Mhe. Makonda awahimiza wananchi wa Arusha kupima afya ya moyo
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Paul Makonda akiangalia daftari maalumu la usajiri wa wagonjwa alipotembelea banda la Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakati wa kambi maalumu ya kupima na kutibu magonjwa ya binadamu inayofanyika katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid uliopo jijini Arusha. Wapili kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa JKCI Dkt. Peter Kisenge
Afisa Uuguzi wa Hospitali
ya Arusha Lutheran Medical Centre (ALMC) ambayo inasimamiwa na Taasisi ya Moyo
Jakaya Kikwete (JKCI) Nadia Zuberi akimuonesha majibu ya sukari kwenye damu
mwananchi aliyefika kufanya uchunguzi wa afya katika banda la JKCI wakati wa
kambi maalumu ya kupima na kutibu magonjwa ya binadamu inayofanyika katika
uwanja wa Sheikh Amri Abeid uliopo jijini Arusha.
Afisa Uuguzi wa Taasisi
ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hania Bwahama akimpima shinikizo la damu (BP)
mwananchi aliyefika kufanya uchunguzi wa afya katika banda la Taasisi hiyo wakati
wa kambi maalumu ya kupima na kutibu magonjwa ya binadamu inayofanyika katika
uwanja wa Sheikh Amri Abeid uliopo jijini Arusha.
Daktari wa Hospitali ya
Arusha Lutheran Medical Centre (ALMC) ambayo inasimamiwa na Taasisi ya Moyo
Jakaya Kikwete (JKCI) Ibrahim Gulamhessein akimpatia maelekezo mwananchi
aliyefika kufanya uchunguzi wa afya katika banda la JKCI wakati wa kambi
maalumu ya kupima na kutibu magonjwa ya binadamu inayofanyika katika uwanja wa
Sheikh Amri Abeid uliopo jijini Arusha.
Na JKCI
*******************************************************************************************************
Wananchi wa Mkoa wa
Arusha na Mikoa ya jirani wametakiwa kujitokeza kupima moyo katika banda la
Taasisi ya Moyo Jakaya kikwete (JKCI) linalotoa huduma bingwa bobezi za
uchunguzi wa magonjwa ya moyo kwa kutumia teknolojia za kisasa.
Rai hiyo imetolewa leo
na Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini Mhe. Paul Makonda wakati wa kambi maalumu ya
kupima na kutibu magonjwa ya binadamu inayofanyika katika uwanja wa Sheikh Amri
Abeid uliopo jijini Arusha.
Mhe. Makonda alisema
JKCI ni Taasisi bora katika kutoa huduma bingwa bobezi za moyo Africa Mashariki
na Kati hivyo wananchi watumie uwepo wa Taasisi hiyo kufanyiwa uchunguzi wa
afya na kupata taarifa sahihi kuhusu afya zao.
“Msiposhiriki katika
kambi hii kupata huduma bingwa za uchunguzi na matibabu ya moyo hapo baadaye
mkikutwa na magonjwa haya mnaweza kutumia mtaji wenu wote kwaajili ya kupata
matibabu, ni muhimu sasa mkapima”, alisema Mhe. Makonda
Mhe. Makonda alisema
JKCI wamefungua tawi lake mkoani Arusha kwaajili ya watu wa kanda ya Kaskazini
hivyo wale wote watakaogundulika kuwa na matatizo ya moyo kupitia kambi hiyo
watatibiwa katika Hospitali ya Arusha Lutheran Medical Centre ambalo ni Tawi la
JKCI.
Kwa upande wake
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Peter Kisenge
alisema JKCI imejipanga kuwahudumia watu wote wanaohitaji huduma za uchunguzi
na matibabu ya magonjwa ya moyo hivyo wasisite kufika katika banda hilo
kwaajili ya matibabu.
Dkt. Kisenge alisema
kupitia kambi hiyo wataalamu mabingwa wabobezi wa magonjwa ya moyo kwa watoto
na watu wazima wameshiriki kwa kutoa huduma lakini pia kutoa elimu ya namna ya
kujikinga na magonjwa yasiyoambukiza yakiwemo magonjwa ya moyo.
“Tupo hapa madaktari wa
kutosha kutoka JKCI makao makuu na JKCI Arusha Lutheran Medical Centre (ALMC),
lengo letu ni kuhakikisha kuwa huduma za matibabu ya moyo zinawafikia wananchi
wote”, alisema Dkt. Kisenge.
Aidha Dkt. Kisenge
alisema JKCI tawi la Arusha Lutheran Medical Centre (ALMC) inaenda kuzindua
huduma ya kuwafuata wagonjwa majumbani kwa kuwawekea kifaa maalumu
kinachojulikana kwa jina la DOZEE ambacho kinawekwa chini ya godoro la mgonjwa
akiwa nyumbani na kuweza kusoma shinikizo la damu, kiwango cha hewa mwilini,
mapigo ya moyo na umeme wa moyo.





Comments
Post a Comment