Huduma za moyo karibu na wananchi, JKCI Kawe yahudumia zaidi ya wagonjwa 8,000
Mkurugenzi wa Magonjwa ya Moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Tatizo Waane akizungumza na wagonjwa waliofika kupata huduma za matibabu ya moyo JKCI tawi la Kawe lililopo jengo la Mkapa Health Plaza barabara ya Tuari wilaya ya Kinondoni wakati wa hafla fupi ya maadhimisho ya mwaka mmoja tangu kuanzishwa kwa kliniki hiyo.
Mkurugenzi wa Magonjwa ya Moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Tatizo Waane akizungumza na Daktari Bingwa Magonjwa ya Moyo na msimamizi wa JKCI tawi la Kawe Dkt. Johnstone Kayandabila wakati wa hafla fupi ya maadhimisho ya mwaka mmoja tangu kuanzishwa kwa kliniki hiyo iliyopo jengo la Mkapa Health Plaza barabara ya Tuari wilaya ya Kinondoni.
Mkurugenzi wa Magonjwa ya Moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Tatizo Waane akikata keki na baadhi ya wafanyakazi wa Taasisi hiyo ikiwa ni maadhimisho ya mwaka mmoja tangu kuanzishwa kwa JKCI tawi la Kawe lililopo jengo la Mkapa Health Plaza barabara ya Tuari wilaya ya Kinondoni.
************************************************************************************************************************************************************************************
Tawi la Kawe la Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) limepiga hatua kubwa katika utoaji wa huduma za kibingwa kwa kuwahudumia wagonjwa 8,050 ndani ya mwaka mmoja tangu kuanzishwa kwake. Lengo ni kuhakikisha wananchi wanapata huduma karibu na makazi yao huku wakipunguziwa usumbufu na gharama za usafiri kwenda makao makuu ya JKCI Upanga.
Kliniki
hiyo iliyopo ndani ya jengo la Mkapa Health Plaza, Kawe, wilaya ya Kinondoni jijini
Dar es Salaam imechangia kupunguza msongamano katika makao makuu ya JKCI na
kurahisisha upatikanaji wa huduma kwa haraka.
Akizungumza
leo jijini Dar es Salaam wakati wa maadhimisho ya mwaka mmoja ya kliniki hiyo
Mkurugenzi wa Matibabu ya Moyo JKCI, Dkt. Tatizo Waane alisema kliniki ya Kawe inatoa huduma
za uchunguzi na matibabu ya moyo kwa watoto na watu wazima ikiwemo wagonjwa
wenye bima, wasio na bima na wale wasio na uwezo wa kugharamia matibabu.
“Wagonjwa
wanaogundulika kuwa na matatizo yanayohitaji upasuaji hupelekwa katika makao
makuu ya JKCI kwa hatua zaidi,” alisema Dkt. Waane.
Kwa
upande wake msimamizi wa tawi hilo Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo Dkt. Johnstone Kayandabila alieleza
kuwa kliniki hiyo pia inahudumia wagonjwa wa shinikizo la damu na kisukari.
“Tunahakikisha
kila mgonjwa anahudumiwa ndani ya muda mfupi bila usumbufu wa foleni. Muda wa
wastani wa matibabu ni saa mbili,”
alisema Dkt. Kayandabila.
Nao
Wagonjwa waliopatiwa huduma wameeleza kuridhishwa na ukaribu wa huduma, ufanisi
na usimamizi bora unaowezesha kupatikana
kwa matibabu ya mkazi haraka.
“Nimetibiwa
hapa baada ya kusikia tangazo redioni. Huduma ni bora, hakuna foleni na hali yangu
ya shinikizo la damu imeimarika,” alisema Khadija Ally
mkazi wa Mbagala.
Mohamed Baajun mkazi wa Mabibo aliongeza, “Tunashukuru kuona JKCI inasogea karibu nasi. Inatusaidia kupunguza gharama na kupata huduma bora bila usumbufu”.
Comments
Post a Comment