Viatu vyenye kisigino kirefu hatari kwa afya ya magoti.
Afisa
Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group Beatrice
Nangawe akitoa elimu ya afya bora kwa wafanyakazi
wa Bohari ya Dawa (MSD) wakati wa kambi maalumu ya siku mbili ya uchunguzi wa
afya iliyofanyika hivi karibuni katika ofisi za MSD Kanda ya Mabibo jijini Dar
es Salaam.
Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Mohamed Aloyce akimpa ushauri mmoja wa wafanyakazi wa Bohariy a Dawa (MSD) wakati wa kambi maalumu ya uchunguzi wa afya iliyofanyika hivi karibuni katika ofisi za MSD Kanda ya Mabibo jijini Dar es Salaam.
Daktari bingwa wa watoto wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Theophilly Mushi akitoa elimu kuhusu magonjwa ya moyo kwa wafanyakazi wa Bohari ya Dawa (MSD) wakati wa kambi maalumu ya uchunguzi wa afya iliyokuwa ikifanywa na wataalamu wa JKCI hivi karibuni katika ofisi za MSD Kanda ya Mabibo jijini Dar es Salaam.
Mtaalamu wa mazoezi tiba wa Taasisi
ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group Jackline Mariki akitoa elimu
kuhusu umuhimu wa afya ya viungo kwa wafanyakazi wa Bohari ya Dawa (MSD) wakati wa
kambi maalumu ya uchunguzi wa afya iliyofanyika hivi karibuni katika ofisi za
MSD Kanda ya Mabibo jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wafanyakazi wa Bohari ya
Dawa (MSD) wakifuatilia mada zilizokuwa zikitolewa na wataalamu kutoka Taasisi
ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakati wa kambi maalumu ya uchunguzi wa afya
kwa wafanyakazi wa MSD iliyofanyika hivi karibuni katika ofisi za MSD Kanda ya
Mabibo jijini Dar es Salaam.
Picha na: JKCI
****************************************************************************************************************************
Wanawake wametakiwa kuzingatia uvaaji wa viatu vyenye
kisigino kifupi kuimarisha afya ya miguu na kuepuka kuvaa viatu vyenye kisigino
kirefu ama kisigino flati ambavyo ni hatari kwa afya ya magoti.
Hayo yamesemwa na Mtaalamu wa mazoezi tiba kutoka Taasisi ya
Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group Jaqline Mariki wakati
akizungumza na wafanyakazi wa Bohari ya Dawa (MSD) katika kambi ya matibabu ya siku
mbili ya uchunguzi wa afya iliyofanyika katika ofisi za MSD Kanda ya Mabibo
jijini Dar es Salaam.
Jaqline alisema mtu anatakiwa kuvaa viatu vyenye kisigino kifupi
ili unyayo uweze kunyanyuka kidogo kusaidia ugawanyishwaji wa uzito kwenye
mwili hivyo kutoleta maumivu katika mwili.
“Tunashauri wanawake wasivae viatu virefu au vile ambavyo ni
flati bali wavae viatu ambavyo vina kisigino kifupi ili unyayo uweze kunyanyuka
kidogo, kwani uvaaji wa viatu vyenye kisigino kirefu unaweza kusababisha
ulemavu wa miguu”, alisema Jaqcline
Aidha, mtaalamu huyo alihimiza wafanyakazi kuwa na utamaduni
wa kunywa maji ya kutosha ili kuuweka mwili katika hali bora ya kiafya,
akieleza kuwa ukosefu wa maji mwilini unaweza kusababisha maumivu ya kichwa,
uchovu na kupungua kwa ufanisi wa kazi.
“Kama tunavyofahamu wafanyakazi wengi maofisini hawapendelei
kunywa maji mengi kwasababu muda mwingi wanautumia wakiwa wamekaa, jambo ambalo
linaweza kusababisha maumivu ya kichwa na kupunguza ufanisi wa kufanya kazi”,
aliongeza Jaqckline.
Kwa upande wao wafanyakazi wa Bohari ya Dawa (MSD)
waliopatiwa mafunzo hayo wameshukuru kwa kupatiwa uelewa mpana kuhusu afya ya
moyo, viungo vya mwili pamoja na matumizi sahihi ya dawa za kuzuia maambukizi
ya Virusi vya Ukimwi (VVU).
“Nilikuwa sifahamu kabisa kama ugonjwa wa homa ya ini unaweza
kusababisha saratani, kupitia mafunzo hayo nitahakikisha nakuwa makini kwa
kuchukua hatua ya kupima na kupata chanjo”, alisema Haika Regnald
“Binafsi mafunzo haya na upimaji huu ni fursa nzuri kwangu
kuweza kujua hali yangu ya moyo, kisukari na uzito kwani katika mafunzo haya
tumesisizwa kuwa na utamaduni wa kufanya mazoezi ya mara kwa mara” alisema Ally
Mlete.






Comments
Post a Comment