JKCI yaihamasisha jamii kupata chanjo ya homa ya ini
Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Florah Kasembe akitoa elimu kuhusu namna ya kujikinga na magonjwa ya moyo kwa wananchi waliotembelea banda la Taasisi hiyo wakati wa Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (SABASABA). Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Agnes Kajangwa akimpima wingi wa sukari kwenye damu mwananchi aliyetembelea banda la Taasisi hiyo wakati wa maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (SABASABA) yanayoendelea katika viwanja vya Mwalimu Nyerere vilivyopo barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam. Mhasibu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) DianaRose Kaugila akizungumza na mwananchi aliyefika katika banda la Taasisi hiyo kwaajili ya kufanya uchunguzi wa magonjwa ya moyo wakati wa maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (SABASABA) yanayoendelea katika viwanja vya Mwalimu Nyerere vilivyopo barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam. Mtunza kumbukumbu za Afya ambaye pia ni mjumbe wa kamati ...