Bodi ya wadhamini yaipongeza JKCI kwa mafanikio

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akimkabidhi tuzo aliyekuwa Kaimu Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi hiyo Asha Izina wakati wa kikao cha mwisho cha Bodi hiyo kilichofanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akimkabidhi tuzo aliyekuwa mjumbe wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi hiyo Balozi Mwanaidi Maajar wakati wa kikao cha mwisho cha Bodi hiyo kilichofanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam.

Aliyekuwa Kaimu Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Asha Izina akimkabidhi tuzo aliyekuwa mjumbe wa bodi hiyo CPA Godfrey Kilenga wakati wa kikao cha mwisho cha Bodi hiyo kilichofanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi hiyo Dkt. Peter Kisenge

Aliyekuwa Kaimu Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Asha Izina akimpa mkono wa pongezi aliyekuwa mjumbe wa bodi hiyo Prof. Mohamed Janabi wakati wa kikao cha mwisho cha Bodi hiyo kilichofanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi hiyo Dkt. Peter Kisenge

Aliyekuwa Kaimu Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Asha Izina akimkabidhi tuzo aliyekuwa mjumbe wa bodi hiyo Adv. Haruni Matagane wakati wa kikao cha mwisho cha Bodi hiyo kilichofanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi hiyo Dkt. Peter Kisenge

Aliyekuwa Kaimu Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Asha Izina akimkabidhi tuzo aliyekuwa mjumbe wa bodi hiyo Abdulmalick Mollel wakati wa kikao cha mwisho cha Bodi hiyo kilichofanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi hiyo Dkt. Peter Kisenge

Aliyekuwa Kaimu Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Asha Izina akitoa neno la shukrani kwa viongozi wa Taasisi hiyo wakati wa kikao cha mwisho cha Bodi hiyo kilichofanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam. 

Mkurugenzi wa Fedha na Mipngo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Agnes Kuhenga akitoa taarifa ya fedha za taasisi hiyo wakati wa kikao cha mwisho cha Bodi ya Wadhamini wa JKCI kilichofanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam.

Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo kwa watoto na mwenyekiti wa kamati ya kuratibu fedha zinazotolewa kwaajili ya matibabu ya watoto Naizhijwa Majani akitoa taarifa ya fedha zilizokusanywa kwenye hafla ya gala dinner wakati wa kikao cha mwisho cha Bodi ya Wadhamini wa JKCI kilichofanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam.


Aliyekuwa Kaimu Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Asha Izina akiwa katika picha ya pamoja na waliokuwa wajumbe wa bodi hiyo na viongozi wa JKCI baada ya kumalizika kwa kikao cha mwisho cha Bodi kilichofanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam.

Na: JKCI

*************************************************************************************************

Bodi ya Wadhamini ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) iliyomaliza muda wake yajivunia kufanya kazi vizuri na uongozi wa Taasisi hiyo kuifanya kutambulika kimataifa.

Akizungumza wakati wa kikao cha mwisho cha bodi hiyo kilichofanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam aliyekuwa Kaimu Mwenyekiti wa Bodi hiyo Asha Izina alisema mafanikio yaliyopo JKCI yanatokana na ushirikiano mzuri uliopo pamoja na kujitoa kwa viongozi na wafanyakazi wote.

Asha alisema menejimenti ya JKCI imekuwa na hari ya kufikia malengo waliyojiwekea ili iweze kuwa tofauti na wengine jambo ambalo limefanikiwa kwa asilimia 100.

“Leo tunasimama tunajivunia kwa kipindi cha miaka mitatu tumeweza kufanya kazi nzuri katika taasisi hii na kuitambulisha ndani na nje ya nchi lakini pia tumeiweka katika hadhi yakimataifa”, alisema Asha.

Asha amewataka wafanyakazi wa Taasisi hiyo kuendelea kuwa na ushirikiano kwani bodi hiyo inaondoka ikiwa na matumaini ya kuendelea kuiona JKCI ikikuwa zaidi na isirudi nyuma.

“Bodi inawashukuru kwa ushirikiano mliokuwa nao twetu kwani hatujapata changamoto kufanya kazi na nyie, pale tulipokuwa tukikumbushana ilikuwa ni kwaajili ya kujenga na kuleta mafanikio katika taasisi yetu”, alisema Asha

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge alisema bodi hiyo imeleta mageuzi makubwa katika taasisi hiyo ambayo yameongeza weledi na mafanikio kwa nchi.

“Nimekuwa nikiiona taasisi hii tangu ilivyoanzishwa mwaka 2015, kwakweli ilipofikia sasa ni hatua kubwa sana imepiga na hii inatokana na ushirikiano uliopo kati ya Bodi, Menejimenti na wafanyakazi wote”, alisema Dkt. Kisenge

Dkt. Kisenge aliishukuru bodi ya wadhamini inayomaliza muda wake kwa kuwa na maono ambayo yameifanya taasisi hiyo kupiga hatua na kuweza kuongeza huduma za kibingwa bobezi kutolewa hapa nchini.

“Mnaweza msiyaone mafanikio tuliyofikia lakini waliopo nje wanatupongeza sana kwa hatua hii kubwa tuliyopo sasa hii yote inatokana na uongozi mzuri uliopo baina yetu”,

“Bodi hii ilivyoanza tulikuwa na tawi moja la Upanga lakini leo mnamaliza muda wenu tukiwa na matawi matatu ambayo ni Dar Group, Kawe na Oyster bay ambalo litafunguliwa wakati wowote mwezi ujao, nawashukuru sana”

Naye mjumbe wa bodi hiyo inayomaliza muda wake CPA Godfrey Kilenga aliwashukuru wajumbe wa bodi na menejimenti ya JKCI kwa ushirikiano waliouonyesha kupelekea kupata fursa mbalimbali za kuijenga na kuikuza.

CPA Kilenga alisema Taasisi ikifanya vizuri safa uenda kwa kila mtu na ikitokea ikafanya vibaya sifa mbaya zitaenda kwa kila mtu hivyo wao wanajivunia kuona wanapata sifa nzuri kutoka kwa wadau wa afya nchini.

“Ninahakika bodi mpya itakayokuja nayo mtaipa ushirikiano na kuweza kufanya nayo kazi vizuri, hii yote ni kwaajili ya kuijenga Tanzania yetu na kuifanya dunia kutujua katika sekta hii ya kutoa huduma za kibingwa za matibabu ya moyo”, alisema CPA Kilenga.


Comments

Popular posts from this blog

JKCI na AICC Hospitali kutoa huduma za uchunguzi na matibabu ya moyo katika kikao kazi cha wenyeviti na watendaji wakuu wa Taasisi za Umma

JKCI yapata tuzo ya taasisi ambayo imetoa mchango wa kipekee kiuchumi na kijamii katika kuleta matokeo makubwa kwa kipindi cha mwaka 2023/2024

Maabara ya JKCI yapata ithibati ya kimataifa (ISO 15189:2012)