Posts

Showing posts from 2025

Banda la JKCI lawavutia wananchi kupima moyo

Image
Naibu katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na wenye Ulemavu Zuhura Yunus akiwa katika picha ya Pamoja na wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) alipotembelea banda la JKCI kwaajili ya kuangalia huduma wanazozitoa katika  maonesho ya Kimataifa ya Wiki ya Usalama na Afya Mahali Pa kazi yanayofanyika katika viwanja vya Mandewa mkoani Singida. Afisa Muuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group Fatma Joseph akimpima shinikizo la damu (BP) mkazi wa Singida aliyefika katika viwanja vya maonesho Mandewa kwaajili ya kupata huduma za uchunguzi na matibabu ya moyo zinazotolewa bila malipo katika Maonesho ya Kimataifa ya Wiki ya Usalama na Afya Mahali Pa Kazi. Mkurugenzi wa Usalama na Afya kutoka Wakala wa Usalama na Afya Mahala pa Kazi (OSHA) Dkt. Jerome Materu akisaini kitabu cha wageni alipotembelea banda la Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakati wa maonesho ya Kimataifa ya Wiki ya Usalama na Afya Mahali Pa kazi yanayofanyika k...

Singida wafurahia huduma za matibabu ya moyo

Image
Afisa Muuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group Fatma Joseph akimpima kiwango cha sukari kwenye damu mkazi wa Singida aliyefika katika banda la JKCI kwaajili ya kupata huduma za uchunguzi na matibabu ya moyo zinazotolewa bila malipo katika Maonesho ya Kimataifa ya Wiki ya Usalama na Afya Mahali Pa kazi yanayofanyika katika viwanja vya maonesho Mandewa mkoani Singida Fundi sanifu wa moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group Devotha Bertram akimpima kipimo cha kuangalia jinsi mfumo wa umeme wa moyo unavyofanya kazi (Electrocardiography – ECG) mkazi wa Singida aliyefika katika Maonesho ya Kimataifa ya Wiki ya Usalama na Afya Mahali Pa Kazi yanayofanyika katika viwanja vya maonesho Mandewa mkoani Singida. Na: Jeremiah Ombelo ************************************************************************************************************* Wananchi wa Mkoa wa Singida wamepongeza huduma zinazotolewa na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) k...

Singida wafikiwa na huduma za kibingwa za matibabu ya moyo

Image
Daktari bingwa wa magonjwa yatokanayo na kazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group Elias  Birago akitoa ushauri wa afya ya moyo  kwa Nelson Mnyanyi aliyetembelea banda la taasisi hiyo wakati wa Maonesho ya Kimataifa ya Wiki ya Usalama na Afya Mahali Pa Kazi yanayofanyika katika viwanja vya maonesho  Mandewa, mkoani Singida. Afisa Utafiti wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Makrina Komba akimpima urefu na uzito mkazi wa Singida aliyefika katika Maonesho ya Kimataifa ya Wiki ya Usalama na Afya Mahali Pa Kazi yanayofanyika katika viwanja vya maonesho   Mandewa mkoani Singida. Na: Jeremiah Ombelo ************************************************************************************************************ Katika jitihada za kuboresha huduma za afya nchini, Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kutoa huduma za uchunguzi na elimu kwa wananchi kuhusu njia bora za kujikinga na magonjwa ya moyo kupitia maonesho ya Kimataifa ya Wiki ya Usamala na ...

CardioTan2025

Image

Uwekezaji sekta ya afya wawezesha utalii tiba nchini

Image
Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt. Seif Shekalaghe akizungumza na wataalamu wa afya walioshiriki kambi maalumu ya matibabu iliyofanyika nchini Comoro mwaka 2024 wakati wa kupokea ripoti ya kambi hiyo leo jijini Dar es Salaam. Kambi hiyo ilifanywa na wataalamu kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI), Hospitali ya Mifupa Muhimbili (MOI), Taasisi ya Saratani Ocean Road (ORCI), na Hospitali ya Benjamin Mkapa (BMH). Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt. Seif Shekalaghe akipokea ripoti ya kambi maalumu ya matibabu iliyofanyika nchini Comoro mwaka 2024 kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakati wa hafla fupi ya kupitia na kupokea ripoti hiyo iliyofanyika leo jijini Dar es Salaam. Kambi hiyo ilifanywa na wataalamu kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Taasisiya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI), Hospitali ya Mifupa Muhimbili (MOI), Taasisi ya Saratani Ocean Road (ORCI), na Hospitali ya Benjamin Mkapa (BMH) Mkurugenzi Mtendaji wa...

Wataalamu wa afya wapata mafunzo ya kuwasaidia wagonjwa wa shambulio la moyo

Image
Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo kutoka Global Fips Hospital iliyopo nchini Marekani Parag Patel akiwafundisha wataalamu wa afya kutoka hospitali mbalimbali nchini namna ya kutambua na kumsaidia mgonjwa aliyepata shambulio la moyo wakati wa mafunzo ya siku moja yaliyofanyika katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) leo jijini Dar es Salaam. Wataalamu wa magonjwa ya moyo kutoka Hospitali 46 nchini wakisikiliza wakati wa mafunzo ya siku moja ya namna ya kutambua na kumsaidia mgonjwa aliyepata shambulio la moyo yaliyokuwa yakitolewa na Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo kutoka Global Fips Hospital iliyopo nchini Marekani Parag Patel leo katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) iliyopo jijini Dar es Salaam. Picha na: JKCI ****************************************************************************************************  

Waandishi wa Habari watakiwa kutumia kalamu zao kuelimisha jamii magonjwa ya moyo

Image
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akimkabidhi Waziri wa Afya Zanzibar Mhe. Nassor Ahmed Mazrui tuzo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kumpongeza kwa kuwa kiongozi mwenye maono ya kuleta mabadiliko katika matibabu ya magonjwa ya moyo Afrika. Tuzo hiyo imetolewa jana wakati wa kufunga mkutano wa siku tatu wa kimataifa wa magonjwa ya moyo uliofanyika Sea Clif & Spa Zanzibar Waziri wa Afya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe. Dkt. Nassor Ahmed Mazrui akifundishwa jinsi ya kutoa huduma ya kuokoa maisha wakati wa kufunga mkutano wa tatu wa kimataifa wa magonjwa ya moyo ulioandaliwa na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na kumalizika jana katika Hoteli ya Sea Clif & Spa Zanzibar. Waziri wa Afya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe. Dkt. Nassor Ahmed Mazrui akizungumza na Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo kutoka Shirika la Madaktari Afrika lililopo nchini Marekani Mazen Albaghdadi wakati wa kufunga...

Waingizaji na wasambazaji wa vifaa tiba wakutana mkutano wa kimataifa wa magonjwa ya moyo

Image
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akizungumza na wataalamu kutoka kampuni ya uingizaji na usambazaji wa vifaa tiba Kas Medics Limited alipotembelea banda la maonesho la kampuni hiyo wakati wa mkutano wa tatu wa kimataifa wa magonjwa ya moyo unaofanyika Zanzibar. Washiriki wa mkutano wa tatu wa kimataifa wa magonjwa ya moyo wakipata elimu kuhusu matumizi ya vifaa tiba katika banda la maonesho la Bohari Kuu ya Dawa wakati wa mkutano huo unaondelea Zanzibar.  Mwakilishi kutoka Kampuni ya Snibe Diagnostic Flora M. Kawa akiwaelezea wataalamu wa famasia kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) huduma zinazotolewa na kampuni hiyo wakati wa mkutano wa tatu wa kimataifa wa magonjwa ya moyo unaofanyika Zanzibar. Washiriki wa mkutano wa tatu wa kimataifa wa magonjwa ya moyo wakipata elimu katika banda la maonesho la kampuni ya Bariki Pharmacy wakati wa mkutano wa tatu wa kimataifa wa magonjwa ya moyo unaofanyika Zanzibar. Mkurugenzi Mtendaji w...

Wataalamu kutoka nchi 25 washiriki mkutano wa magonjwa ya moyo nchini

Image
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akifanya kikao na viongozi kutoka Hospitali za moyo za nchini Zambia, Rwanda, Uganda pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Save a Child’s Heart la nchini Israel Simon Fisher wakati wa mkutano wa tatu wa kimataifa wa magonjwa ya moyo unaofanyika katika hoteli ya Sea Clif iliyopo mjini Zanzibar Meneja wa kampuni ya usambazaji dawa za binadamu ya Sun Pharma Tanzania Abhishek Gahlot akimuelezea bidhaa zinazopatika katika kampuni hiyo Mkurugenzi wa Hospitali ya Taifa ya Moyo ya nchini Zambia Chabwela Shumba alipotembelea banda la kampuni hiyo wakati wa mkutano wa tatu wa kimataifa wa magonjwa ya moyo unaofanyika katika hoteli ya Sea Clif iliyopo mjini Zanzibar Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo kutoka Global Fips Hospital iliyopo nchini Marekani Parag Patel  akiwafundisha wataalamu wa magonjwa ya moyo kutoka nchi mbalimbali namna ya kugundua magonjwa mbalimbali ya moyo wakati wa mkutano wa tatu wa kima...

Watu milioni 4.9 nchini husumbuliwa na magonjwa ya moyo

Image
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akimuelezea Makamu wa pili wa Rais Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla namna wanavyofanya upasuaji wa kubadilisha valvu ya moyo bila kufungua kifua wakati wa ufunguzi wa mkutano wa tatu wa kimataifa wa magonjwa ya moyo uliofanyika jana mjini Zanzibar. Afisa masoko kutoka kampuni ya Snibe Diagnostic Vonnie Feng akimuelezea Makamu wa pili wa Rais Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla huduma zinazotolewa na kampuni hiyo wakati wa ufunguzi wa mkutano wa tatu wa kimataifa wa magonjwa ya moyo uliofanyika jana mjini Zanzibar.   Kaimu Mtendaji Mkuu wa shirika lisilo la kiserikali Heart Team Africa Foundation (HTAF) Linda Gideon akimuonesha mmoja wa washiriki wa mkutano wa tatu wa kimataifa wa magonjwa ya moyo bidhaa zinazouzwa na shirika hilo kwaajili ya kukusanya fedha za matibabu ya watoto wenye magonjwa ya moyo wanaotibwa katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI...

JKCI yapata tuzo utoaji huduma bora za Afya 2025 ngazi ya hospitali maalum na Taifa

Image
Waziri wa Afya Mhe. Jenista Mhagama akimkabidhi tuzo ya mshindi wa utoaji wa huduma bora za Afya mwaka 2025 kundi la Hospitali maalumu na Taifa Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge wakati wa maadhimisho ya wiki ya Afya Kitaifa iliyohitimishwa leo jijini Dodoma. Waziri wa Afya Mhe. Jenista Mhagama akizungumza na mtoto Naima Kasiki aliyewahi kufanyiwa upasuaji wa moyo katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) alipotembelea banda la Taasisi hiyo wakati wa maadhimisho ya wiki ya Afya Kitaifa yaliyohitimishwa leo jijini Dodoma Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akimuelezea Waziri wa Afya huduma za utalii tiba zinazofanywa na Taasisi hiyo alipotembelea banda la JKCI wakati wa maadhimisho ya wiki ya Afya Kitaifa yaliyohitimishwa leo jijini Dodoma Wananchi wa mkoa wa Dodoma wakipata elimu kuhusu magonjwa ya moyo kutoka kwa wataalamu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) walipotembelea banda la Taasisi...