Wagonjwa wenye matatizo ya mishipa ya damu ya miguu kutanuka kutibiwa JKCI
*****************************************************************************************************************************************************************************************************************************
TAARIFA KWA WATAALAMU WA AFYA NCHINI
KAMBI
MAALUMU YA MATIBABU YA MAGONJWA YA MISHIPA YA DAMU YA MIGUU KUTANUKA (VARICOSE
VEIN)
Taasisi ya Moyo Jakaya
Kikwete (JKCI) inawaomba wataalamu wa afya nchini kutoka Hospitali za Wilaya, Mikoa na Rufaa kuwatuma
wagonjwa wenye matatizo ya mishipa ya damu kutanuka kwenye miguu kwa jina la
kitaalamu Varicose Vein waje kutibiwa katika kambi maalumu ya uchunguzi na
matibabu ya kutanuka kwa mishipa hiyo.
Matibabu hayo
yatakayotolewa tarehe 12 hadi 15 Februari 2025 yatafanywa na wataalamu wa JKCI kwa kushirikiana na wenzao
kutoka Hospitali ya Andalusia ya nchini
Misri.
Matibabu yatakayofanyika
katika kambi hiyo ni ya upasuaji kwa njia ya kutumia matundu madogo katika
kutibu mishipa ya damu ya vein iliyotanuka kwa kutumia kifaa cha umeme
kijulikanacho kwa jina la laser ablation machine.
Aidha tunawaomba wagonjwa
wenye matatizo ya vidonda vya miguu visivyopona kwa muda mrefu, matatizo ya
mishipa ya damu miguuni kutanuka, ganzi ya miguu na mabadiliko ya rangi
miguunii wafike katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Upanga kwaajili ya
kufanyiwa uchunguzi na kupata matibabu.
Kwa taarifa zaidi
wasiliana kwa simu namba 0716-696217 Dkt. Alex Joseph, 0716162295 Dkt. Alex
Msoka na 0788-308999 Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete .
“Afya ya Moyo
Wako ni Jukumu Letu”.
Comments
Post a Comment