JKCI kufungua tawi DRC Congo
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI)
Dkt. Peter Kisenge akimpatia zawadi Gavana wa jimbo la Maniema la Jamhuri ya
Kidemokrasia ya Congo (DRC) Mhe. Mussa Kabwankubi Moise alipotembelea Taasisi
hiyo leo kwaajili ya kuona huduma zinazotolewa pamoja na kuangalia namna ya
kushirikiana na Taasisi hiyo kukuza huduma za moyo nchini Congo.
Balozi wa Tanzania katika nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya
Congo (DRC) Mhe. Said Juma Mshana akielezea dhumuni la ziara ya Gavana wa jimbo
la Maniema nchini Congo Mhe. Mussa Kabwankubi Moise alipotembelea Taasisi ya
Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) leo kwaajili ya kuona huduma zinazotolewa pamoja na
kuangalia namna ya kushirikiana na Taasisi hiyo kukuza huduma za moyo nchini
Congo.
Gavana wa jimbo la Maniema la Jamhuri ya Kidemokrasia ya
Congo (DRC) Mhe. Mussa Kabwankubi Moise akiwa katika picha ya pamoja na
viongozi kutoka nchini Congo na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI)
alipotembelea Taasisi hiyo leo kwaajili ya kuona huduma zinazotolewa pamoja na
kuangalia namna ya kushirikiana na Taasisi hiyo kukuza huduma za moyo nchini
Congo.
Na JKCI
**********************************************************************************************************
Taasisi ya Moyo Jakaya
kikwete (JKCI) imepanga kuvuka mipaka ya nchi na kufungua tawi katika Jamhuri
ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) kuimarisha ushirikiano baina ya nchi hizo mbili
katika kutoa huduma bingwa bobezi za matibabu ya moyo.
Hayo yamesemwa na Mkurugenzi
mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt Peter Kisenge wakati wa
ziara ya Gavana wa jimbo la Maniema la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC)
Mhe. Mussa Kabwankubi Moise alipotembelea JKCI leo jijini Dar es Salaam.
Dkt. Kisenge alisema
JKCI inataka kusogeza huduma za matibabu ya moyo kwa wananchi wa Congo kuwapunguzia
adha ya kusafiri umbali mrefu kwenda katika mataifa ya mbali kupata huduma
hizo.
“Tunawaahidi watu
kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kuwa tutatoa ushirikiano na kuwasaidi
wasitumie gharama nyingi ambazo wanazitumia kupeleka wagonjwa nje ya Afrika kwa
kuwasogozea huduma hizo karibu” alisema Dkt. Kisenge
Kwa upande wake Gavana
wa jimbo la Maniema la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) Mhe. Mussa
Kabwankubi Moise alisema baada ya kutembelea Taasisi hiyo ameridhishwa na uwekezaji
mkubwa uliofanywa na Serikali ya Tanzania na kuifanya JKCI kuwa kinara katika
utoaji wa huduma bingwa bobezi za upasuaji wa moyo Afrika Mashariki na kati.
“Nimevutiwa sana na
ubora wa huduma zinazotolewa na JKCI ni jambo la kujivunia kuona Taasisi ya Serikali
ikitoa huduma za kiwango cha juu namna hii”, alisema Mhe. Moise
Mhe. Moise aliongeza kuwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo itashirikiana na JKCI kwa kuwaleta wagonjwa waliokuwa wakipelekwa nje ya nchi kutibiwa ili waweze kupunguza gharama zinazotumiwa na Serikali hiyo kuwasafirisha watu wake kwa ajili ya matibabu ya moyo katika nchi za mbali.
Naye Balozi wa Tanzania
katika nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) Mhe. Juma Saidi Mshana aliipongeza menejimenti ya Taasisi hiyo kwa
kushirikiana vema na nchi ya Congo katika kuimarisha uhusiano mzuri uliopo
baina ya nchi hizo mbili.
Comments
Post a Comment