Posts

Showing posts from May, 2024

Tanzania ya kwanza Afrika kutumia Mashine ya kufuatilia wagonjwa nyumbani

Image
  Mkuu wa Mkoa wa  Dar es Salaam Mhe. Albert Chalamila  mashine ya Dozee iliyotengenezwa na Sakaar Health Tech LTD ambayo inatumika kuwafuatilia wagonjwa  wa moyo wakiwa nyumbani ili kujua hali zao na kutoa msaada wa haraka endapo utahitajika. *********************************************************************************************************************************************************************************** Kwa mara ya kwanza barani Afrika Taasisi ya moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na Sakaar Health Tech LTD wamezindua rasmi mashine  maalum  itakayotumika  kufuatilia wagonjwa  wa moyo wakiwa nyumbani ili kujua hali zao na kutoa msaada wa haraka endapo utahitajika. Kufuatia uzindunzi wa mashine hiyo iitwayo Dozee Tanzania sasa imekuwa nchi ya tatu Duniani kutoa huduma hivyo huku ikiwa nchi ya kwanza barani Afrika.   Akizungumza wakati wa uzinduzi huo jana jijini Dar es Salaam,mkuu wa mkoa huo Mhe. Albert Chalamila ...

Maabara ya JKCI yapata ithibati ya kimataifa (ISO 15189:2012)

Image
 Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge  akizunguma na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam kuhusu maabara ya Taasisi hiyo kupata  ithibati ya viwango vya ubora wa kimataifa (ISO 15189:2012) katika kutoa huduma za vipimo vya magonjwa ya moyo pamoja na magonjwa mengine.Kulia ni Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano wa JKCI Anna Nkinda. Kaimu Mkuu wa Maabara ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Emmanuel Mgao akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam kuhusu maabara hiyo kukidhi vigezo vilivyowekwa kimataifa katika kutoa huduma na kupata  ithibati yenye namba ISO 15189:2012 . Wafanyakazi wa Maabara ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi hiyo Dkt. Peter Kisenge  wakati akizunguma na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam kuhusu maabara hiyo kupata  ithibati ya viwango vya ubora wa kimataifa (ISO 15189:2012) katika kutoa hudu...

Wahandisi wafanyiwa vipimo vya viashiria magonjwa ya moyo

Image
Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Faizat Ndosa akimpima sukari kwenye damu mhandisi aliyetembelea banda la JKCI wakati wa mkutano wa 30 wa wahandisi washauri Afrika (FIDIC Africa) unaofanyika katika ukumbi wa kimataifa wa Mwalimu Nyerere International Convention Center (JNICC) uliopo jijini Dar es Salaam. Mtaalamu wa huduma za afya za mtandao kutoka kampuni ya Cloudscript inayofanya kazi na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Beatrice Mmari akiwafundisha wahandisi namna ya kutumia huduma ya afya mtandao kupitia mfumo wa Cloudscript walipotembelea banda la JKCI wakati wa mkutano wa 30 wa wahandisi washauri Afrika (FIDIC Africa) unaofanyika katika ukumbi wa kimataifa wa Mwalimu Nyerere International Convention Center (JNICC) uliopo jijini Dar es Salaam. Na: JKCI ********************************************************************************************* Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) inatoa huduma za uchunguzi wa magonjwa ya moyo na ushauri wa lishe bora kwa...

Watu 602 wafikiwa na huduma ya tiba mkoba ya moyo mkoani Rukwa

Image
Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Beatrice Daniel akimpima sukari kwenye damu mwananchi aliyefika katika Hospitali ya  Rufaa ya Mkoa wa Rukwa wakati wa kambi maalumu ya uchunguzi na matibabu ya moyo iliyofanywa na wataalamu wa JKCI kwa kushirikiana na wenzao wa hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Rukwa. Na: JKCI ******************************************************************************************* Watu 602 wakiwemo watu wazima 577 na watoto 25 wamepata huduma za uchunguzi na matibabu ya kibingwa ya magonjwa ya moyo katika kambi maalumu ya matibabu iliyomalizika hivi karibuni mkoani Rukwa. Huduma hiyo ya matibabu ya tiba mkoba ijulikanayo kwa jina la Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Outreach Services ilitolewa kwa siku tano na wataalamu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na wenzao wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Sumbawanga Akizungumza wakati wa kuhitimisha kambi hiyo Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) ...

Wauguzi wapigwa msasa wa jinsi ya kuwahudumia wagonjwa wa dharura na mahututi

Image
Mkufunzi wa mafunzo ya jinsi ya kuwahudumia wagonjwa wa dharura na mahututi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Afisa Muuguzi Kiasha Mclnnis akiwafundisha wauguzi wa taasisi hiyo jinsi ya kuwahudumia wagonjwa hao. Afisa Muuguzi wa Chumba cha Wagonjwa wanaohitaji Uangalizi Maalumu (ICU) wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Lucy Kabeya akiwafundisha wauguzi wa Taasisi hiyo namna ya kuwahudumia wagonjwa wa dharura na mahututi. Maafisa Uuuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakifuatilia mafunzo ya jinsi ya kuwahudumia wagonjwa wa dharura na mahututi yaliyofanyika hivi karibuni katika Taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam.

Wapelekeni watoto kupata matibabu ya kibingwa

Image
Daktari bingwa wa magojwa ya moyo kwa watoto wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Theophil Ludovic akimpima mtoto kipimo cha kuangalia jinsi moyo unavyofanya kazi (Echocardiography -ECHO) wakati wa kambi maalumu ya siku tano ijulikanayo kwa jina la Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Outreach inayofanyika katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Saumbawanga. Na: JKCI ************************************************************************************************************* Wananchi wametakiwa kuwapeleka watoto kupata matibabu ya kibingwa pale zinapotokea kambi mbalimbali za matibabu ya moyo ili nao waweze kupata matibabu hayo. Rai hiyo imetolewa jana na kaimu Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Asha Izina alipotembelea huduma ya tiba mkoba ijulikanayo kwa jina la Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Outreach Services inayofanyika katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Sumbawanga. Asha ambaye pia ni mratibu wa huduma za afya ya uzazi na mtoto mkoani Rukwa ali...

Wauguzi wafundishwa jinsi ya kuwahudumia wagonjwa wa dharura na mahututi

Image
Daktari bingwa wa wagonjwa wa dharura na mahututi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Vivian Mlawi akiwafundishwa namna ya kumhudumia mgonjwa anayehitaji uangalizi maalumu wauguzi wanaochukua mafunzo ya kuwahudumia wagonjwa hao yanayotolewa na taasisi hiyo kwakushirikiana na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM). Wauguzi kutoka nchini Zambia na mmoja kutoka nchini Tanzania wanaochukua mafunzo ya kuwahudumia wagonjwa wa dharura na mahututi yanayotolewa na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) wakiwa katika mazoezi ya kutumia mashine ya kumsaidia mgonjwa kupumua (Ventilator). Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Mary Haule akiwafundisha wauguzi wanaochukua mafunzo ya kuwahudumia wagonjwa wa dharura na mahututi yanayotolewa na JKCI kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) kumhudumia mtoto aliyelazwa katika chumba cha uangalizi maalumu wakati wa mafunzo kwa vitendo. Wauguzi wanaochukua mafunzo ya kuw...

JKCI SACCOS mkombozi wa maisha ya wafanyakazi

Image
Mwenyekiti wa Chama cha kuweka akiba na mikopo (Saccos) cha Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Tulizo Shemu akiwashukuru wanachama wa Saccos hiyo kwa kumuamini na kumchangua tena kuwa mwenyekiti wakati wa mkutano mkuu wa mwaka wa kuchagua viongozi wapya na kuangalia maendeleo ya chama hicho uliofanyika jana jijini Dar es Salaam. Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akizungumza na wanachama wa Chama cha kuweka akiba na mikopo (Saccos) cha Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakati wa mkutano mkuu wa mwaka wa kuchagua viongozi wapya na kuangalia maendeleo ya chama hicho uliofanyika jana jijini Dar es Salaam. Wanachama wa chama cha kuweka akiba na mikopo (Saccos) cha Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakifuatilia mada zilizokuwa zikitolewa wakati wa mkutano mkuu wa mwaka wa kuchagua viongozi wapya na kuangalia maendeleo ya chama hicho uliofanyika jana jijini Dar es Salaam. Na: JKCI ***************************************************...

Burundi kuendelea kuwatuma wagonjwa wa moyo kutibiwa JKCI

Image
Daktari bingwa wa moyo Constantin Nyamuzangula na Daktari bingwa wa sukari Ndikumana Sudi kutoka nchini Burundi wakiangalia huduma zinazotolewa katika chumba cha uangalizi maalumu (ICU) cha Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) walipotembelea taasisi hiyo leo kwaajili ya kuangalia huduma zinazotolewa. Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Agnes Lugendo akiwaelezea huduma zinazotolewa katika wodi ya wagonjwa waliofanyiwa upasuaji wa moyo Daktari bingwa wa moyo Constantin Nyamuzangula na Daktari bingwa wa sukari Ndikumana Sudi kutoka nchini Burundi walipotembelea JKCI leo kwaajili ya kuangalia huduma zinazotolewa na Taasisi hiyo. Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) anayefanya kazi chumba cha uangalizi maalumu cha watoto (ICU) Jackline Siane akiwaelezea namna wanavyowahudumia watoto Daktari bingwa wa moyo Constantin Nyamuzangula na Daktari bingwa wa sukari Ndikumana Sudi kutoka nchini Burundi walipotembelea Taasisi hiyo leo kwaajili ya kuangalia huduma zi...

Watu 310 wapima moyo siku ya shinikizo la juu la damu duniani

Image
Afisa Lishe wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Husna Faraji akimuelimisha mwananchi kuhusu lishe bora wakati wa Kambi maalumu ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Outreach Services iliyofanyika kwa siku mbili katika Hospitali ya JKCI Dar Group kuadhimisha siku ya Shinikizo la juu la damu duniani inayoadhimishwa kila ifikapo tarehe 17 Mei. Mkurugenzi wa tiba wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Tatizo Waane akizungumza na wananchi waliofika katika Hospitali ya JKCI Dar Group wakati wa Kambi maalumu ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Outreach Services iliyofanyika kwa siku mbili katika kuadhimisha siku ya Shinikizo la juu la damu duniani inayoadhimishwa kila ifikapo tarehe 17 Mei. Mteknolojia maabara wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete Hospitali ya JKCI Dar Group Emmanuel Mapula akiwagawia vipeperushi vinavyoelezea ugonjwa wa shinikizo la damu wananchi waliojitokeza wakati wa Kambi maalumu ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Outreach Services iliyofanyika kwa siku mbili katika kuadhi...

Wakazi wa Dar es Salaam wapima moyo bure

Image
Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete Hospitali ya JKCI Dar Group Patrice Justine akimpima shinikizo la damu mwananchi aliyejitokeza kupima wakati wa kambi maalumu ya Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan Outreach Services inayofanyika katika Hospitali hiyo katika kuadhimisha siku ya shinikizo la damu duniani inayoadhimishwa kila ifikapo tarehe 17 Mei. Daktari wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete Hospitali ya JKCI Dar Group Masanja James akizungumza na mwananchi aliyefika katika kambi maalumu ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Outreach Services inayofanyika katika Hospitali hiyo katika kuadhimisha siku ya shinikizo la damu duniani inayoadhimishwa kila ifikapo tarehe 17 Mei. Mwakilishi kutoka kamupuni ya dawa za binadamu ya Sun Pharma Oresta Mwila akimhudumia mwananchi aliyepatiwa matibabu katika kambi maalumu ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Outreach Services inayofanyika katika Hospitali ya JKCI Dar Group katika kuadhimisha siku ya shinikizo la damu duniani inayoadhimishwa kila ifikapo tar...

Asilimia 60 ya wagonjwa wa presha hawajitambui

Image
Kaimu Mkuu wa Hospitali ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dar Group Dkt. Tulizo Shemu akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam kuhusu upimaji utakaofanyika tarehe 16 na 17 Mei 2024 katika Hospitali hiyo ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha siku ya shinikizo la damu duniani inayoadhimishwa kila ifikapo tarehe 17 mwezi Mei. Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo kwa watoto wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Sulende Kubhoja akielezea kuhusu tatizo la shinikizo la juu la damu kwa watoto wakati wa mkutano na waandishi wa habari kuhusu siku ya shinikizo la damu inayoadhimishwa kila ifikapo tarehe 17 mwezi Mei. JKCI itaadhimisha siku hiyo kwa kufanya upimaji bila gharama kwa wananchi wa Dar es Salaam siku ya tarehe 16 na 17 Mei 2024. Na: JKCI ************************************************************************************************* Zaidi ya asilimia 60 ya watu wenye shinikizo la juu la damu hapa nchini hawajitambui kama wana tatizo hilo kwani tafiti zinaonesha k...

Serikali kufungua tawi la JKCI – Chato

Image
  Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu akiingia bungeni leo jijini Dodoma kwaajili ya kuwasilisha hotuba ya makadirio ya bajeti ya wizara hiyo kwa mwaka wa fedha wa 2024/25. Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu na Naibu Waziri wa Afya Mhe. Dkt. Godwin Mollel wakiwa wameshika  hotuba ya makadirio ya bajeti ya wizara hiyo kwa mwaka wa fedha wa 2024/25 kabla haijasoma leo bungeni jijini Dodoma. ************************************************************************************************************************************************************************************** Serikali imepanga kufungua tawi la Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) Kanda ya Ziwa katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda Chato (JKCI- Chato) iliyopo mkoani Geita. Hayo yamesemwa leo bungeni jijini Dodoma na Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu wakati akiwasilisha hotuba ya makadirio ya bajeti ya wizara hiyo kwa mwaka wa fedha wa 2024/25. Katika kutekeleza hilo Wizara ya Afya moja ya vipaumbele vyake kwa mwaka wa f...