Daktari wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Sahiya Yahya akimpatia ushauri mara baada ya kufanya uchunguzi wa afya mkazi wa Dar es Salaam aliyefika katika viwanja vya Police Office Mess Oysterbay wakati wa bonanza la NBC kuelekea mbio za NBC zitakazofanyika Julai 26 mwaka huu kwaajili ya kuchangia matibabu ya watoto wenye magonjwa ya moyo wanaotibiwa na JKCI.


Na JKCI

*******************************************************************************************************************************************************************************************************************************************
 Watu zaidi ya 50 wamefanyiwa uchunguzi wa afya kuelekea mbio za NBC zitakazofanyika Julai 26 mwaka huu kwaajili ya kuchangia matibabu ya watoto wenye magonjwa ya moyo wanaotibiwa katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI).
Uchunguzi huo umefanywa na wataalamu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakati wa Bonanza la NBC lililofanyika leo katika viwanja vya Police Office Mess vilivyopo Oysterbay jijini Dar es Salaam.
Watu hao wamefanyiwa uchunguzi wa afya kwa kupimwa shinikizo la damu (BP), kiwango cha sukari kwenye damu, uzito, urefu pamoja na uwiano wa uzito kwa urefu (BMI) kama sehemu ya kutathmini hali zao za kiafya na kupata ushauri kutoka kwa wataalamu wa afya.
Akizungumza wakati wa Bonanza hilo Daktari wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Moris Budotela alisema kati ya watu waliofika kwaajili ya kufanyiwa uchunguzi wa afya, watu wanne walibainika kuwa na changamoto za kiafya zilizohitaji ufuatiliaji zaidi hivyo kupewa rufaa ya kufika katika Taasisi hiyo kwaajili ya uchunguzi zaidi.
Aidha Dkt. Moris alisema tatizo kubwa ambalo limekuwa likibainika mara kwa mara wataalamu wanapoweka kambi za uchunguzi wa afya ni tatizo shinikizo la damu hivyo kuiomba jamii kuendelea kufanya uchunguzi wa afya wa mapema na kuchukua hatua.
Kwa upande wake Juma Kisuma mkazi wa Ilala jijini Dar es Salaam aliyeshiriki bonanza hilo alisema kuchunguza kwake afya kumemsaidia kujitambua na kuona umuhimu wa kufanya uchunguzi wa afya mara kwa mara.
“Tunaishukuru JKCI kwa kufanya zoezi la kutupima afya katika bonanza hili kwani huduma hizi ni muhimu kwetu sote ,” alisema Kisuma

Comments

Popular posts from this blog

Kutoka miaka 22 hadi kustaafu: Safari ya Lemmah yatoa somo kwa Watumishi wa Umma

Wanawake waaswa kulinda mioyo yao, kuepuka sukari na chumvi kupita kiasi