Mbeya kufikiwa na kambi maalumu ya uchunguzi na matibabu ya kibingwa ya moyo


Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group Marcia Tillya akimpima mkazi wa Dar es Salaam kipimo cha kuangalia jinsi moyo unavyofanya kazi wakati wa kambi maalumu ya siku mbili ya upimaji na matibabu ya moyo ikiwa ni maadhimisho ya siku ya moyo duniani iliyofanyika katika kliniki ya JKCI  Kawe.

*********************************************************************************************************************************************************************************************************************************************************

UPIMAJI NA MATIBABU YA MOYO MKOANI MBEYA

Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) na Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya (MZRH) tutatoa huduma za tiba mkoba zijulikanazo kwa jina la Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Outreach Services kwa kufanya upimaji na matibabu ya magonjwa ya moyo kwa washiriki wa mkutano wa 109 wa Wadau wa Elimu kwa Umma na wananchi wa mkoa wa Mbeya.

 

Upimaji huu utafanyika bila malipo yoyote kwa watoto na watu wazima tarehe 17 - 21/02/2025 saa 2:00 asubuhi hadi saa 10:00 jioni katika viwanja vya City Park  Garden mkabala na uwanja wa mpira wa miguu Sokoine jijini Mbeya.

 

Kutakuwa na wataalamu wa lishe watakaotoa elimu ya lishe bora itakayowapa wananchi uelewa wa  kufuata mtindo bora wa maisha utakaowasaidia kuepukana na magonjwa ya moyo ambayo ni moja ya magonjwa yasiyoambukiza na yanaweza kuepukika kwa kufuata ushauri wa kitaalamu.

Watakaogundulika kuwa na matatizo ya moyo watafanyiwa uchunguzi zaidi na kupatiwa matibabu hapo hapo na wale watakaokuwa na matatizo yatakayohitaji matibabu ya kibingwa watapewa rufaa ya kuja kutibiwa katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) iliyopo Upanga jijini Dar es Salaam.

Tunawaomba wananchi mjitokeze kwa wingi kupima afya zenu kujua kama mna matatizo ya moyo ili kuanza matibabu mapema kwa atakayegundulika kuwa mgonjwa.

Kwa taarifa zaidi wasiliana kwa simu namba 0785460858 na 0735215430.

“Afya ya Moyo Wako ni Jukumu Letu”.


Comments

Popular posts from this blog

JKCI na AICC Hospitali kutoa huduma za uchunguzi na matibabu ya moyo katika kikao kazi cha wenyeviti na watendaji wakuu wa Taasisi za Umma

JKCI yapata tuzo ya taasisi ambayo imetoa mchango wa kipekee kiuchumi na kijamii katika kuleta matokeo makubwa kwa kipindi cha mwaka 2023/2024

Wafanyakazi waliohama JKCI waagwa