Gambia kushirikiana na JKCI tiba ya matibabu ya moyo

 


Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Delilah Kimambo akiwatembeza katika baadhi ya maeneo ya Taasisi hiyo viongozi kutoka  Wizara ya Afya na wengine kutoka Taasisi ya Bima ya Afya ya Gambia walipotembelea taasisi hiyo kwaajili ya kujifunza na kuona uwekezaji uliowekwa na Serikali leo jijini Dar es Salaam.

Mkuu wa Kitengo cha Ubora wa Huduma wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Naiz Majani akiwaelezea namna ambavyo huduma zinatolewa kwa wagonjwa viongozi kutoka  Wizara ya Afya na wengine kutoka Taasisi ya Bima ya Afya ya Gambia walipotembelea taasisi hiyo kwaajili ya kujifunza na kuona uwekezaji uliowekwa na Serikali leo jijini Dar es Salaam.

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Delilah Kimambo akiwaonesha moja ya chumba cha VIP viongozi kutoka Wizara ya Afya na wengine kutoka Taasisi ya Bima ya Afya ya nchini Gambia walipotembelea taasisi hiyo kwaajili ya kujifunza na kuona uwekezaji uliowekwa na Serikali leo jijini Dar es Salaam.

Katibu Mkuu kutoka Wizara ya Afya nchini Gambia Dkt. Omar Jah akielezea lengo la ujio wa wataalamu kutoka nchini Gambia walipotembelea Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) leo kwaajili ya kujifunza na kuona uwekezaji uliowekwa na Serikali.

Katibu Mkuu kutoka Wizara ya Jinsia Watoto na Maendeleo ya Jamii nchini Gambia Roheyatou Kah akieleza namna alivyojifunza wakati ya ziara ya viongozi kutoka Wizara ya Afya na wengine kutoka Taasisi ya Bima ya Afya ya nchini Gambia walipotembelea Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) leo kwaajili ya kujifunza na kuona uwekezaji uliowekwa na Serikali.


Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Delilah Kimambo akielezea mafanikio ya taasisi hiyo kwa viongozi kutoka Wizara ya Afya na wengine kutoka Taasisi ya Bima ya Afya ya nchini Gambia walipotembelea JKCI kwaajili ya kujifunza na kuona uwekezaji uliowekwa na Serikali leo jijini Dar es Salaam.

Baadhi ya viongozi kutoka Wizara ya Afya na wengine kutoka Taasisi ya Bima ya Afya ya nchini Gambia wakisikiliza walipotembelea Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) leo kwaajili ya kujifunza na kuona uwekezaji uliowekwa na Serikali.


Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Delilah Kimambo akiwa katika picha ya pamoja na viongozi kutoka Wizara ya Afya na wengine kutoka Taasisi ya Bima ya Afya ya nchini Gambia mara baada ya kutembelea taasisi hiyo leo kwaajili ya kujifunza na kuona uwekezaji uliowekwa na Serikali.

Picha na: Khamis Mussa

*********************************************************************************************************************************************************************************************

Viongozi 15 wa ngazi ya juu kutoka Serikali ya Gambia wametembelea Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwaajili ya kuona huduma za matibabu ya moyo zinatolewa na kuangalia namna ambavyo nchi hiyo itashirikiana na JKCI katika matibabu ya moyo.

Viongozi hao waliotembelea taasisi hiyo leo iliyopo jijini Dar es Salaam  ni  makatibu wakuu, wenyeviti wa bodi, wakuu wa taasisi za afya na mamlaka za usimamizi wa afya za nchi hiyo .

Akizungumza mara baada ya kumaliza ziara ya kutembelea Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya ya nchini Gambia Dkt. Omar Jah alisema wako nchini kwaajili ya kujifunza mambo ya afya ikiwemo kuona huduma za matibabu ya kibingwa zinazotolewa pamoja na mifumo ya TEHAMA jinsi inavyofanya kazi.

Dkt. Jah alisema wameona jinsi Tanzania ilivyofanikiwa  katika mfumo wa bima ya afya  wamejifunza katika mifumo na kuona inavyofanya  kazi  pia wameona jinsi ambavyo huduma za kibingwa za matibabu mbalimbali zinavyotolewa

“Wenzetu hawa wa JKCI wako mbele katika tiba ya moyo tumekuja hapa ili kuona namna gani  tutashirikiana nao ili wawatume madaktari wao nchini kwetu kutoa huduma,tuwalete wanafunzi wetu waje kujifunza jinsi ya kutibu magonjwa ya moyo pamoja na kuwaleta wagonjwa wetu waje kutibiwa hapa kuliko kuwapeleka nje ya Afrika.

“Ushirikiano baina ya nchi za Afrika ni mzuri kwani ni rahisi na unaimarisha mahusiano kati ya nchi moja na nyingine  tumejifunza vitu vingi hivyo basi ninawaomba wataalamu  wa afya wa Tanzania waje kutembelea nchini kwetu naamini nao watajifunza kitu”, alisema Dkt. Jah.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt.Delilah Kimambo aliishukuru serikali kwa uwekezaji mkubwa ulioifanya ya kuwekeza   katika sekta ya afya hasa katika Taasisi hiyo jambo lililosababisha nchi nyingi kwenda kujifunza namna wanavyotoa  huduma za matibabu ya moyo pamoja na mafunzo wanayoyatoa.

“Leo hii tumepokea ugeni wa viongozi 15 kutoka nchini Gambia ambao wamekuja kujifunza katika Taasisi yetu,  tunaona faraja na furaha kuona nchi zingine zinakuja kujifunza Tanzania kuona namna  ambavyo serikali ilivyowekeza katika matibabu ya moyo pamoja na kuona kazi kubwa inayofanywa na wataalamu wetu”, alisema Dkt. Delilah.



Comments

Popular posts from this blog

JKCI na AICC Hospitali kutoa huduma za uchunguzi na matibabu ya moyo katika kikao kazi cha wenyeviti na watendaji wakuu wa Taasisi za Umma

JKCI yapata tuzo ya taasisi ambayo imetoa mchango wa kipekee kiuchumi na kijamii katika kuleta matokeo makubwa kwa kipindi cha mwaka 2023/2024

Maabara ya JKCI yapata ithibati ya kimataifa (ISO 15189:2012)