Dkt. wa JKCI kupewa tuzo kutoka American College of Cardiology - ACC
Chuo cha taaluma ya magonjwa ya moyo (American College of Cardiology
– ACC) cha nchini Marekani kutoa tuzo kwa daktari bingwa wa moyo wa Taasisi ya
Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Khuzeima Khanbhai.
Tuzo hiyo inatolewa baada ya kamati ya tuzo ya ACC kupokea
fursa za wanazuoni za Hani Najm Global ambao huwapa washindi fursa kubadilishana
ujuzi na wataalamu wenzao yatakayofanyika katika kliniki ya Clevaland iliyopo
Ohio’s.
Akizungumzia tuzo hiyo Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya
Kikwete (JKCI) Khuzeima Khanbhai alisema mbali na kupewa tuzo hiyo wakati wa
mkutano wa ACC utakaofanyika Chicago mwezi Machi mwakani pia atapata fursa ya
kushiriki mafunzo ya wiki nne yatakayotolewa katika kliniki ya Clevaland
iliyopo Ohio’s nchini Marekani.
“Fursa hii hutolewa kila mwaka kwa wataalamu wa magonjwa ya
moyo duniani ambapo mwaka huu tumepata nafasi wataalamu watatu nikiwemo mimi
kutoka nchini Tanzania”, alisema Dkt. Khuzeima
Dkt. Khuzeima alitoa shukrani zake kwa Chuo cha taaluma ya
magonjwa ya moyo (American College of Cardiology – ACC) kwa kumpa nafasi hiyo
ambayo inaenda kumuongezea utaalamu zaidi katika kutoa huduma kwa wagonjwa wa
moyo.
********************************************************************************************************
Comments
Post a Comment