Upimaji wa magonjwa ya moyo kwa wanawake, wajawazito na watoto mkoani Arusha
*******************************************************************************************************************************************************************************************************
Katika kuadhimisha siku ya Kimataifa ya
Wanawake tarehe 08/03/2025 Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha tutatoa huduma za tiba mkoba zijulikanazo kwa
jina la Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Outreach Services kwa kufanya upimaji wa
magonjwa ya moyo kwa wanawake, wajawazito na watoto.
Watakaogundulika kuwa na matatizo ya moyo watafanyiwa uchunguzi zaidi na kupatiwa matibabu hapo hapo na wale watakaokutwa na matatizo yatakayohitaji matibabu ya kibingwa watapewa rufaa ya kuja kutibiwa katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) iliyopo Upanga jijini Dar es Salaam.
Tunawaomba wanawake, wajawazito, wazazi na walezi wenye watoto wajitokeze kwa wingi kupima afya zao kujua kama wana matatizo ya moyo ili kuanza matibabu mapema kwa watakaogundulika kuwa wagonjwa.
Kwa taarifa zaidi
wasiliana kwa simu namba 0754849850 na 0752211081.
“Afya ya Moyo Wako ni Jukumu
Letu”.
Comments
Post a Comment